Jana nìpo zangu duka la vifaa vya umeme kuulizia kifaa flani, mara akaja jamaa mmoja akawa anaulizia kifaa cha kucontrol taa zijiwashe na kujizima zenyewe pindi giza linapoingia (Photocell).
Muuzaji akamuambia yule jamaa kwamba hicho kifaa kipo bei yake 50,000/=, jamaa akatoa pesa akalipia then akaondoka zake. Nilimuangalia yule muuzaji mara mbili mbili (bila yeye kuniona), wakati huo nasubiri wanitafutie kifaa changu niondoke
Hivi ndivyo maboss wengi wanavyopigwa huko hardware kwa kutojua bei halisi, bei aliyolipia jamaa ni zaidi ya mara 3 ya bei halisi na hii yote ni kwa sababu ya kutojua. Wauzaji wengi wa hardware sio wamiliki wa hizo hardware, wengi wameajiriwa kwa hivyo kwa situation kama hii muuzaji anaweka pesa ya boss pembeni (bei halisi), iliyobaki yote ni ya kwake.
Hakikisha kabla hujaenda mahali kununua kitu, uwe tayari unajua bei yake halisi maana wauzaji huwa wanataja bei kulingana na muonekano wa mtu jinsi ulivyo (wakiona umenawiri nawiri ndio wanakupiga vizuri zaidi, lakini wakiona hueleweki eleweki wanatakujia bei ya kawaida maana wanajua wakikutajia bei ya juu utakimbia)
Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane