RC Mtwara: Hali ya Mtwara ni shwari kabisa!

RC Mtwara: Hali ya Mtwara ni shwari kabisa!

Wana JF,

Naomba kupewa haki ya kikatiba kwa kupewa habari za huyu Bwana ambae kwasasa ni mkuu wa mkoa wa Mtwara Joseph Simbakalia

Juu ya ;
Uwezo wake kiutendaji kwa wale waliowahi kufanya nae kazi

Imani yake kwa MUNGU na watu wake kwa wale waliowahi/ wanaeishi nae kwenye pwani ile ya Mtwara

Wakubwa wa Magogoni wanamuonaje kuwa ni mtetezi wao ama ni mtetezi wa Taifa zima ?

ANGALIZO;
Alishawahi kuwaita wana Mtwara Wahaini na Wahuni juu ya namna wanavyodai haki zao.

The Fixer,

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Col (rtd) Joseph Simbakalia kwangu mimi ni mtendaji mzuri. Akiwa Col. Jeshini alipewa jukumu la kuongoza NDC wakati huo ikiwa hoi. Ni mwasisi wa Mradi wa Mtwara Corridor wakati wa utawala wa Mkapa. Pia ni mtaalam wa mambo ya Private Public Partnership. Nadhani alipelekwa Mtwara tokea Kigoma ili akaendeleze mipango yak eile ya NDC kuhusu mambo ya Mtwara Corridor.
 
Hilo jina la kuitwa wahuni ni sahihi wewe unafikili unafanya fujo za kijinga unataka uitweje,wewe mtu mzima hovyo umekaa kiuchochezi hata huna aibu jifunze kutoa elimu kwa watu kwa lengo la kuisaidia jamii na wala siyo kuchochea vurugu.
 
Hilo jina la kuitwa wahuni ni sahihi wewe unafikili unafanya fujo za kijinga unataka uitweje,wewe mtu mzima hovyo umekaa kiuchochezi hata huna aibu jifunze kutoa elimu kwa watu kwa lengo la kuisaidia jamii na wala siyo kuchochea vurugu.

We kweli kibwete, ki kwetu kibwete ni kabaang
 
Hilo jina la kuitwa wahuni ni sahihi wewe unafikili unafanya fujo za kijinga unataka uitweje,wewe mtu mzima hovyo umekaa kiuchochezi hata huna aibu jifunze kutoa elimu kwa watu kwa lengo la kuisaidia jamii na wala siyo kuchochea vurugu.

Diiiiiih !
Yaaaani siku hizi hata kuomba kufahamishwa juu ya jambo flani ni UCHOCHEZIII.....!???

Ama kweli Kiswahili kimekuwaa...
 
SUNDAY, JANUARY 27, 2013

COL. (RETD) SIMBAKALIA FORESAW MTWARA UPRISING?



"Mtwara Region is poised to become the new growth pole of Tanzania, based on the exploitation of world class resources of natural gas and industrial minerals. Local communities do not have a skills base which would immediately qualify its people to be considered for employment in the new start-up mega projects. Therefore, without deliberate and planned interventions by Government and other stakeholders, the high trajectory growth envisaged to take place in Mtwara region will exclude local population and create an atmosphere of resentment and animosity to investment in the local communities" - Col. (Retd) Joseph Leon Simbakalia, Regional Commissioner of Mtwara, on The Role of Regional Administration and Local Government in Influencing Inclusive Growth Strategies: The Case of Mtwara Region
<http://esrf.or.tz/docs/TheRoleofRegionalAdministration.pdf>


 
Licha ya vurugu na patashika iliyotokea leo na inayoendelea katika viunga mbalimbali vya mji wa Mtwara, Mkuu wa Mkoa huo Bw.Joseph Simbakalia amezungumza na Wapo Radio jioni ya leo akisema kwamba kwa siku nzima ya leo Mtwara hali ilikuwa,
shwari kabisa na changamoto zilizotokea ni za kawaida tu.

