RC Mtaka yupo sahihi. Ni kweli kabisa viongozi wetu hawana uchungu na elimu ya watoto wetu

Kanamusi

Member
Apr 9, 2020
22
65
Pamoja na approach aliyoitumia ila alichokisema RC antony mtaka ni ukweli uliochelewa kusemwa kwa sababu ni kwa miaka mingi sana elimu yetu imekuwa ikifanyiwa siasa na kuharibiwa na viongozi tuliowapa dhamana ya kuisimamia.

Mara kadhaa kumekuwa kukitolewa matamko yasiyo na kichwa wala miguu kuhusiana na elimu yetu na hakuna anayehoji, matokeo yake tumeacha wanasiasa ndio wawe waamuzi wa mwisho wa hatma ya maisha ya watoto wetu katika suala zima la elimu na mbaya zaidi viongozi hao hawana uchungu wowote kwa sababu watoto wao hawasomi shule zetu hizi za kata almaarufu kama shule za yebo yebo.

Ni juzi tu nimetoka kumsikia waziri wa TAMISEMI ambaye amepewa dhamana ya kusimamia elimu ya msingi na sekondari akisema wamemaliza tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi mashuleni.

Kwa kauli hiyo ya waziri kama mtu una uchungu na elimu unaweza kujikuta unatumia lugha ngumu kama aliyotumia Antony Mtaka kukemea uongo huo. Kwa sababu sisi wazazi tunaosemesha watoto wetu kwenye hizi shule za kata ndio tunajua adha wanazopata watoto wetu ikiwemo kukosa vipindi kwa sababu ya kutokuwa na walimu wa sayansi lakini waziri anatoka usingizini na kulipuka kwamba tatizo la walimu wa sayansi limekwisha. Hivi waziri kama huyu unaweza kusema ana uchungu kweli na elimu ya watoto wetu?

Leo kama taifa tunajadili na kutenga bajeti ya kujenga sanamu lakini wakati huo huo shule zetu hazina walimu wa kutosha na wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa madawati. Sasa tujiulize hivi hilo sanamu lina tija gani kwa taifa kwanini hiyo bajeti isipelekwe kwenye shule zetu kutatua hata changamoto ya madawati ili watoto wetu wasome katika mazingira rafiki yaliyo boreka?

Waziri wa elimu naye yupo yupo tu hana habari ni kama hana kazi ya kufanya kwa sababu majukumu yote ya kielimu kwa sasa yanafanywa na Tamisemi ambayo ipo chini ya Rais labda ndio maana elimu inafanyiwa siasa kwa sababu jambo lolote la kuboresha elimu mfano kuajiri walimu kwenye shule zetu ni hadi Rais atolee matamko kwenye majukwaa ya kisiasa jambo ambalo ni hatari sana kwa ustawi wa elimu yetu.

Sasa kwa mambo kama haya kwa mtu ambaye yuko well committed na suala la elimu lazima atajisikia uchungu na kutumia lugha ngumu kufikisha ujumbe kwa viongozi labda ndipo wataamka na kuchukua hatua stahiki za kuboresha elimu ya watoto wetu.

Kwa hili nasimama na RC Mtaka kwa 100%.
 
Kuna baadhi ya nchi kiongozi lazima watoto wake wasome shule za serikali.

Sikumbuki vizuri ni mwaka gani lakini kuna waziri mmoja Uingereza alikosolewa vikali kumpeleka mwanae shule binafsi, akajitetea mtoto wake alikua na ulemavu uliohitaji uangalizi wa karibu. Hata hivyo ikaja hoja kwamba kwanini serikali wasiwe na shule za aina hiyo kwakua watoto wenye hayo matatizo wapo wengi?

Waliweka hivyo ili kuweka msisitizo wa viongozi kuona umuhimu wa kuboresha huduma za umma.
 
Nchi hii inashindwa kupiga hatua inayotakiwa kimaendeleo kwa sababu ya hawa wasomi wetu wenye vyeti lukuki, huku wakikosa kabisa maarifa vichwani mwao! Ndalichako tangu aingie kwenye siasa, amepoteza kabisa ule weledi aliokuwa nao enzi zile akiwa Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa!

Hivyo wakiendelea kupigwa ngumi za uso, watapunguza huu ujinga wao wa kutuendesha kama magari mabovu. Nitapenda kuona wakina Mtaka wa aina nyingi kuanzia sasa.
 
