Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Tronic Digital timer taa za nnje zinawaka muda wowote unaotaka na kujizima muda wowote unaotaka. 0749247920 kwa msaada zaidi nipigie kwa namba izo.

Bei zake ni Tsh 40, 000/=
 

Attachments

  • EM-DT25.jpg
    EM-DT25.jpg
    95.7 KB · Views: 40
  • EMDT31.jpg
    EMDT31.jpg
    60.3 KB · Views: 38
  • EM-DT16.jpg
    EM-DT16.jpg
    53.2 KB · Views: 43
ndugu Hechy Essy kuna mahali nimeona mabati ya mgongo mpana limeandikwa hivi coating class D

kumbe hizi rangi zina class yake?
Ndio, roof coating zina madaraja yake na huwa inawakilisha uwezo wa bati kustahmili moto (fire resistance). Kuna class A, Class B na Class C ambapo class A ndio ina uwezo mkubwa wa kustahmili moto kuliko class zingine na class C ndio ina uwezo mdogo wa kustahmili moto kulinganisha na hizo class zingine. Hiyo Class D binafsi sijawahi kukutana nayo, labda kama ni daraja jipya wamelianzisha hivi karibuni au labda lipo lakini ni adimu kuonekana
 
Ndio, roof coating zina madaraja yake na huwa inawakilisha uwezo wa bati kustahmili moto (fire resistance). Kuna class A, Class B na Class C ambapo class A ndio ina uwezo mkubwa wa kustahmili moto kuliko class zingine na class C ndio ina uwezo mdogo wa kustahmili moto kulinganisha na hizo class zingine. Hiyo Class D binafsi sijawahi kukutana nayo, labda kama ni daraja jipya wamelianzisha hivi karibuni au labda lipo lakini ni adimu kuonekana
ahaa nikajua ni ubora wa rangi ya bati
 
Kwa siku moja inatakiwa usizidishe urefu wa mita 1.5 katika ujenzi wa kuta. Kwa hizi tofali za kawaida (block), mita 1.5 ni sawa na kama kozi 6 hivi.

Hii inasaidia kuupa muda zaidi udongo wa kozi zilizotangulia kunyauka na kukomaa vizuri kabla ya kubeba kozi zingine juu yake ndani ya siku moja hiyo hiyo.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Hii ni moja ya mbinu inayotumika kupata nguzo kubwa mfano zile nguzo za getini. Hapa nguzo ya zege inakuwa ndani ya box lililojengwa kwa kuta za tofali kama unavyoona kwenye picha, baada ya hapo zege inamiminwa ndani ya hilo box.
20250902_074657.jpg
 
Sa
Plaster nzuri ni ile ambayo ukimwagia ukuta maji, ukuta unakauka bila kuchora alama za matofali. Kiujumla michoro ya tofali katika ukuta uliopigwa plaster hutokea pale ratio ya udongo uliotumika kujengea tofali ni kali kuzidi ratio ya udongo uliotumika kupigia plaster

Kitaalam udongo wa kujengea tofali tunatumia ratio ya 1:6 na udongo wa kupigia plaster tunatumia ratio ya 1:4 na 1:5 (ratio ya 1:4 inatumika kwenye kuta upande wa nje, na 1:5 upande wa ndani)

Ratio ya plaster inatakiwa iwe kali kuzidi ratio ya udongo uliotumika kujengea

Kwa mahitaji ya ramani, makadirio ya vifaa vya ujenzi tuwasiliane
Safi mkuu kwa maelezo mazuri..
Naomba nikuulize, hivi ratio ya udongo wa kutengenezea/kufyatulia tofali inapaswa kuwa ngapi..?
 
PLN 0001 2BR

Ramani ya Vyumba Viwili
  • Living room (Sebule)
  • 1 Master bedroom with a Dressing room (W.I.C)
  • 1 Single bedroom
  • Kitchen (Jiko)
  • Public toilet (Choo cha jumuiya)
Ramani hii ina privacy na ventilation ya hali ya juu sana

Bei: Tsh. 100,000/=

Ramani inakuwa na Makadirio yake ya vifaa vya ujenzi kuanzia hatua ya msingi mpaka finishing ambapo itakusaidia kukuongoza katika manunuzi ya vifaa na kuepuka kulanguliwa na mafundi wenye tamaa ya kukuzidishia hesabu ili wajinufaishe zaidi.
View attachment 2694970
Kazuri
 
Sa
Safi mkuu kwa maelezo mazuri..
Naomba nikuulize, hivi ratio ya udongo wa kutengenezea/kufyatulia tofali inapaswa kuwa ngapi..?
Hapo inategemea na size ya tofali (urefu, upana na unene) pamoja na idadi ya tofali unazotaka kutengeneza kwa kila mfuko mmoja wa cement
 
Hapo inategemea na size ya tofali (urefu, upana na unene) pamoja na idadi ya tofali unazotaka kutengeneza kwa kila mfuko mmoja wa cement
Je ni sahihi kutumia mbao za size moja kwa paa kama hili. (mfano 2*3 zote au 2*4 zote)..?
FB_IMG_1755953576361.jpg
 
Je ni sahihi kutumia mbao za size moja kwa paa kama hili. (mfano 2*3 zote au 2*4 zote)..?View attachment 3463866
Sio sahihi,
Ukitumia mbao kubwa pote mfano 2*4 utafanya paa liwe na uzito mkubwa, na ukitumia mbao ndogo pote mfano 2*3 kuna mbao zitaelemewa na mzigo na kupelekea kukatika.

