RC Makalla: Machinga wote Dar walio katika hifadhi ya barabara, Wataondolewa na vibanda vyao kuanzia Septemba 13, 2021

Niombe chama tawala kwa dharura waingilie kati swala la hawa wamachinga wanaopambani haki zao wakiwa uchi hapo Kariakoo.

Nadhani RC Makalla hajaeleweka vizuri hivyo chama kiingilie kati kuokoa jahazi.

cc: Mzee Mgaya
Akili fupi Makala toa takataka hizo
 
Sioni mafanikio kwenye haya maamuzi. Wizi, na vurugu vitaongezeka kwa haraka sana.

Wangeanza kutenga machinga streets ndani ya Kariakoo huko huko na Posta ili maeneo mengine yaachwe bila vurugu.
 
Tatizo huyu mkulu matamko mengi, utekelezaji zero. Tungoje hili labda litatekelezwa.
 
Leo hii umegeuka reporter wa ccm
Hakika kazi ya ccm imeonekana
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla ameingia Kariakoo kwa kutumia basi la Mwendokasi (haijulikani alikotokea) na kutoa Maagizo kwamba baada ya siku 7 njia zote za watembea kwa miguu kwenye eneo hilo ambazo zimejaa wamachinga, mama lishe, wachoma mihogo na wauza Alikasusi ziwe wazi.

Haijulikani ni wapi wamachinga hao watapelekwa.

=======

View attachment 1930594

RC MAKALLA: MARUFUKU MACHINGA KUFANYA BIASHARA KWENYE NJIA ZA WATEMBEA KWA MIGUU.

- Asema agizo hilo ni kwa Wafanyabiashara Mkoa mzima.

- Amtaka DC Ilala na Uongozi wa Machinga kuweka utaratibu mzuri kuwapanga Machinga Kariakoo.

- Awapo mbinu ya kufunga baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya Biashara.

- Wamachinga wakiri kuingilia maeneo ya watembea kwa miguu na kuahidi kuhama.

- Aeleza dhamira yake ya kuboresha mandhari ya Dar es salaam.

View attachment 1930596


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amepiga marufuku ufanyaji wa Biashara Kwenye maeneo hifadhi ya barabara zote za Mkoa huo baada ya utaratibu huo kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani na ongezeko la ajali.

RC Makalla
ametoa maelekezo hayo alipotembelea Soko la Kariakoo na kujionea Kero ya Ufanyaji biashara holela Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.

Kutokana na hilo RC Makalla amewaelekeza Mkuu wa Wilaya ya Ilala kufanya kikao na Wafanyabiashara hao Jumatatu ya *September 13 na kuainisha maeneo ya kuwapeleka wote waliovamia hifadhi ya Barabara.

Aidha RC Makalla amewaelekeza Kuangalia utaratibu mzuri wa kufunga na kufungua baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya biashara Kutokana na ufinyu wa maeneo ili Waweze kupata riziki.

Hata hivyo RC Makalla amesema kwa tathimini aliyofanya amebaini Hali ya Ufanyaji biashara holela Dar es salaam ipo kwa kiwango kikubwa na kuwanyima watembea miguu haki zao za msingi.

Pamoja na hayo RC Makalla ameelekeza Manispaa zote za Mkoa huo kuweka Vibao vya kuzuia biashara Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.

View attachment 1930600
 
Mwendazake alituachia msala mkubwa sana, dar, mwanza, Arusha, Mbeya ni kero sana hata hamu ya kwenda kufanya manunuzi haipo tena

Wewe unafikiria kwa nini ilifikia hapa na mpaka akawapa vitambulisho vya 20,000/-? Sasa'asitokee mtu akataka kujisahaulisha haya. RC Makalla anatakiwa ajue anapowaondoa anawapeleka wapi kwenye wateja? Waelimishwe waelewe faida ya wao kuhamishwa wanapo hamishiwa na hiyo faida iwepo kweli isiwe ni nadharia tu. Wawahamishe kwa awamu na wale wanaobaki wakisubiria kuhamishiwa mahali mwafaka wajiridhishe wenzao ambao wameshahama maisha yanaendelea. Hii ndio moja ya kazi ya kiongozi kuonesha njia ya suluhisho la matatizo ya unaowaongoza. Vinginevo ikitumika nguvu kwa vile iko tutarajie majanga.
 
Walipe kodi inayostahili kutumia kuboresha vitambulisho vyao wataondoka wenyewe
 
Safi sana, kimsingi Kariakoo kwa sasa inapaswa ihamie Maeneo ya MBEZI MWISHO, STENDI YA MAGUFULI.

JIJI la DSM ljnapaswa lipanuke, tubadilike, wataalamu wa mipango miji wapo lkn hawataki kutumia taaluma zao vyema.
Mkuu kimsingi machinga biashara zao ni za kutembeza, hao wenye vibanda vya damu ya mzee ni wafanya biashara kama wafanyabiashara ambao wamepanga kwenye myumba za watu na wengine wana mali za mtaji mkubwa tu ila wanakwepa kulipa kodi, pango za kupangisha nyumba nk. Mfano utawakuta wengine wanakonteina la vinywaji (bia, soda nk) lenye mtaji mkubwa na anauza kuliko mwenye leseni ya bar ambaye analipa pango la nyumba ya biashara. Machinga feki mwingine utamkuta ana kakibanda chake cha bati ngumu amejaza spea za magari zenye mtaji mkumbwa kuwashinda hata wale wanaouza spea ambao wanalipa kodi zote. Ni wakati sasa wa TRA kuwatambua watu hawa. Kwa lugha ya kiuchumu ni kwamba utitiri huu wa wajasiliamali waliojibatiza jina la wamachanga ili wakwepe kulipa kodi za Serikali ni wengi sana ndio wanao sababisha Serikali kukosa fedha za kodi maana hawa ni wengi na halipi kodi. Serikali iwajengee sehemu za biashara ili walipe kodi, wapo wengi hivyo makusanyo ya kodi yatakuwa makubwa sana ili iwe mbadala wa hizi TOZO
 
Pale Mbezi maeneo ya CRDB Jamaa wakaona haitoshi wameamua kuweka mabanda yao barabarani kabisa. Magari ndiyo yanafanya kukwepa biashara zao.
Mkuu Mbezi inatisha kwa hawa watu, wamevamia kwelikweli utazani Mbezi kuna machimbo ya madini. Imepabwa na vibanda vyenye maturubai chakavu/mabovu. Ukiwaangalia kwa haraka haraka utadhani wamepewa vibali vya kuendesha biashara sehemu hizo.
 
Makalla akifanikiwa baada ya hiyo wiki alkiyotoa basi nitamnunulia beer.....
na nyamachoma count on me, hili ni jambo gumu sana kiutekelezaji maana limelelewa awamu kwa awamu na limekua sugu, linahitaji sera ya kitaifa na kuungwa mkono na serikali yote na wapenda ustaarabu.

Kila la heri Makalla, mwenyekiti chake akitengua maagizo haya kwa simu tu umeumia, si unajua ni msikivu na huwa anasikiliza zile huziita "kelele"?!
 
Usidanganyike wewe.

Machinga ndio wapiga kura wa CCM na wako kimkakati.

Subiri tamko kutoka juu kwamba Machinga wasibughuziwe!
Machinga hawajawahi kuwa wapiga kura wa mtu yeyote yule, aliyesema machinga ni wapiga kura wake alitafuta kushangiliwa tu.

Kura za CCM zipo vijijini si kwa wamachinga. Kuendelea kuwalea kwa kudhani ni wapiga kura ni kujidanganya.
 
Back
Top Bottom