Mahara Nguku
Member
- Dec 9, 2014
- 27
- 7
muda mrefu nimekuwa nikimfikiria sana rais Kikwete, kwamba anachofanya sijui ni kutafuta kupendwa au namna gani? maana tangu watangulizi wake kama Mwl. Nyerere, Mwinyi, na MKapa hatujawahi kuona wakiwakaribisha wasanii wa miziki ikulu, sijui ndio kupungua kwa hadhi ya ikulu? mara tunamuona na mzee yusufu wa taarabu, mara Ray c, mara diamond, sijui kuna nini kati ya rais na wasanii hawa, amekuwa rais wa kwanza tz kukingia kifua maovu ya serikali yake, sijui waliomchagua rais huyu wanalionaje hili? maana hawamshauri hata kidogo.