#COVID19 Ramaphosa: Hakuna sababu za Kisayansi za kuweka marufuku ya kusafiri kwa nchi za Kusini mwa Afrika

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ametoa wito kwa nchi za Ulaya na Marekani zilizoweka vikwazo vya usafiri kwa Mataifa ya Kusini mwa Afrika yaliyobainika kuwa na maambukizi ya aina mpya ya Virusi vya Corona kuondoa vikwazo hivyo.

Katika hotuba yenye urefu wa dakika 29, Rais Ramaphosa amesema kugundulika kwa aina ya kirusi cha Omicron kunatokana na ufanisi na juhudi za Wataalamu wa Afya nchini Afrika Kusini.

“Marufuku ya Usafiri kwa Mataifa ya Kusini mwa Afrika iliyowekwa haina uhalali wowote na inaongeza ubaguzi kwetu na kwa nchi za Kusini mwa Afrika na haisaidii kuzuia madhara ya maambukizi ya virusi bali inaongeza maumivu ya kiuchumi katika nchi zetu.

“Natoa wito kwa mataifa hayo kuondoa marufuku ya kusafiri haraka kabla madhara ya kiuchumi kwa nchi zetu na madhara kwa maisha ya wananchi hayajatokea zaidi. Hakuna sababu zozote za kimsingi za Kisayansi za kuweka marufuku hiyo.

“Tunafahamu kuwa virusi hivi, kama aina nyingine ya virusi vya corona, hubadilika na uwezekano wa kutokea kwa aina nyingine yenye nguvu zaidi ya virusi hivi ni mkubwa,” alisema Rais Ramaphosa.

Rais Ramaphosa amesisitiza pia kuwepo usawa wa chanjo kwa nchi zinazoendelea, akisema madhara ya virusi vya corona yanaweza kupunguzwa ikiwa wananchi wengi wa nchi zinazoendelea watapata chanjo.

Kirusi cha corona cha B.1.1529 kilichopewa jina Omicron kilitambuliwa nchini Afrika Kusini Novemba 26, na tayari kimekwisha sambaa katika nchi kadhaa za Ulaya, Australia na Asia.

 
Mzungu ndio ana lazima ya kuja Africa

Sio mwafrika ana lazima ya kwenda Ulaya

Siku tukilitambua hili tutawatawala hao mabeberu
Upo sawa endapo tu,

Tafsiri ya maendeleo haitahusisha teknolojia, mashine za kisasa, Elimu ya sayansi na yafananayo na hayo. Tafsiri ya maendeleo iwe ni kulima mpate chakula basi.

Afrika inajivunia jambo moja tu: Ardhi yenye rutuba rafiki kwa mali asili, kilimo, gesi, mafuta na mawe yenye thamani.

Afrika ina udhaifu mmoja mkubwa: Uwezo wa teknolojia na akili ya kunufuaika na mali asili, kilimo, gesi, mafuta na mawe ya thamani.
 
Upo sawa endapo tu,

Tafsiri ya maendeleo haitahusisha teknolojia, mashine za kisasa, Elimu ya sayansi na yafananayo na hayo. Tafsiri ya maendeleo iwe ni kulima mpate chakula basi.

Afrika inajivunia jambo moja tu: Ardhi yenye rutuba rafiki kwa mali asili, kilimo, gesi, mafuta na mawe yenye thamani.

Afrika ina udhaifu mmoja mkubwa: Uwezo wa teknolojia na akili ya kunufuaika na mali asili, kilimo, gesi, mafuta na mawe ya thamani.
Ni sawa pia,
Ila wengi wetu tunaenda kuficha mali tuliyoiba, kujenga na kuwekeza, na labda kutembea na mambo kama hayo yasiyo na tija sana, lau tungewekeza huku na kusimamia demokrasia na haki ya kweli hizo
Sayansi na teknolojia wao wenyewe wangekuja na kutuuzia kwa kuwa ni biashara kama zingine
 
Rais wa S.Africa kiherehere cha nchi yake kimemponza. Walijifanya watangazaji mahiri wa tatizo la UVICO...Sasa wazungu wanakupongeza Kwa kutangaza, Kisha malipo yake ni kuitenga nchi yako. Upuzi ulioje?
Hahahaha
 
Umeshakunywa chimpumu akili nazo zimegeuka chimpumu!
Hio simu unayotumia unaweza kuiunda?
Ukiachwa jinsi ulivyo hiyo simu inaundwa, kila kitu kinagundulika kutokana na mazingira na mahitaji. Mbona watu wanapata majibu kwenye maswali magumu.
 
Back
Top Bottom