Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Kuna hii miti ya kisasa ya kivuli ambayo inakuaga na vitunda vidogo vya rangi nyekundu, Nyoka huwa wanaipenda sana. Nadhani huwa wanafuata hivi vitunda (sina uhakika, lakini nilijaribu kuvionja nikagundua kuwa vina sukari, hata Ndege pia wanavipenda sana)


Hapa ninapoishi kuna hii miti ya kivuli miwili, na ndani ya wiki moja tu nimeua Nyoka watatu, mmoja katika hao ni mrefu anazidi futi 4 kwa hivyo ni vyema sana kuwa makini na hii miti.

Usiruhusu mti ukawa mkubwa mpaka kufikia hatua matawi yakawa yanakaribia ama kugusa kuta za nyumba kwani itakuwa rahisi Nyoka kuingia ndani ya nyumba kupitia dirishani au sehemu yoyote iliyo wazi na mara nyingi hawa Nyoka huwa utawaona kipindi cha baridi au mvua inaponyesha (wanatafuta hifadhi katika majumba baada ya mashimo/miti kuloana na maji)

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Katika hatua ya kufanya wiring katika nyumba, kuna mbinu mbali mbali zinazotumika kupunguza gharama za material.

Leo nitaelezea mbinu moja wapo

Ikitokea vyumba viwili vina-share ukuta, basi tafuta point moja katika huo ukuta ambayo itakuwa comfortable kwa vyumba vyote kuweka socket pande zote mbili. Hii inasaidia kupunguza matumizi ya waya na bomba tofauti na kuweka socket katika point tofauti tofauti.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Mara nyingi level huwa inatafutiwa wakati wa kufunga box la mkanda lakini pia unaweza ukatafuta level kozi mbili kabla ya kufikia hatua ya mkanda.
Kama ulivyopendekeza kwenye comments za nyuma juu ya matumizi ya level pipe. Je, haiwezekani ukatumia mbao ama kamba yenye urefu fulani, mfano kama ukuta umefika futi 7, ukatumia kamba au mbao yenye futi 7 kupimia hiyo level ya ukuta kwa kila upande?.
 
Kama ulivyopendekeza kwenye comments za nyuma juu ya matumizi ya level pipe. Je, haiwezekani ukatumia mbao ama kamba yenye urefu fulani, mfano kama ukuta umefika futi 7, ukatumia kamba au mbao yenye futi 7 kupimia hiyo level ya ukuta kwa kila upande?.
Inawezekana, ila mara nyingi hii tunatumia ktk ujenzi wa msingi hasa sehemu zenye muinuko (msingi kuwa na steps)

Baada ya kuchimba msingi pote, unachomeka mbao za 2x2 kama pegs katika kila kona ya nyumba, then unatafuta peg ambayo ipo ktk muinuko zaidi. Katika peg hii ndio utaamua sasa level ya msingi iwe wapi mfano unaweza ukasema msingi wangu utokeze juu kwa futi moja au futi moja na nusu (utapima then utaweka alama)

Utatumia pipe level kutafuta hiyo level katika mbao zingine zote kisha utaanza kuchora mark za kozi kutokea hiyo level ya msingi kushuka chini (wakati huo unakuwa umeshatoa kimo cha mkanda kutokea huko juu)

Kama utatumia tofali za nchi 5, basi utakuwa unachora mark kila baada ya nchi 6 (tofali nchi 5, udongo nchi 1) na kuandika majina yake mfano 1,2,3 n.k kuanzia chini kwenda juu

Utakuwa unatumia kamba kufunga katika hizo mark ulizoweka kulingana na kozi husika unayotaka kujenga. Hii itakusaidia pia kujua kozi ya kwanza ya ukuta flani itaenda kukutana na kozi ya ngapi katika ukuta mwingine kwahivyo kuta hazitapishana usawa. Mfano unaweza ukakuta kozi ya kwanza ya ukuta ambao upo katika muinuko inakuja kukutana na kozi ya nne ya ukuta ambao upo bondeni, kama ulichora vizuri mark zako, kozi zako zitakuwa zinaumana zenyewe bila yoyote
 
Katika hatua ya kufanya wiring katika nyumba, kuna mbinu mbali mbali zinazotumika kupunguza gharama za material.

