Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,447
- 7,823
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anaongelea mambo mbalimbali kuhusu mkoa wa Dar. Miongoni ni suala la wamachinga na kupoa kwa Serikali baada ya kutoa tangazo la kuwaondoa. RC Makala amesema kwasasa wameweka kipaumbele kwenye kutoa elimu na anaamini hawatafika kwenye kutumia nguvu.
RC Makala: Ili kuboresha usafi jiji la Dar lazima tudhibiti ufanyaji biashara holela hivyo nikaona kuna haja ya kuwasaidia watu wetu sio kuwaondoa. Watu kwenye mfereji wameweka zege na kuweka kibanda juu yake, ukiziba?
Tumeanza kuweka vibao, usifanye biashara hapa! Nitoe wito kwa wafanyabiashara, ukiona vibao hivyo usifanye biashara.
Naendelea kutoa elimu, niwaombe mahali kote ambao kumewekwa vibao sio eneo la kufanya biashara. Masoko yako na hayana watu.
RC Makala: Ili kuboresha usafi jiji la Dar lazima tudhibiti ufanyaji biashara holela hivyo nikaona kuna haja ya kuwasaidia watu wetu sio kuwaondoa. Watu kwenye mfereji wameweka zege na kuweka kibanda juu yake, ukiziba?
Tumeanza kuweka vibao, usifanye biashara hapa! Nitoe wito kwa wafanyabiashara, ukiona vibao hivyo usifanye biashara.
Naendelea kutoa elimu, niwaombe mahali kote ambao kumewekwa vibao sio eneo la kufanya biashara. Masoko yako na hayana watu.