Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi alazwa kwa maradhi ya kifua

"Mzee Ali Hassan Mwinyi amepelekwa hospitali akiugua maradhi ya kifua. Anaendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari" - Nukuu.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi amepelekwa hospitali akiugua maradhi ya kifua. Anaendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Kutokana na ushauri wa madaktari wake, familia imeona ni vyema apate faragha akiwa anapatiwa matibabu. Hivyo Familia inaiomba jamii kumkumbuka kwenye Dua, Sala, na Maombi.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie shifaa ya haraka Mzee wetu pamoja na wagonjwa wengine wote wanaokabiliwa na maradhi mbali mbali.

Abdullah Ali Mwinyi
Msemaji wa Familia
Uangalizi huu ni ule wa "Intensive Care Unit, ICU" ama wa ni wa "High Dependency Unit, HDU"?

Ukifikifikisha umri wa miaka 70 wewe tayari ni "pensioner of God", na kwa kufikisha miaka >95 hapo basi "formular" zote za uhai wa mwanadamu zinabakia kwa Muumba mwenyewe.

Nahisi Taifa letu linakwenda kushuhudia tena bendera zikipepea kwa nusu mlingoti. Asante sana kwa familia kwa kuwaandaa watu kisaikolojia.
 
Safari imewadia, kodi zetu tangu 1995 zitapumua
Wewe utakua ni mtu ambae umepigika kinoma,ndio ukaamua hasira zako uzielekeze kwa wengine,

Unaamini kua kushindwa kwako kumesababishwa na wengine,chuki haziwezi kukutoa kwenye umasikini,kulaumu wengine kwa kushindwa kwako hakuwezi kubadili kitu,pambana ufanikiwe ili usiwe na chuki za kijinga.
 
Wewe utakua ni mtu ambae umepigika kinoma,ndio ukaamua hasira zako uzielekeze kwa wengine,

Unaamini kua kushindwa kwako kumesababishwa na wengine,chuki haziwezi kukutoa kwenye umasikini,kulaumu wengine kwa kushindwa kwako hakuwezi kubadili kitu,pambana ufanikiwe ili usiwe na chuki za kijinga.
Huyo naona ana matatizo ya akili yanayomsumbua ambayo yanahitaji matibabu ya haraka sana.maana mtu mwenye akili Timamu hawezi kuandika ujinga aliouandika.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ndugu Abdullal Alli Mwinyi Msemaji wa familia ya Rais mstaafu wa awamu ya pili mzee Mwinyi ameiomba jamii kumkumbuka mzee wetu na Rais wetu mstaafu kwa sara,dua na maombi.

Ambapo amepelekwa hospitalini kutokana na maradhi ya kifua na kuendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari wake.

Kwa hiyo watanzania wenzangu tumuombee mzee wetu na Rais wetu mstaafu ambaye ndiye muasisi wa mageuzi ya kisiasa hapa nchini.

Ni wakati wake ndio mfumo wa vyama vingi uliingia nchini na demokrasia kuanza kuchukua nafasi yake na kutoa nafasi ya watu kuzungumza kwa uhuru bila shida. Ni wakati wake ambapo mabadiliko makubwa sana ya kiuchumi yalifanyika katika kuwaondoa watanzania katika dimbwi la umaskini uliotopea.

Kwa waliosahau au kutoelewa ni kuwa mzee wetu huyu hapo mwakani panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu atatimiza miaka mia moja yaani karne moja.jambo ambalo kiukweli kufikisha umri huo hapa Duniani ni lazima umshukuru Mungu na kusema imekuwa hivyo kwa neema tu ya Mungu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Akufe tu zee gani limedinya hadi mama mzazi
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ndugu Abdullal Alli Mwinyi Msemaji wa familia ya Rais mstaafu wa awamu ya pili mzee Mwinyi ameiomba jamii kumkumbuka mzee wetu na Rais wetu mstaafu kwa sara,dua na maombi.

Ambapo amepelekwa hospitalini kutokana na maradhi ya kifua na kuendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari wake.

Kwa hiyo watanzania wenzangu tumuombee mzee wetu na Rais wetu mstaafu ambaye ndiye muasisi wa mageuzi ya kisiasa hapa nchini.

Ni wakati wake ndio mfumo wa vyama vingi uliingia nchini na demokrasia kuanza kuchukua nafasi yake na kutoa nafasi ya watu kuzungumza kwa uhuru bila shida. Ni wakati wake ambapo mabadiliko makubwa sana ya kiuchumi yalifanyika katika kuwaondoa watanzania katika dimbwi la umaskini uliotopea.

Kwa waliosahau au kutoelewa ni kuwa mzee wetu huyu hapo mwakani panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu atatimiza miaka mia moja yaani karne moja.jambo ambalo kiukweli kufikisha umri huo hapa Duniani ni lazima umshukuru Mungu na kusema imekuwa hivyo kwa neema tu ya Mungu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Mungu ampe wepesi mzee wetu.

Lakini Lucas Mwashambwa, mbali na kuwa chawa, wewe ni msemaji wa Serikali? Mbona una kimbelembele sana?
 
Pamoja na mapungufu yao. Lakini ubinadamu wao unapaswa kutunzwa kama namna ambavyo sisi tunavyotaka kuheshimiwa kama watu.

Tusivuke mipaka sana ya utu. Tukatae matendo yao lakini tuhwshimu na kuenzi utu
Watoto wa Mwinyi wengine tumewakaribisha kutoka Zanzibar, tumesoma nao vizuri, tumekuwa marafiki wakiwa watu wa kawaida sana mpaka tukawa tunatilia shaka kama hawa ni watoto wa rais kweli au tunadanganywa tu, kwa jinsi walivyoishi maisha ya kawaida.

Ni wazi walilelewa kwa maadili ya kuthamini utu wa watu kuliko kujiona wao watoto wa rais.

Kwa hivyo huyu Mzee unaweza kumuangalia kama "Mzee Ruksa" Mwinyi ex president, lakini watu wengine huyu ni mzazi wa rafiki tuliyeishi naye vizuri kwa heshima kubwa.

Hivyo tuangalie hilo pia.

Sio kila kitu siasa.
 
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi amepelekwa hospitali akiugua maradhi ya kifua. Anaendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Kutokana na ushauri wa madaktari wake, familia imeona ni vyema apate faragha akiwa anapatiwa matibabu. Hivyo Familia inaiomba jamii kumkumbuka kwenye Dua, Sala, na Maombi.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie shifaa ya haraka Mzee wetu pamoja na wagonjwa wengine wote wanaokabiliwa na maradhi mbali mbali.

Abdullah Ali Mwinyi
Msemaji wa Familia
Wakutanikapo tai ndipo mzoga ungalipo
 
Back
Top Bottom