Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ni vyema dirisha zako ukaziweka kati kati ili mkanda wako juu ya dirisha uwe na support za kuta zinazolingana (support width, kushoto na kulia)

Mfano kama ukuta wako una urefu/upana wa mita 3.6 ndani kwa ndani na dirisha lako lina upana wa mita 1.5 basi dirisha lako inabidi lianzie umbali wa mita 1.05 sawa na sentimita 105 kutokea katika kona ya chumba

X = (3.6 - 1.5)/2 = 1.05m kutokea kwenye kona ya chumba

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Ni vyema dirisha zako ukaziweka kati kati ili mkanda wako juu ya dirisha uwe na support za kuta zinazolingana (support width, kushoto na kulia)

Mfano kama ukuta wako una urefu/upana wa mita 3.6 ndani kwa ndani na dirisha lako lina upana wa mita 1.5 basi dirisha lako inabidi lianzie umbali wa mita 1.05 sawa na sentimita 105 kutokea katika kona ya chumba

X = (3.6 - 1.5)/2 = 1.05m kutokea kwenye kona ya chumba

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Kiongozi kwa makadilio ya vyumba viwili na sebure sehemu tambalale inaweza chukua tofali ngap hadi kukamilika
 
Ukienda kununua kiwanja mahali hasa hivi vya bei kubwa, pendelea kutumia mfumo wa malipo ya awamu hata kama unaweza kulipia pesa yote kwa pamoja.

Hii itamfanya hata muuzaji (na watu wengine kama madalali nk) wajue kwamba pesa yako ni ya kuunga unga (ifanye hali yako ya kiuchumi kuwa ni siri hasa kwa watu usiowajua)

Ukiwa unamiliki kitu ambacho wengi hawana na wanakitafuta kwa nguvu zote basi ujue kwako hiyo ni risk hivyo epuka kujionesha au kutaka kuonekana kuwa unacho.
 
Ukienda kununua kiwanja mahali hasa hivi vya bei kubwa, pendelea kutumia mfumo wa malipo ya awamu hata kama unaweza kulipia pesa yote kwa pamoja.

Hii itamfanya hata muuzaji (na watu wengine kama madalali nk) wajue kwamba pesa yako ni ya kuunga unga (ifanye hali yako ya kiuchumi kuwa ni siri hasa kwa watu usiowajua)

Ukiwa unamiliki kitu ambacho wengi hawana na wanakitafuta kwa nguvu zote basi ujue kwako hiyo ni risk hivyo epuka kujionesha au kutaka kuonekana kuwa unacho.
Mkuu mbona unapotea sana tuna miss madini kama haya
 
Hivi ujenzi wa fensi urefu 40 upana 20 hatua sehemu inabonde kidogo.... Gharama ya fundi tu ni sh ngapi?
 
Wakati wa kufunga mkanda wa juu, kuna hizi mbao za sahani kwa ajili ya sehemu za madirisha na milango (hizi itabidi ununue, huwezi kukodi kwa sababu ni mbao za kukata na wanaokodisha hawataki mbao zao zikatwe)

Size ya mbao za sahani huwa inategemea umetumia tofali za nchi ngapi katika ujenzi wa boma. Kama umetumia tofali za nchi 6, utanunua mbao za 1x6 na kama umetumia tofali za nchi 5 utanunua mbao za 1x5

Mbao za 1x5 zinapatikana kwa kuchana mbao za 1x6 ili kuondoa hiyo nchi 1 iliyozidi. Sasa in case kama umekosa mbao za 1x5, nunua mbao za 1x6 wakuchanie hapo machineni na pia hivyo vipande walivyovichana vibebe uondoke navyo (utaenda kutumia kama mbao za kabali katika mkanda)

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Katika pita pita zako ndio imetokea umepita mahali ukakuta kuna milango miwili ambayo imeshatengenezwa tayari, mmoja una upana wa 90cm na mwingine una upana wa 80cm lakini katika ujenzi upana wa uwazi ulioachwa kwa ajili ya mlango ni 85cm utachukua mlango upi?

Katika mazingira haya ni bora ukachukua mlango uliozidi kipimo (sehemu ya ukuta iliyozidi ukakata na grinder) kuliko ukachukua mlango uliopungua kipimo (ukajazia udongo kwenye mapengo)

Mlango unatakiwa ubane vizuri kwenye ukuta kabla hata ya kuuchapia udongo. Kiujumla fundi milango inatakiwa afike site na apime milango yote, asiangalie vipimo kwenye ramani (ramani inaweza ikaonesha mlango ni 90cm, lakini katika ujenzi ukashangaa uwazi una upana wa 94cm)

Ili kuepuka hizo kazi za kukata kuta au kujaza mapengo, fremu za milango zinatakiwa zifit sawa sawa na kipimo cha uwazi ulioachwa

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Nondo kavu
Ukienda hardware kununua nondo, kuwa makini...fanya field test hapo hapo kabla ya kulipia na kuondoka na mzigo (mchukue fundi abebe na bender yake, uongozane nae hardware).

Nondo kavu ukiikunja huwa inakatika, ni kama mti uliokauka sana.
Nondo inayofaa katika ujenzi haitakiwi kukatika pale inapokunjwa.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
20260216_143427.jpg
 
Kama kiwanja chako ni kidogo na unatamani siku za mbeleni uje uweke uzio (fence), basi ni vyema wakati wa kuset nyumba, nyumba yako ukaiset kwenye kona moja wapo ya kiwanja ili ubaki na eneo upande wa mbele na pembeni tu badala ya kuwa na eneo pande zote nne za nyumba (kwa maana ya kuset nyumba ndani ya kiwanja ambapo nafasi inayobaki kuzunguka nyumba inakuwa ndogo zaidi)


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Kama unatamani kujenga nyumba ya paa la kuficha lakini unaogopa mambo ya paa kuvuja maji kipindi cha mvua, basi unaweza ukatumia mfumo wa mifereji ya nje (badala ya mifereji inayojengwa katika kuta za ndani)

Katika mfumo huu, mifereji yote inayobeba maji inabebwa na kuta za nje na mapaa yake yote yanakuwa yanarusha maji yake huko. Ni baadhi tu ya kuta za kati ndizo hurefushwa juu kwa ajili ya kugawanya paa kulingana na mpangilio wa gutter ulivyo.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Nyumba za paa la kuficha kupendeza kwake ni kule kupishana kwa kuta za juu ya mkanda.