Leo nitaelezea mbinu moja wapo

Ikitokea vyumba viwili vina-share ukuta, basi tafuta point moja katika huo ukuta ambayo itakuwa comfortable kwa vyumba vyote kuweka socket pande zote mbili. Hii inasaidia kupunguza matumizi ya waya na bomba tofauti na kuweka socket katika point tofauti tofauti.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Mbinu nyingine
Usifunge bomba za umeme kwa kufuata mbao za dari jinsi zilivyopigiliwa, hii itakulazimisha bomba zako ziwe zinakutana kwa kutengeneza nyuzi 90 kitu ambacho kitaongeza matumizi ya waya na bomba.

Pendelea kuunga points ambazo hazipo katika uelekeo mmoja kwa kutengeneza diagonal na sio kutengeneza "L"

Kwenye ile Pythagoras theorem ya A²+B²=C²

Mfano kama A ni 3ft, na B ni 4ft basi C itakuwa ni 5ft, kwahivyo utaona kama ukilaza bomba diagonally kati ya point na point utatumia waya na bomba zenye urefu wa 5ft tofauti na ungelaza bomba kwa kutengeneza "L" ambapo ungetumia waya na bomba zenye urefu wa 7ft (yani 3ft +4ft)

Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane (Bado offer ya punguzo la bei inaendelea mpaka siku ya saba saba)
 
Mara nyingi taa ya koridoni, switch yake huwa inawekwa mwanzoni mwa korido kwa hivyo kama mtu yupo mwishoni mwa korido atalazimika kuifata switch ilipo ili azime/awashe taa kisha arudi tena mwishoni mwa korido huku akiwa anatembea gizani.

Ili kukabiliana na hii changamoto, ni vyema taa ya koridoni ikawa na swichi mbili (two way switch) mwanzoni na mwishoni mwa korido ili mtu aweze kuwasha/kuzima taa akiwa popote

Njia hii inatumika pia na kwenye taa inayomulika ngazi (kwa majengo ya ghorofa) ambapo switch moja inawekwa chini kabla ya kupanda ngazi na switch nyingine inawekwa juu baada ya kumaliza kupanda ngazi

Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
 
Mara nyingi taa ya koridoni, switch yake huwa inawekwa mwanzoni mwa korido kwa hivyo kama mtu yupo mwishoni mwa korido atalazimika kuifata switch ilipo ili azime/awashe taa kisha arudi tena mwishoni mwa korido huku akiwa anatembea gizani.

Ili kukabiliana na hii changamoto, ni vyema taa ya koridoni ikawa na swichi mbili (two way switch) mwanzoni na mwishoni mwa korido ili mtu aweze kuwasha/kuzima taa akiwa popote

Njia hii inatumika pia na kwenye taa inayomulika ngazi (kwa majengo ya ghorofa) ambapo switch moja inawekwa chini kabla ya kupanda ngazi na switch nyingine inawekwa juu baada ya kumaliza kupanda ngazi

Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
Hakuna Three way switch yaan unawasha mara tatu
 
Hakuna Three way switch yaan unawasha mara tatu
Kama unataka kuwe na switch zaidi ya mbili (mfano 3) unaongeza switch ya 4-ways (intermediate switch) katika hizo switch mbili za 2-ways.

Switch ya 2-ways ina terminal 3, terminal moja wapo huwa inaingiza moto (phase) kutoka kwenye source au kutoa moto kutoka kwenye switch na kupeleka kwenye taa (au kifaa kingine chochote). Terminal mbili zinazobaki (L1 na L2) zinaenda kuungwa kwenye terminal mbili za 2-way switch ya pili

Switch ya 4- ways ina terminal 4 kwahivyo nyaya mbili za 2-way switch ya kwanza zinaenda kwenye terminal mbili za 4-way switch na terminal mbili za 2-way switch ya pili zinaenda kwenye terminal mbili za 4-way switch zilizobakia. Kwa kufanya hivi, utaweza kuzima au kuwasha kifaa cha umeme kwa kutumia switch yoyote katika hizo switch tatu
 
Mara nyingi taa ya koridoni, switch yake huwa inawekwa mwanzoni mwa korido kwa hivyo kama mtu yupo mwishoni mwa korido atalazimika kuifata switch ilipo ili azime/awashe taa kisha arudi tena mwishoni mwa korido huku akiwa anatembea gizani.

Ili kukabiliana na hii changamoto, ni vyema taa ya koridoni ikawa na swichi mbili (two way switch) mwanzoni na mwishoni mwa korido ili mtu aweze kuwasha/kuzima taa akiwa popote

Njia hii inatumika pia na kwenye taa inayomulika ngazi (kwa majengo ya ghorofa) ambapo switch moja inawekwa chini kabla ya kupanda ngazi na switch nyingine inawekwa juu baada ya kumaliza kupanda ngazi

Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
Unaweza ukaongeza switch ya taa/feni pembeni kidogo ya kitanda ili usilazimike kuinuka kitandani kwenda kuzima/kuwasha taa mlangoni.

