Baada ya stori kuenea kwamba Mwigizaji RAY anahusika moja kwa moja na kifo cha mwigizaji STEVEN KANUMBA, mwigizaji huyo amezungumza yafuatayo kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM.
Amesema "Nimekua nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambae simfahamu anaitwa Mange Kimambi"
"Alikua ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Osterbay kwamba Ray ndio aliepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba, Mungu ndie anaejua" – Ray
Amesema "Nimekua nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambae simfahamu anaitwa Mange Kimambi"
"Alikua ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Osterbay kwamba Ray ndio aliepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba, Mungu ndie anaejua" – Ray