Changamoto iliyopo ni mafundi kulazimisha kuta zote zilingane urefu hata kama hakuna ulazima.

Kule juu ya mkanda, kuna kuta zingine kazi yake ni kusimama kama kingo tu za mifereji ya maji kwa hivyo hakuna ulazima wa kujenga kozi nyingi wakati unaweza ukajenga kozi mbili au tatu tu na ukaokoa idadi kubwa ya tofali.

Mbali na kuokoa tofali, pia inapunguza mzigo wa jengo katika ardhi


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Nondo kavu
Ukienda hardware kununua nondo, kuwa makini...fanya field test hapo hapo kabla ya kulipia na kuondoka na mzigo (mchukue fundi abebe na bender yake, uongozane nae hardware).

Nondo kavu ukiikunja huwa inakatika, ni kama mti uliokauka sana.
Nondo inayofaa katika ujenzi haitakiwi kukatika pale inapokunjwa.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasilianeView attachment 3544797
Sasa ukiacha nondo kavu niulizie nondo gan hizo zingine? Nondo mbichi au?
 
Nyumba za paa la kuficha kupendeza kwake ni kule kupishana kwa kuta za juu ya mkanda.

Changamoto iliyopo ni mafundi kulazimisha kuta zote zilingane urefu hata kama hakuna ulazima.

Kule juu ya mkanda, kuna kuta zingine kazi yake ni kusimama kama kingo tu za mifereji ya maji kwa hivyo hakuna ulazima wa kujenga kozi nyingi wakati unaweza ukajenga kozi mbili au tatu tu na ukaokoa idadi kubwa ya tofali.

Mbali na kuokoa tofali, pia inapunguza mzigo wa jengo katika ardhi


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Nauliza juu ya matumizi ya DPM kwenye hatua ya jamvi. Mfano baada ya kujaza kifusi na mawe kisha ukasuka nondo ( mf. Kwenye jamvi la ghorofa) na kufunika kwa DPM kisha ukamwaga zege. Swali langu ni juu ya kuzifunika nondo kwa DPM haiwezi kuleta shida kwenye mambo ya stability ukizingatia kwamba zege linatakiwa lishikane na nondo moja kwa moja ili kupata mshikamano uliokusudiwa?.
 
Nauliza juu ya matumizi ya DPM kwenye hatua ya jamvi. Mfano baada ya kujaza kifusi na mawe kisha ukasuka nondo ( mf. Kwenye jamvi la ghorofa) na kufunika kwa DPM kisha ukamwaga zege. Swali langu ni juu ya kuzifunika nondo kwa DPM haiwezi kuleta shida kwenye mambo ya stability ukizingatia kwamba zege linatakiwa lishikane na nondo moja kwa moja ili kupata mshikamano uliokusudiwa?.
DPM haiwekwi juu ya nondo ndg, nondo zinalazwa juu ya DPM.

Nondo unalaza juu ya DPM, kwa maana hata nondo pia zinatakiwa zilindwe na unyevu ili zisipate kutu ambapo hiyo kazi inafanywa DPM

Kiufupi DPM inatenganisha tabaka la mawe (hardcore) na zege (jamvi)
 
DPM haiwekwi juu ya nondo ndg, nondo zinalazwa juu ya DPM.

Nondo unalaza juu ya DPM, kwa maana hata nondo pia zinatakiwa zilindwe na unyevu ili zisipate kutu ambapo hiyo kazi inafanywa DPM

Kiufupi DPM inatenganisha tabaka la mawe (hardcore) na zege (jamvi)
Shukrani kwa ufafanuzi. Kuna picha niliiona kwenye page ya NHC, huenda labda sikuangalia vizuri mpangilio wa mawe, DPM na nondo.
 
DPM haiwekwi juu ya nondo ndg, nondo zinalazwa juu ya DPM.

Nondo unalaza juu ya DPM, kwa maana hata nondo pia zinatakiwa zilindwe na unyevu ili zisipate kutu ambapo hiyo kazi inafanywa DPM

Kiufupi DPM inatenganisha tabaka la mawe (hardcore) na zege (jamvi)
20260228_205224.jpg

Picha niliiangalia kwa haraka. Maelezo yako ni sahihi kwa mujibu wa picha.
 
Ujenzi una hatua zake, na hatua zingine zinatakiwa zitangulie kabla ya zingine. Ukivuruga mpangilio ujue lazima utaingia gharama ya ziada huko mbeleni

Mfano unakuta mtu ameanza kupigilia mbao za dari wakati bado hajapachika bomba za umeme ukutani, baadae akitaka kuweka hizo bomba anaanza kufumua mbao za pembeni ili apitishe bomba.

Ikumbukwe kwamba fundi ukimuita site, yeye atafanya kazi yake husika na hawezi kukuambia kwamba inabidi fundi wa tasnia flani ndio anatakiwa aanze kabla yake kwa kuhofia kuzungukwa na fundi mwenzake na kukosa hiyo kazi kwahivyo wewe mwenye kazi (boss) ndio unatakiwa ujue ikitoka hatua hii inafuata hatua gani

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Back
Top Bottom