Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, makadirio, Elimu na ushauri kuhusu Ujenzi

Ghorofa sio mali ya watu wote broo [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Vi apartment vya 2 bedroom vi2 na kimoja 1 bedroom is vyumba vyote self
Hapana usiseme hivyo, wewe weka tu nadhiri na umuombe Mungu, yeye ndiye anayejua kesho zetu zipoje na kwake hakuna kinachoshindikana pale anapoamua kitu kiwe, kinakuwa

Inawezekana hiyo bei ikawa ni pamoja na kujenga boma (labda), maana katika hali ya kawaida huwezi ukamchaji mtu pesa nyingi kiasi hicho, haiendani kabisa na aina ya jengo unalotaka kujenga
 
Hapana usiseme hivyo, wewe weka tu nadhiri na umuombe Mungu, yeye ndiye anayejua kesho zetu zipoje na kwake hakuna kinachoshindikana pale anapoamua kitu kiwe, kinakuwa

Inawezekana hiyo bei ikawa ni pamoja na kujenga boma (labda), maana katika hali ya kawaida huwezi ukamchaji mtu pesa nyingi kiasi hicho, haiendani kabisa na aina ya jengo unalotaka kujenga
Ah ndio hivyo wanasema oh sijui unspata ramsni zote ...sasa sijui ndio mmie sielewi haya mambo
 
Mkuu hii kampuni ya Ando unaizungumziaje kwenye Bati zake
Kwa kweli sina uzoefu nayo mkuu, huwa nayasikia tu...na kupata feedback ni mpaka umpate mtu ambaye ameshayatumia miaka kadhaa nyuma japo pia ubora unaweza ukabadilika siku za mbeleni mana kila batch huwa ina material (malighafi) yake
 
Ndugu zangu nataka nijitupe kwa Bati Bomba kutokana na ufinyu wa bajeti. Vipi mnazionaje hizi ndugu zangu.
 
Kwa kweli sina uzoefu nayo mkuu, huwa nayasikia tu...na kupata feedback ni mpaka umpate mtu ambaye ameshayatumia miaka kadhaa nyuma japo pia ubora unaweza ukabadilika siku za mbeleni mana kila batch huwa ina material (malighafi) yake
Kwaiyo bora tu turuke na ALAF
 
nimeona G30 wanauza 38k bati la futi 10 sio bei sana mbona
Yah inawezekana, Alaf wana aina nyingi za bati.... Mara nyingi bei zake huwa ni kwa kipimo cha mita mfano Tsh 19,500/running meter kwa hivyo kama unataka bati la mita 4 mfano, unazidisha Tsh 19,500 kwa 4m kupata bei ya pc 1 ya huo urefu
 
Rafiki yangu mmoja ananiambia kwamba nyumbani kwao kila siku lazima mtu ajikwae kwenye ngazi, mwanzo wakawa wanahisi labda ni mambo ya kishirikina.

Wakapambana vya kupambana lakini bado ile hali ikawa inajirudia. Sasa siku moja ikabidi niende kwao na tape measure kwa lengo la kuhakiki vipimo, na katika kupima pima tukagundua kwamba ngazi zilikuwa hazilingani (zinatofautiana urefu)

Ikabidi tiles zitolewe kwenye ngazi na finishing ikafanyika upya ili kuhakikisha ngazi zote zinalingana urefu. Baada ya hapo, lile tatizo la kujikwaa mara kwa mara likawa limetoweka.

Mtu anapopanda ngazi ya kwanza, basi miguu inakuwa imeshacopy ule urefu wa ngazi ya kwanza kwa hivyo hata miguu itakuwa inainuka kwa urefu ule ule wa ngazi ya kwanza na ndio maana mtu anaweza akawa anapanda ngazi bila kuangalia chini na asijikwae.

Ikitokea ngazi moja wapo ikawa ni ndefu kuliko ngazi ya kwanza, asilimia za kujikwaa ni kubwa zaidi na ikitokea ngazi moja wapo ni fupi kuliko urefu wa ngazi ya kwanza, kuna ile hali mtu mguu unakuwa kama abadumbukia kwenye shimo

Kabla ya kutafuta suluhisho la tatizo, ni muhimu kwanza ukajua tatizo linasababishwa na nini.


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Ili taa zako ziweze kujiwasha zenyewe pindi giza linapoanza kuingia na kujizima zenyewe pindi kunapoanza kupambazuka unahitaji kuwa na kifaa kinachoitwa Photocell ambacho kinafungwa nje ya nyumba katika sakiti (circuit) ya taa nje.

Hii itasaidia taa zako kujicontrol zenyewe hata kama utakuwa umesafiri/unachelewa kurudi nyumbani kwako lakini pia kinasaidia sana kupunguza matumizi ya umeme, hata ukisahau kuzima taa za nje manually, hichi kifaa kitazizima chenyewe.

Kama ulishawahi kukiona mahali kimefungwa, basi hiyo ndio kazi yake. Kama upo kwenye hatua ya kufanya wiring, msisitize fundi wako akuwekee hicho kifaa

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane (Offer ya punguzo la bei inaendelea mpaka tarehe 1 July)
20250615_214547.jpg
 
Hakikisha unatafuta mtaalam wa masuala ya ujenzi kila baada ya hatua flani ili kubaini kama kuna makerekebisho ya kufanya kabla ya hatua inayofuata kufanyika.

Sio kila fundi anaweza kuficha makosa ya fundi aliyetangulia mfano fundi kupaua akikuta kuta zako hazina level moja anaweza akapaua tu hivyo hivyo kwa kufuata hizo kuta na hatimae paa nalo linainama.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Naendelea kuwasisitiza ndg zanguni, kwa wale mnaoweka socket za kuchajia nje ya nyumba hakikisha ndani kuna switch ya kuzima hizo socket ili mtu asiweze kuzitumia vinginevyo utakuwa umewasaidia wezi kurahisisha kazi ya kukata nondo za madirisha kwa kutumia grinder na kuingia ndani pindi unapokuwa haupo

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Hakikisha unatafuta mtaalam wa masuala ya ujenzi kila baada ya hatua flani ili kubaini kama kuna makerekebisho ya kufanya kabla ya hatua inayofuata kufanyika.

Sio kila fundi anaweza kuficha makosa ya fundi aliyetangulia mfano fundi kupaua akikuta kuta zako hazina level moja anaweza akapaua tu hivyo hivyo kwa kufuata hizo kuta na hatimae paa nalo linainama.

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Hivi ili kutavziwe na level moja inatakiwa itaftiwe hatua gani iyo level
 
Hivi ili kutavziwe na level moja inatakiwa itaftiwe hatua gani iyo level
Mara nyingi level huwa inatafutiwa wakati wa kufunga box la mkanda lakini pia unaweza ukatafuta level kozi mbili kabla ya kufikia hatua ya mkanda.

Hii itasaidia kugawanya utofauti wa level uliopatikana katika kozi zingine mfano wakati mwingine unakuta kuta zimetofautiana kwa nchi 2 au na zaidi (mmoja mfupi, mmoja mrefu) ambapo kama ungenotice mapema basi ungeweza kuongeza udongo wa kujengea nchi 1 katika kila kozi kuliko kurundika udongo wote katika kozi moja ya mwisho.

Njia nzuri ni kutafuta level chini, kisha ukawa unajenga kwenda juu kwa kufuata hizo level kama alama ambapo utakapofikia hatua ya mkanda, utaona juu kuta zako zote zimelingana
 
Back
Top Bottom