1. Mbao za Rafter, Kingpost, na Struts tumia 2x4

2. Mbao za Wall plate tumia 2x4

3. Mbao za Tie beam tumia 2x6 (kama mfuko unaruhusu, ukishindwa tumia 2x4). Uzito wa paa unabebwa na hizi mbao, na kuusafirisha katika mbao za Wall plate.

4. Mbao za purlin tumia 2x2 (ukiweza tumia 2x3 maana 2x2 za siku hizi ni nyembamba, ukipima na tape hazitimii hiyo nchi 2)

5. Mbao za fascia board tumia 1x6, au 1x8
 
Nyumba ya vyumba viwili yenye sebule, jiko, dining, public toilet na store inaweza isiwe na utofauti au zikazidiana kidogo katika gharama na Nyumba ya vyumba vitatu yenye sebule, jiko na public toilet.

Kama unataka kujenga nyumba ndogo kwa lengo la kupunguza gharama, basi angalia vitu vya ulazima kuwepo. Jiko lazima liwepo, choo lazima kiwepo, sebule lazima iwepo, dining room ni optional kwa maana watu wanaweza wakalia chakula sebleni, store pia ni optional kwa maana unaweza ukajenga jiko kubwa kidogo ili kusiwe na ulazima wa kuwepo store.

Hii ni kwa kujenga nyumba ndogo kwa lengo la kupunguza gharama vinginevyo unaweza ukavijumuisha tu na hivyo vyumba ambavyo ni optional kuweka.
 
Nyumba ya vyumba viwili yenye sebule, jiko, dining, public toilet na store inaweza isiwe na utofauti au zikazidiana kidogo katika gharama na Nyumba ya vyumba vitatu yenye sebule, jiko na public toilet.

Kama unataka kujenga nyumba ndogo kwa lengo la kupunguza gharama, basi angalia vitu vya ulazima kuwepo. Jiko lazima liwepo, choo lazima kiwepo, sebule lazima iwepo, dining room ni optional kwa maana watu wanaweza wakalia chakula sebleni, store pia ni optional kwa maana unaweza ukajenga jiko kubwa kidogo ili kusiwe na ulazima wa kuwepo store.

Hii ni kwa kujenga nyumba ndogo kwa lengo la kupunguza gharama vinginevyo unaweza ukavijumuisha tu na hivyo vyumba ambavyo ni optional kuweka.
kuna ulazima wa kuweka public toilet ikiwa room zote ni self
 
Kuna wale tunatamani kumiliki mijengo mikubwa lakini kipato kidogo. Nikaamua kufata ramani yangu ile ya mjengo mkubwa lakini nikaujenga nusu yake. Kimbembe kinakuja kwenye kupaua sasa. Hivi mkuu Hechy Essy nyumba moja inaweza kupauliwa mapaa mawili tofauti yanayojitegemea? Yaani nijenge nusu ya nyumba niipaue kabisa, then nikimaliza nusu ya pili nipaue iungane bila kuathiri ya mwanzo? Ila yawe mapaa ya kisasa
 
Kuna hii miti ya kisasa ya kivuli ambayo inakuaga na vitunda vidogo vya rangi nyekundu, Nyoka huwa wanaipenda sana. Nadhani huwa wanafuata hivi vitunda (sina uhakika, lakini nilijaribu kuvionja nikagundua kuwa vina sukari, hata Ndege pia wanavipenda sana)


Hapa ninapoishi kuna hii miti ya kivuli miwili, na ndani ya wiki moja tu nimeua Nyoka watatu, mmoja katika hao ni mrefu anazidi futi 4 kwa hivyo ni vyema sana kuwa makini na hii miti.

Usiruhusu mti ukawa mkubwa mpaka kufikia hatua matawi yakawa yanakaribia ama kugusa kuta za nyumba kwani itakuwa rahisi Nyoka kuingia ndani ya nyumba kupitia dirishani au sehemu yoyote iliyo wazi na mara nyingi hawa Nyoka huwa utawaona kipindi cha baridi au mvua inaponyesha (wanatafuta hifadhi katika majumba baada ya mashimo/miti kuloana na maji)

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Mkuu, unataka kusema hata miti ya matunda itakuwa inafatwa na hao viumbe kwa sababu ya sukari?
 
Back
Top Bottom