Elimu inaendeshwa kwa sera na sheria.

Waziri yuko pale kusimamia sera hizo na kuagiza zifuatwe.

Huyo mtaka ni mlevi tu ambaye hajui mipaka yake ya kazi.
 
Elimu inaendeshwa kwa sera na sheria.

Waziri yuko pale kusimamia sera hizo na kuagiza zifuatwe.

Huyo mtaka ni mlevi tu ambaye hajui mipaka yake ya kazi.
Huna hoja wewe! Zaidi ya kuwashwashwa tu na kuweweseka. Na kama ndiyo umetumwa na huyo Ndalichako wako, basi atakuwa amekosea sana kukuchagua wewe.

Maana hata hujielewi! Kule kwenye ule uzi wako uchwara, umemtuhumu Mtaka kama mtu mpenda sifa, amenunua watu mitandaoni ili wamsifie! Hapa unasema Mtaka ni mlevi tu ambaye hajui mipaka yake ya kazi!!

Mipasho tu ndiyo iliyokujaa!
 
Nina maneno mawili tu kwenu ninyi watanzania "ACHENI UNAFIKI". Antony Mtaka yupo sahihi. Nchi hii imekuwa ya hovyo kwa sababu ya unafiki wa raia wake. Mitanzania imekaa kama mizombi hivi. Imekalia kujipendekeza tu ili kushibisha mitumbo yao haijali kabisa maslahi mapana ya nchi. Mijitu imekalia kusifia sifia tu hata pale pasipostahili kusifia.

Akijitokeza mtu wa kusema ukweli na kuyaongea matatizo halisi tuliyonayo kama nchi inatokea minafiki inaanza kulaumu mpaka unajiuliza hii mijiti ni binadamu au misukule tu? Ina maana haina hata aibu? Nchi hii ipo katika hali hii kwa sababu ya unafiki wa hii mitanzania. Kariakoo imeteketea kwa moto kwa sababu ya unafiki wa hii mitanzania. Dar es salaam mifoleni kibao kwa sababu ya unafiki wa mitanzania.

Matatizo kibao tunayo hapa nchini lakini kwa unafiki yapo kimya ila akitokea mtu akayaongea kinagaubaga hayo matatizo minafiki inaanza kupinga kwa kujipendekeza. Nani asiyejua shule zetu nyingi za serikali hazina hata waalimu wa masomo ya sayansi na hesabu.

Mtaka kaongea ukweli mtupu tena wenye lengo la kuwasaidia watoto wetu wanaotoka kwenye familia fukara lakini minafiki inakuja kupinga kwa kujipendekeza ili kushibisha mitumbo yao.

Viongozi wanatembelea maviete ya milioni 500 huko wakati kuna watoto wanasomea chini ya miti, wakati kuna madarasa ya udongo na yasiyokuwa na madawati lakini hii minafiki haioni kama hili ni tatizo. Kuna sanamu la milioni 450 linataka kujengwa wakati vijiji vingi havina maji ya kunywa halafu kuna takataka zinatetea hili sanamu.

Watanzania acheni unafiki. Tusiwavunje moyo viongozi wanaotetea watanzania maskini. Nchi hii ina matatizo kibao yaliyosababishwa na viongozi wetu watetea matumbo yao. Tunapopata viongozi wenye kaliba kama Mtaka inatakiwa tuwatie Moyo.
 
Hujazuiwa kufunga ndoa na Mtaka. Songa mbele! Tunaomjua tangu vyuoni, tunafahamu akili yake inalenga nini.
 
Wajinga, wapumbavu, wa.sh.enzi na wanafiki ndiyo wanaona na kusema anthony amekosea.

Wale wanaosomesha watoto shule binafsi unakuta wazazi wanalipa ada 3mil lakini wanapoambiwa waongeze ili madarasa ya mitihani (std four,seven, form two, four, six) wafundishwe muda wa ziada wazazi wanatoa pasipo hiyana.

Watoto shule binafsi madarasa ya mitihani wanafundishwa kuanzia saa 12 au saa moja alfajiri hadi saa 10, kisha saa moja-saa nne supervised prep jtatu mpaka ijumaa. Jumamosi wako darasani nusu siku, jumapili supervised prep. Na unakuta watoto wote wako boarding.

Kisha tunamponda Mtaka tunashabikia upuuzi wa waziri
 
Back
Top Bottom