Ulishawahi kujikwaa kidole cha mwisho kwenye angle ya kitanda wakati unarudi kitandani baada ya kwenda mlangoni kuzima taa? Basi na hili linaepukika pia kwa kutumia njia hii

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Ushauri wa fundi kabla na baada ya mapatano ya bei

Kabla ya Mapatano
Kabla ya mapatano, fundi huwa anatoa ushauri mzuri tu ili akuset umpe kazi mfano anaweza akakuambia hapa inabidi msingi uende chini, tuweke na nguzo kwenye kona n.k ili nyumba iwe imara (lengo ni kukuonesha kuwa kazi itakayofanyika ni kubwa hivyo hata gharama ya ufundi pia atataja bei kubwa)

Baada ya Mapatano
Baada ya kupatana bei ya ufundi, fundi huwa anakuja na ushauri mwingine tofauti na ule wa awali mfano anaweza akasema kutokana na aina ya huu udongo, chini tukizamisha hata kozi 3 tu inatosha na wala haina haja ya kuweka nguzo yoyote (anaweza akakupa na mifano kwamba kuna mahali walijenga hivyo na hakujatokea shida yoyote)

Hapa kumbuka kuwa lengo hasa ni kujipunguzia kazi ambapo kama utakubali ushauri wake, basi kwake itakuwa ni faida zaidi kwa kuwa gharama za ufundi zitabaki kuwa vile vile kama mlivyokubaliana licha ya kazi kupungua.

Baadae likitokea tatizo lolote, huyo fundi hutompata tena na hivyo utaingia gharama zingine za marekebisho ama kuanza upya kabisa kutokana na kufuata ushauri wa fundi unaolenga kujipunguzia kazi.

Kutokana na kupungua kwa idadi ya material, wengi hukubaliana na huu ushauri wa awamu ya pili ambapo baadae inaweza ikakuletea shida na kujikuta unaingia gharama mara mbili.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Hatua ya kuweka umeme katika nyumba imejigawa katika phase tatu

Phase ya kwanza
Hii huwa inafanyika kabla ya kupigilia mbao za dari ambapo inahusisha uwekaji wa box za switch na sockets sambamba na bomba zake zinazoelekea juu ya kuta, lakini pia kama taa zako utaamua kuzifungia ukutani badala ya kufungia kwenye dari itabidi uweke na hizo point za taa katika kuta kwenye hii hatua.

Phase ya pili
Hii huwa inafanyika baada ya kupigilia mbao za dari ambapo hapa inahusisha uungaji wa bomba juu ya dari na kufanya wiring

Phase ya tatu
Hii huwa inafanyika baada ya kuta kupakwa rangi, ambapo huwa inahusisha ufitishaji wa switch, sockets, taa za ukutani n.k



NB: Wengine huwa wanaweka bomba kabla ya kupiga plaster kuta, kama utafanya hivi basi inabidi box zako za switch na socket zitokeze nje kidogo na kusakafia plaster kuzunguka box zako ili zisiwe uchi pembeni vinginevyo box zako zitakuwa zimefukiwa na plaster na hivyo zoezi la ufungaji wa switch/sockets linakuwa gumu.


Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
 
Kabla ya zoezi la kubandika tiles, lazima kwanza ujue tiles zako ni tiles za aina gani. Kuna tiles ambazo huwezi kubandika mpaka uziloweke kwenye maji na kuna tiles zingine unaweza ukazibandika bila kuloweka kwenye maji.

Tiles zinalowekwa kwenye maji kabla ya kubandikwa ili zishibe maji na zisifyonze maji yaliyopo kwenye udongo wa kujengea (mortar) hali itakayosababisha tiles kutoshika vizuri kutokana na kupotea kwa maji ya kwenye udongo

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Ni nini tofauti ya DPM na Dpc?
DPC (Damp proof course) inalazwa juu ya mkanda wa chini kabla ya kuanza ujenzi wa tofali za boma, lakini DPM (Damp proof membrane) yenyeye ni pana na inatandikwa kama mkeka chini ya jamvi/floor

Zote kazi yake ni moja, kuzuia unyevu kutoka sehemu ya chini ya nyumba (msingi) na kwenda juu ya nyumba (boma)
 
