Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akishuhudia Sherehe ya Utiaji Saini Mkataba wa SGR LOT 6 (Tabora - Kigoma) katika Ukumbi wa Kikwete Hall - Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 20 Desemba, 2022.
Utiaji saini huo utahusisha kati ya Serikali kupitia Shirika la Reli na Kampuni za ubia wa CCECC na CRCC kutoka China.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla anazungumza:
Hali ya usalama ni shwari, nashukuru kwa Shilingi Bilioni 12.3 ulizotupa za kujenga madarasa 618, nikuhakikishe hakuna mtoto ambaye hatakwenda shule
Dar ndio Jiji la kibiashara, sisi ni wanufaika wa kwanza wa mradi wa SGR, hivi karibuni ulinipa fursa ya Kwenda kuifunza mambo ya usafi Rwanda, wanakushukuru kwa kufungua biashara.
Unayoyafanya yameandikwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi, chama cha siasa kazi yake ni kushika dola, unayoyafanya unatekeleza kile kilichopo kwenye ilani.
Ukishaona mtu mzima anacheza michezo ya kitoto kwa mfano ‘hide and see’ au kujipikilisha ujue mambo sio mazuri, juzi tumesikia wenzetu wanachagua Bunge la Mtandao, linaitwa Bunge na lina Spika, sasa hapo tunaona kabisa wanacheza mchezo wa hide and see, wamechanganyikiwa, hii ni kutokana na kazi nzuri unayofanya.
Masanja Kadogosa, Mkurugenzi wa TRC anazungumza:
Utiaji Saini huu wa leo unafanya utimilifu wa reli ya kati, kutoka Dar- Mwanza na Dar-Kigoma, kwingine kote kutakapofuata ni reli za matawi
Mheshimiwa Rais ulisema tuanze kujenga reli kuelekea DRC kwa kuwa tusipofanya hivyo wenzetu watajenga
Kwa ujenzi huu wa jumla wa kilometa 2102 unaifanya Tanzania kuwa Nchi yenye ujenzi wa SGR ndefu kuliko zote Afrika.
Reli ya SGR itaunganisha bandari ya Dar, DRC kupitia bandari ya Kigoma, hivyo katika miji mikubwa ndani ya DRC tutakuwa tumefikia miji mitatu yenye idadi kubwa ya watu, hiyo ni fursa kwa wafanyabiashara.
Ujenzi wa Tabora-Kigoma una kilometa 506, tutakuwa na station 10, vituo vikubwa vya miziko Uvinza na Katosho.
Thamani ya mkataba ni Dola bilioni 2.21 bila kodi, ukijumuisha kodi inakuwa Dola bilioni 2.7 sawa na Tsh. Trilioni 6.34 na ujenzi huu unatarajiwa kutuchukua miezi 48.
Kwa kusaini kipande hiki, Serikali itakuwa imewekeza Dola Bilioni 10.04, sawa na Tsh, Trilioni 23.3 kwa maana ya awamu ya Dar-Mwanza na Tabora-Kigoma.
Mikataba yote tuliyosaini haitakuwa na mabadiliko ya bei, mfano bei ya vitu vya ujenzi ikibadilika na bei ibadilike, hiyo haitakuwepo. Kama tukekubali hilo inamaanisha kuwa kungekuwa na nyongeza ya zaidi ya Dola Bilioni 1.304.
Hii inamaana kungekuwa na ongezeko la 30.3%, kwa maana ya thamani ya fedha.
Serikali inaendelea na ununuzi wa vitendea kazi, tumenunua mabehewa 59, ambapo tayari mabehewa 14 mapya yameingia, kuna mabehewa 30 na vichwa viwili 'used' vitaingia Machi – Aprili 2023.
Tulikuwa na matatizo na msambazaji wa kwanza wa Uturuki, tuliamua kuvunja mkataba baada ya kushauriana Serikalini, tukampa mtu mwingine aliye Ujerumani kwa ajili ya kumalizia kazi, tulifanya maamuzi hayo kwa nia njema.
Pia tuna vichwa vya treni 17 kutoka Korea Kusini, vitaanza kuingia Juni 2023, tuna seti 10 ya treni za kisasa (EMU), ambapo seti mbili za kwanza zinaingia Juni 2023.
Tuna mabehewa ya mizigo 1430 kutoka China, yataingia Nchini Septemba 2023, kuna vifaa kutoka Korea Kusini, hivyo uwekezaji huu kwa jumla unafanya kuwa na thamani ya jumla Dola milioni 557.731 sawa na Tsh. Trilioni 1.29
Niweke wazi pia tenda ya ununuzi ilitangazwa mara mbili lakini hatukupata mtu wa uhakika, tukaamua kwenda kwa mzalishaji moja kwa moja.
Kuna kampuni kutoka Urusi, Korea Kusini, Japan, Ujerumani, Uholanzi, Malaysia ambazo zilifuata taratibu zote na mwisho tukapata 'lowest evaluated bidder' lakini kwa kujali ubora na kujali mahitaji yetu tuliyowaambia.
Hivyo, yanayozungumzwa kuhusu bei ni mambo ya mitandaoni tu.
