Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Namna sahihi ya kukunja ringi za nguzo/mkanda
20250524_213858.jpg
 
Ukienda hardware kununua material, jitahidi pia kuongozana na muuzaji ili na wewe ukachague bidhaa unayoipenda maana kawaida wauzaji huwa wanaanza kuuza bidhaa zenye kasoro ili wabaki na bidhaa nzuri dukani mfano upande wa nondo watakupatia nondo ambazo zimeshaanza kupata kutu wakati nondo mpya zipo, upande wa mbao watakupatia mbao zilizopinda/nyembamba wakati mbao zilizonyooka zipo n.k

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
PLN 0001 2BR

Ramani ya Vyumba Viwili
  • Living room (Sebule)
  • 1 Master bedroom with a Dressing room (W.I.C)
  • 1 Single bedroom
  • Kitchen (Jiko)
  • Public toilet (Choo cha jumuiya)
Ramani hii ina privacy na ventilation ya hali ya juu sana

Bei: Tsh. 100,000/=

Ramani inakuwa na Makadirio yake ya vifaa vya ujenzi kuanzia hatua ya msingi mpaka finishing ambapo itakusaidia kukuongoza katika manunuzi ya vifaa na kuepuka kulanguliwa na mafundi wenye tamaa ya kukuzidishia hesabu ili wajinufaishe zaidi.
View attachment 2694970
Ungeweka namba ya simu ingependeza mkuu.Nawaza kujenga naamini utakuwa msaada wangu wa karibu
 
Mkuu hii kampuni ya Ando unaizungumziaje kwenye Bati zake
 
Pia ni muhimu kalo la choo kama nyumba ipo bondeni yan siyo kilimani kwenye kujenga ni muhimu likatoka juu hata nusu futi ili kama kutakuwa na maji ya mvua yasiweze kuingia kwenye kalo ilo la choo
 
Hivi ni standard ya milango kwenye nyumba ni ngapi? Kwa mfano mlango wa 110 unafaa kuwa mlango wa kuingilia?
 
Hivi ni standard ya milango kwenye nyumba ni ngapi? Kwa mfano mlango wa 110 unafaa kuwa mlango wa kuingilia?
Mlango wa chumba kawaida ni sentimita 90 sawa na around futi 3
Mlango wa kuingilia sebleni kawaida ni sentimita 120 sawa na around futi 4 (huu wa sebleni unakuwaga ni double door)
 
Mlango wa chumba kawaida ni sentimita 90 sawa na around futi 3
Mlango wa kuingilia sebleni kawaida ni sentimita 120 sawa na around futi 4 (huu wa sebleni unakuwaga ni double door)
Yaani mie nimeacha 100cm milango ya vyumbani na 110 mlango mkubwa
 
Back
Top Bottom