SOURCE: Wapo Radio.
kwa kuwa nyumba yake inalindwa na polisi wenye silaha kali, viongozi wa ccm ndio walivyo usalama ni kwao sio kwa watu wengine
 
Simba kalia endelea na msimamo wako hao wahuni wasikutishe huwezi kuvumilia wahuni.
 
Mkuu,
Maelezo yako yana nusu ukweli na nusu uwongo kabisa.

Ni kweli kwamba Simbakalia alipewa nishani na Papa Benedict wa 16 mwaka jana. Sababu ya kupewa nishani haikuwa kwaajili ya kustawisha kanisa Mkoani kwake, huu ni upotoshaji miongoni mwa wanajamvi.
Ni hatari sana kuandikia au kuelezea kitu usichojua kabisa, ambapo ni sawa na kumwaga sumu kwenye reservoir-tank la mji, maana utaua watu wengi kama si wote.

Kanali Simbakalia alitunukiwa nishani na Papa kutokana na kuwa Mlei Bora wa Mwaka.
Mlei ni Mkristo Mkatoliki ambaye hayuko kwenye daraja la Utume au upakwa mafuta, au kwa maana ingine si Padri au Sista na madaraja mengine ya juu...ni Mkatoliki wa kawaida kabisa.
Vatican ina utaratibu wa kutoa nishani kwa Mlei popote duniani endapo ataonekana kuishi maisha yanayompasa mlei, ikiwa ni pamoja kujitoa kwa ziada katika huduma kwa kanisa. Simbakalia alichaguliwa kwa vigezo hivyo, na si kwa kustawisha kanisa Mkoani Kigoma kama ambavyo post ya hapo juu inavyotaka kuwapeleka watu chakani.

Nadhani nimeeleweka!

Kama mpewa nishani ndiye aliyesema "hali ya mtwara jana ilikuwa shwari basi amemfanya "papa" kuwa dhalili, tutajiuliza maswali mengi likiwemo "michakato kanisa katoliki huendeshwa kwa rushwa?"
Kwa kauli alizotoa huyu simbakalia sidhani kama anapaswa kuwa balozi wa kanisa hata kwa historia.
 
Akiwa Col. Jeshini ,Pia ni mtaalam wa mambo ya Private Public Partnership.

Kumbe Mdau ni Full Col. Mtaalamu pia wa katika medani za kuwa partner ??

Sasa yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi ya Mkoa yaaani ameshindwa kabisa kukaa na hawa jamaa / Wadau wooote wa Mtwara na KUMSHAURI MKUU WA NCHI ( RAIS ) namna bora zaidi ya kusonga mbele bila kumwaga damu kwenye Uvunaji na Unufaikaji wa RASILIMALI ZETU wenyewee...??

Kweli ameshindwaa ??
 
Kwani si ndo ofisi yake imechomwa? Iweje aseme hali ni shwari? Ama mpaka wakachome na anakoishi ndo ataamini hali si shwari
 
We kweli kibwete, ki kwetu kibwete ni kabaang
Huna tofauti na mazoea mitomingi,mambo ya kwenu mi yananihusu nini baki nayo huko kwenu sitaki uhusiano na makabila ya ajabu yanayochochea vurugu watu wafe.
 
RC pengine angesema kuwa serikali inafanya kila jitihada ili Mtwara irudi kwenye hali yake ya kawaida. Lakini kusema kuwa hali ni shwari ni sawa na kuifanya Tanzania ionekane kama nchi ya 'Comical Ali'. Karibu Balozi za nchi zote za Magharibi zimeshatoa security warninga kwa wananchi wao wasitembelee Mtawara, na sababu kubwa waliyotoa ni vurugu. Sasa bwana RC kwanini anajitahidi kidogo kudodosa huku na huko kabla ya kutoa hizi habari za kimagumashi?

Kuna namna ya kufunika mambo lakini sio kwa mtindo huu. Walau taarifa iwe na chembe chembe za uhalisia na sio huu utani.

anaakili za mtope huyo ndugu yenu.
 
