Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Katika nyumba, kuna zile sehemu ambazo uwezekano wa kutokea nyufa katika kuta ni zaidi ya asilimia 80. Hii ni kutokana na utofauti wa kiwango cha stress kati ya eneo moja na eneo jingine katika jengo, sehemu zingine zina stress ndogo na sehemu zingine zina stress kubwa.

Mfano mzuri wa hizi sehemu ambazo zina uwezekano mkubwa wa kutokea kwa nyufa ni chini ya uwazi wa madirisha, ni moja kati ya sehemu dhaifu mno katika jengo ambapo ikitokea movement yoyote, nyufa zinaanza kutokea hapo.

Mara nyingi nyufa huwa zinatokea katika pattern ya zig zag, sasa huwa tunaweka hivi chini ya uwazi wa madirisha (kati kati) ili hizi nyufa za zig zag zisitokee, kiufupi ni kama tunatengeneza ufa wetu wenyewe ambao unakuwa umenyooka kabla huo ufa halisia (zig zag) haujaja.

Hii tunaita Control Joint

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasilianeView attachment 3476210
Hapa sijaelewa mkuu. Huu ufa unakata na grenda? Je unakata mpaka unatokea upande wa pili? Ukikata kila sehemu yenye dirisha hupunguzi uimara wa nyumba?
Je huu ufa unafanyaje kazi ya kuzuia hizo nyufa za zigzag?
 
Mkuu Hechy Essy una ushauri gani juu ya mfumo huu ambao wenyewe wanadai ni mfumo wa kisasa?
1758798194505.jpg
1758798209006.jpg
 
Huu Uzi nilikuwa nimeusave tangu mwaka jana nafikiri ni mda na mm niombe ushauri haka ka ramani
 

Attachments

  • f04fef4b1a6b44e4cb80185acf661639_1.jpg
    f04fef4b1a6b44e4cb80185acf661639_1.jpg
    219.4 KB · Views: 53
Hatimaye nimemaliza kusoma Uzi wote.
Hongera sana fundi ushauri huu ungeuandikia kitabu halafu uweke Kila kitu ndani hakika pesa yangu pia ningeitoa
 
Hii ni moja ya mbinu inayotumika kupata nguzo kubwa mfano zile nguzo za getini. Hapa nguzo ya zege inakuwa ndani ya box lililojengwa kwa kuta za tofali kama unavyoona kwenye picha, baada ya hapo zege inamiminwa ndani ya hilo box.View attachment 3462047
ujenzi upi ni bora kwa fensi yenye kimo mita 2.8 na mzingo mita 270 kati ya hizi mbili katika picha
0011.jpg
0010.jpg
 
Nahitaji kujenga fremu kubwa 12M Kwa 12m ya biashara ya duka na stoo mixers hardware na vyakula naomba cautation kuanzia msingi wa mawe,tofali za broku, mchanga,semint,mbao,bati,misumar,ufundi nk kwa ramani pia unaweza nishauri ramani nzuri eneo ni tambalale mkoa wa Tanga.
 

Attachments

  • IMG_20250923_133803_HDR.jpg
    IMG_20250923_133803_HDR.jpg
    468.3 KB · Views: 43
  • IMG_20250923_133755_HDR.jpg
    IMG_20250923_133755_HDR.jpg
    480.8 KB · Views: 42
Naomba fully cautation kwa ramani hii ya fremu ya biashara kuanzia mchanga,sement,nondo,mbao,bati,ufundi nk
 

Attachments

  • IMG_20251001_125905.jpg
    IMG_20251001_125905.jpg
    405.8 KB · Views: 43
 
Ukimaliza kujenga pagale/boma lako, kama unapumzika kuendelea na ujenzi kwa muda, basi ziba madirisha na milango ya nje kwa kupanga tofali ili nyumba yako isigeuzwe kuwa guest house au choo na wahuni.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Wakuu, anayehitaji nyumba ya kununua maeneo ya Kibamba anicheki. Nyumba bado kupauwa.
Kama unahitaji njoo nikupe maelezo zaidi, mimi ndo mmiliki mwenyewe.
 
Ili jengo lifanane moja kwa moja na ramani kama inavyoonekana katika karatasi, inatakiwa umakini katika zoezi la kuset jengo. Vipimo vikiyumbishwa kidogo, muonekano wa jengo na paa kwa ujumla hubadilika.

Athari kubwa huwa inakuja kwenye paa, kwa kuwa paa huwa linafata kuta za nje zinavyozunguka kwa hivyo mpishano wa kuta ambazo zilitakiwa ziwe katika grid moja huzalisha vipaa vingine vidogo vidogo ili kuziba nafasi zilizo wazi, kitu ambacho kinaongeza gharama katika hatua ya upauaji.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Ili jengo lifanane moja kwa moja na ramani kama inavyoonekana katika karatasi, inatakiwa umakini katika zoezi la kuset jengo. Vipimo vikiyumbishwa kidogo, muonekano wa jengo na paa kwa ujumla hubadilika.

Athari kubwa huwa inakuja kwenye paa, kwa kuwa paa huwa linafata kuta za nje zinavyozunguka kwa hivyo mpishano wa kuta ambazo zilitakiwa ziwe katika grid moja huzalisha vipaa vingine vidogo vidogo ili kuziba nafasi zilizo wazi, kitu ambacho kinaongeza gharama katika hatua ya upauaji.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Mkuu naomba Raman ya vyumba vi 3
Kimoja masters na varanda yake
Ondoa dinning, kitchen, public toilet
 
Hata kama eneo lako halina asili ya maji maji, hakikisha kuta zako za vyoo unatandika nailon (DPC) kabla hujaanza kupandisha kuta za boma kwa sababu vyooni ni sehemu ambazo zinakuwa na maji maji muda mwingi

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Rekebisha hizo vent za huko kwenye paa, hazina kazi yoyote zaidi ya kuozesha ceiling board
Ni kweli. Ila zinasaidia kupunguza madhara ya ceiling kufumuka pia kutokana na wind pressure... Ingawa hii ina minor effect...
 
Back
Top Bottom