Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Kuhusu uwekaji wa kitchen vent, je ni bomba la material ipi linatumika kuwekwa ukutani kuanzia ilipo vent yenyewe hadi nje na huwa lina kipimo cha mm ngapi. Ni lazima lipite ukutani tu au linaweza kutokea juu ya ukuta na kutambaa kwenye dari hadi kuja kutokea kwenye overhang?.
Kawaida bomba lake huwa ni nchi 6 sawa na 150mm kwa majiko ya size ya kawaida mfano haya ya majumbani. Material yanayotumika ni steel (chuma kilichochanganywa na madini mengine kama carbon ili kuifanya isipate kutu)
 
Kabla ya kumwaga zege, hakikisha nondo zako hazigusani kabisa na box lako.
Nondo itakapogusana na box, baada ya kufumua box nondo zako zitakuwa uchi kama inavyoonekana kwenye picha (japo mtu anaweza akasema zitafunikwa na plaster lakini ni vizuri zaidi nondo zote zikamezwa ndani ya zege)
20250819_112127.jpg
 
Jamani nahitajinramani ya 2 bedroom aprtmen vyumba vyote s3l contained sebule jiko na dinning
 
Hechy Essy Naomba msaada mkuu,kuhusu fishabodi zenye urembo wa ngazi,je! Ule ni ubao mmoja?
Hapo huwa tunatumia mbao mbili zinazopishana upana mfano mbao ya 1x8 na mbao ya 1x6 au mbao ya 1x6 na mbao ya 1x4
Wengine wanaweka mbao tatu yani 1x8, 1x6 na 1x4 ili kupata ngazi 3
 
Hapo huwa tunatumia mbao mbili zinazopishana upana mfano mbao ya 1x8 na mbao ya 1x6 au mbao ya 1x6 na mbao ya 1x4
Wengine wanaweka mbao tatu yani 1x8, 1x6 na 1x4 ili kupata ngazi 3
vipi ukiweka 6 4 4 kwa ngazi tatu
 
Kwa umeme wa 3phase vipi? Na bei yake?
Unaweza ukawa unatumia umeme wa 3 phase ila taa unazotumia ni single phase kwa iyo usiogope hata viwandani mashine zinatumia 3 phase ila taa single Phase.maana yake katika izo phase 3 utachagua phase moja unapeleka kwenye taa.taa ya 3phase hakuna boss wangu kwa hapa Tanzania
 
ipoje iyo
Hii inafungwa juu kwenye connection ya taa za nnje.mim ya kwangu nime set saa 12 na dakika 40 iwashe taa, alafu saa 12 asubui ijizime.iyo ni kila siku yenyewe itakuwa inafanya kazi iyo tu hata umeme ukikatika ina betri yake ya kutunza kumbukumbu inakaa hata miezi 3.umeme ukirudi inaendelea pale pale
 
Kwa sababu mbao mbili zitakuwa zinalingana upana, ili ngazi ipatikane kati ya mbao moja na nyingine inatakiwa hizo mbao zipishane upana
mkuu asante kwa elimu,nyumba inahitaji fishabodi 18,kwamaana hii ninapaswa kununua mbao 54 kwaajili ya ngazi 3. Je! Napaswa kuzipeleka kwenye karakana au fundi mwenyewe atatengenezea site?
 
mkuu asante kwa elimu,nyumba inahitaji fishabodi 18,kwamaana hii ninapaswa kununua mbao 54 kwaajili ya ngazi 3. Je! Napaswa kuzipeleka kwenye karakana au fundi mwenyewe atatengenezea site?
Hapana, hiyo ni kazi ya fundi ila wakati mnakubaliana bei ya ufundi inabidi umuambie kwamba unataka fascia board ya aina hiyo maana kawaida fascia board huwa ni mbao moja.

Pia utakaponunua hizo mbao, usisahau kwenda kuziranda, na kama hazijanyooka vizuri uwaambie wakuchongee mbao za upana flani ili kuonndoa sehemu ya mbao iliyopinda mana huwezi ukakata kwa msumeno wa kawaida ikanyooka
 
Hapana, hiyo ni kazi ya fundi ila wakati mnakubaliana bei ya ufundi inabidi umuambie kwamba unataka fascia board ya aina hiyo maana kawaida fascia board huwa ni mbao moja.

Pia utakaponunua hizo mbao, usisahau kwenda kuziranda, na kama hazijanyooka vizuri uwaambie wakuchongee mbao za upana flani ili kuonndoa sehemu ya mbao iliyopinda mana huwezi ukakata kwa msumeno wa kawaida ikanyooka
daah!sina mengi lakini, Ubarikiwe na MUNGU,ndugu yangu
 
Back
Top Bottom