Ushauri wangu kwa simba kalia atumie jeshi tena risasi za moto ndizo zitumike hakuna haja ya kubembeleza wahuni.
 
Kumbe Mdau ni Full Col. Mtaalamu pia wa katika medani za kuwa partner ??

Sasa yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi ya Mkoa yaaani ameshindwa kabisa kukaa na hawa jamaa / Wadau wooote wa Mtwara na KUMSHAURI MKUU WA NCHI ( RAIS ) namna bora zaidi ya kusonga mbele bila kumwaga damu kwenye Uvunaji na Unufaikaji wa RASILIMALI ZETU wenyewee...??

Kweli ameshindwaa ??

Siamini kama suala ni kwa Col. Joseph Simbakalia kushindwa kutatua hili tatizo. Hili tatizo lina mambo mengi ndani yake. Kama kushindwa si kwa Simbakalia peke yake watakuwa wameshindwa wengi. Col. Simbakalia alienda Mtwara wakati mipango yote ya uchimbaji na usafirishaji gas imeishakuwa tayari. Hapa nadhani wanasiasa wetu wameshindwa kuwaandaa wana Mtwara kwa ajili ya Mradi huu na kuna majungu na uchochezi mwingi kuhusu mradi. Hivi ni kweli kabisa kwamba watu wa Mtwara hawataki gas itoke Mtwara? Mita zote hizo za ujazo watazifanyia nini? Wanatakiwa waelimishwe lakini kuna watu badala ya kuwaelimisha wanawachochea wafanye vurugu. Vurugu haina tija kwa Mtwara wala Tanzania. Haiwezekani kwamba gas iwe Mtwara tu wakati sehemu zingine za nchi zinaiihitaji. Barabara na Daraja la Mkapa ambalo ni kiuongo muhimu cha watu wa kusini na mikoa mingine havikujengwa kwa gas bali kwa rasilimali toka sehemu zingine za nchi.

Tanzania ni yetu sote na gas ni ya Tanzania.
 
Kimbunga anawahusudu sana wajeshi wenzake!

Hapana mkuu Companero Ila tu ni kwamba huyu Col. Joseph Simbakalia ni mweledi na ni zaidi ya mwanajeshi. Si hata wewe umeona machapisho yake ya kiutafiti! Kwa kiswahili cha sasa mimi nasema ni JEMBE! Col. Simbakalia ni type ya akina Prof. Maj. Gen. Yadon Kohi yule aliyekuwa COSTECH
 
Siamini kama suala ni kwa Col. Joseph Simbakalia kushindwa kutatua hili tatizo. Hili tatizo lina mambo mengi ndani yake. Kama kushindwa si kwa Simbakalia peke yake watakuwa wameshindwa wengi. Col. Simbakalia alienda Mtwara wakati mipango yote ya uchimbaji na usafirishaji gas imeishakuwa tayari. Hapa nadhani wanasiasa wetu wameshindwa kuwaandaa wana Mtwara kwa ajili ya Mradi huu na kuna majungu na uchochezi mwingi kuhusu mradi. Hivi ni kweli kabisa kwamba watu wa Mtwara hawataki gas itoke Mtwara? Mita zote hizo za ujazo watazifanyia nini? Wanatakiwa waelimishwe lakini kuna watu badala ya kuwaelimisha wanawachochea wafanye vurugu. Vurugu haina tija kwa Mtwara wala Tanzania. Haiwezekani kwamba gas iwe Mtwara tu wakati sehemu zingine za nchi zinaiihitaji. Barabara na Daraja la Mkapa ambalo ni kiuongo muhimu cha watu wa kusini na mikoa mingine havikujengwa kwa gas bali kwa rasilimali toka sehemu zingine za nchi.

Tanzania ni yetu sote na gas ni ya Tanzania.

Hata kama Gas ni kwa manufaa ya Taifa zima, Ukiishi karibu na UWARIDI lazima unukie - John ( Jumanne ) S. Malecela
 
Back
Top Bottom