Wakati mwingine sio lazima sana kuchukua vifaa vyote vya ujenzi vikiwa ktk hali yake ya uzima mfano unapoenda kununua tiles, unanunua box za tiles ambazo ni nzima na ukifika site tiles zingine unazikata ili upate vipande vya kujazia na wakati huo huo pale hardware uliponunulia hizo tiles kuna box za tiles ambazo baadhi ya vipande vimekatika na muuzaji anauza kwa bei ya hasara hivyo kama ungechanganya box nzima na zile zilizokatika ungeokoa kiasi flani cha pesa

Hii pia unaweza ukaapply kwenye gympsum board ktk uwekaji wa dari, tofali n.k kwa lengo la lengo kupunguza gharama

Kabla ya kufanya uamuzi inabidi ufanye mahesabu ili upate makisio kwamba nyumba yako itahitaji vitu vizima vingapi, ili uweze kujua sehemu iliyobaki itahitaji kiasi gani cha material ambazo sio nzima (hapa simaanishi ubovu, namaanisha utimilifu)
Hii ni Moja ya matumizi mazuri ya pesa, ushauri huu uheshimike
 
Kabla ya kufunga mkanda wa chini, jiridhishe kwanza na urefu wako wa msingi kama unakutosha au lah. Wengine hupata wazo la kuongeza urefu wa msingi baada ya kufunga na kumwaga mkanda ambapo wanalaza tofali zingine juu ya mkanda kabla ya kusimamisha tofali za boma kitu ambacho sio sahihi.

Ikiwa msingi wako ni mrefu, ni vyema ukafunga mikanda miwili (mfano baada ya kozi tano ukafunga mkanda, kisha ukaongeza kozi tatu ndipo ukafungwa mkanda mwingine)

Tofali za boma zinatakiwa zikae moja kwa moja juu ya mkanda.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Katika mfumo wa umeme, hakikisha kila sakiti inatumia size ya waya husika. Mfano sakiti ya socket waya wake ni tofauti na waya unaotumika katika sakiti ya taa/feni.

Katika sakiti ya socket, size ya waya inayotumika ni 2.5mm² na katika sakiti ya taa waya unaotumika ni 1.5mm²

Kwa kuwa waya wa 2.5mm² bei yake ipo juu kulinganisha na bei ya waya wa 1.5mm², mafundi wamekuwa na kawaida ya kutumia waya wa 1.5mm² katika sakiti zote licha ya kwamba katika list ya manunuzi waya wa 2.5mm² uliwanunulia (kwao ni bora ubaki waya wa 2.5mm² kuliko ubaki waya wa 1.5mm² ili wakienda kuuza wapate pesa nyingi)

Huo ni mfano mdogo tu, kuna waya wa 4mm² pia ambao unatumika kwenye sakiti ya jiko la umeme, kuna waya wa 6mm² au 10mm² ambao unaenda kupokelea umeme kwenye mita (hapa watakuambia ununue waya wa urefu flani mfano mita 10, lakini kimatumizi unakuta umetumika waya wa mita 4 kwa hivyo muwe makini msije mkamaliza ujenzi mkiwa hoi bin taaban, mkakosa hata hela ya mchele ya kufungulia nyumba siku ya kuhamia)


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Katika mfumo wa umeme, hakikisha kila sakiti inatumia size ya waya husika. Mfano sakiti ya socket waya wake ni tofauti na waya unaotumika katika sakiti ya taa/feni.

Katika sakiti ya socket, size ya waya inayotumika ni 2.5mm² na katika sakiti ya taa waya unaotumika ni 1.5mm²

Kwa kuwa waya wa 2.5mm² bei yake ipo juu kulinganisha na bei ya waya wa 1.5mm², mafundi wamekuwa na kawaida ya kutumia waya wa 1.5mm² katika sakiti zote licha ya kwamba katika list ya manunuzi waya wa 2.5mm² uliwanunulia (kwao ni bora ubaki waya wa 2.5mm² kuliko ubaki waya wa 1.5mm² ili wakienda kuuza wapate pesa nyingi)

Huo ni mfano mdogo tu, kuna waya wa 4mm² pia ambao unatumika kwenye sakiti ya jiko la umeme, kuna waya wa 6mm² au 10mm² ambao unaenda kupokelea umeme kwenye mita (hapa watakuambia ununue waya wa urefu flani mfano mita 10, lakini kimatumizi unakuta umetumika waya wa mita 4 kwa hivyo muwe makini msije mkamaliza ujenzi mkiwa hoi bin taaban, mkakosa hata hela ya mchele ya kufungulia nyumba siku ya kuhamia)


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Siku hizi wanatumia zile single nazo zinaivo vipimo?
 
Back
Top Bottom