Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 944
KOMREDI MWAJABU MBWAMBO AONGOZA UWT MKOA WA DAR ES SALAAM KUTEMBELEA IHSAN ORPHANAGE CENTER KIGAMBONI-KIBADA
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Dar es salaam ukiongozwa na Mwenyekiti UWT Komredi Mwajabu Rajabu Mbwambo wameshirikiana na Uongozi wa UWT Kata Kibada kutembelea kituo cha kulelea watoto Yatima Ihsan Orphanage Center kilichopo Kata ya Kibada Tawi la Kiziza.
Ziara hiyo ya tarehe 27 Januari, 2024 iliambatana na kufanya Dua ya kumuombea Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika siku yake ya kuzaliwa na kutimiza miaka 64 na kuombea Taifa zima kwa ujumla na kutoa mahitaji muhimu kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho na kumkabidhi Mlezi wao Bi. Hidaya.
UWT Imara
Jeshi la mama Samia
Kazi Iendelee