Pamoja na ujenzi wa miundombinu, TRC kwa kushirikiana na TANESCO tunajenga line ya umeme wa kujitegemea, kwa maana tutakuwa na line ya kwetu haitaingiliana na line yoyote kwa ajili ya kupata umeme wa uhakika.
Tunafurahi kwa kuwa ndani ya siku mbili hizi tutakuwa na mchakato wa kujaza maji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere, na sisi tutaenda.
Rais Samia Suluhu Hassan anazungumza:
Namshukuru Mungu kutupa idhini ya kukutana hapa kushuhudia utiaji saini kati ya TRC na kampuni zilizotajwa za kichina, na tuombe Mungu atupe idhini ya kushuhudia kukamilika kwa mradi huu.
Mabehewa tumeyaona na mengine tumeambiwa yanakuja. Hii inafanya gharama za uwekezaji kufikia Bilioni 10.04. Fedha hizo zote ni mikopo, wanaosema awamu hii imekopa sana, waseme pia awamu hii imejenga sana, wasijifanye kama wanaume wa kiislamu, Quran inaruhusu waoe wanawake wanne lakini hawaendelei mbele kusoma inasemaje?
Mfano mwezi huu kuna vijimaneno serikalini hakuna pesa, ni kweli. Mikopo imechelewa kuja, na mikopo miwili ime mature kwa pamoja ilibidi tulipe.
Mikopo hii lazima tulipe, huo ndiyo uungwana. Kuna wakati tutaomba msamaha, bado hatujawa wa kuomba msamaha. Lazima tulipe.
Uvinza kwenda msongati kwenye nickel napo mambo yakiwa tayari tutasaini.
Ndugu wananchi, serikali kwa upande wake itaendelea kujenga miradi hii ya kimkakati ili kuendelea kukuza uchumi. Uwekezaji unakwenda pande zote, kwenye SGR pia tunafufua reli za zamani ili kuunganisha bandari zote na reli zote.
Lengo la serikali ni kufanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara. Nawataka wote wanaohusika na usimamanizi wa ujenzi wa miradi hii kufanya wajibu wao kama inavyotakiwa.
Mradi huu wa SGR umetoa ajira zaidi ya watu 20,000, pia serikali imekusanya kodi bilioni 949 kutoka local content.
Tanzania tumewekwa pahali pazuri na Mwenyezi Mungu, tuna bahari, maziwa makubwa, mito na nchi yetu inapakana na nchi 8. Nataka kusisitiza kwamba fursa hii haiwezi kunufaisha taifa kama hatutaitumia vyema. Tutumie fursa yety hii kijografia.
Niendelee kuitaka wizara, bodi ya wakurugenzi na TRC kuendelea kusimamia miradi hii ikamilike kwa wakati unaotakiwa.
Tumeoneshwa mabehewa hapa, hata kama ya kukarabati, si mabehewa yanayotumika sasa hivi. Niliwahi kupanda treni daraja la kwanza, mabehewa hayo siyo hata hadhi ya tatu ya mabehewa ya sasa. Niwaahidi kwamba serikali yenu tutaendelea kufanya mambo mazuri zaidi.
Nawashukuru, namuomba Mungu aibariki nchi yetu.
Utiaji saini huo utahusisha kati ya Serikali kupitia Shirika la Reli na Kampuni za ubia wa CCECC na CRCC kutoka China.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla anazungumza:
Hali ya usalama ni shwari, nashukuru kwa Shilingi Bilioni 12.3 ulizotupa za kujenga madarasa 618, nikuhakikishe hakuna mtoto ambaye hatakwenda shule
Dar ndio Jiji la kibiashara, sisi ni wanufaika wa kwanza wa mradi wa SGR, hivi karibuni ulinipa fursa ya Kwenda kuifunza mambo ya usafi Rwanda, wanakushukuru kwa kufungua biashara.
Unayoyafanya yameandikwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi, chama cha siasa kazi yake ni kushika dola, unayoyafanya unatekeleza kile kilichopo kwenye ilani.
Ukishaona mtu mzima anacheza michezo ya kitoto kwa mfano ‘hide and see’ au kujipikilisha ujue mambo sio mazuri, juzi tumesikia wenzetu wanachagua Bunge la Mtandao, linaitwa Bunge na lina Spika, sasa hapo tunaona kabisa wanacheza mchezo wa hide and see, wamechanganyikiwa, hii ni kutokana na kazi nzuri unayofanya.
Masanja Kadogosa, Mkurugenzi wa TRC anazungumza:
Utiaji Saini huu wa leo unafanya utimilifu wa reli ya kati, kutoka Dar- Mwanza na Dar-Kigoma, kwingine kote kutakapofuata ni reli za matawi
Mheshimiwa Rais ulisema tuanze kujenga reli kuelekea DRC kwa kuwa tusipofanya hivyo wenzetu watajenga
Kwa ujenzi huu wa jumla wa kilometa 2102 unaifanya Tanzania kuwa Nchi yenye ujenzi wa SGR ndefu kuliko zote Afrika.
Reli ya SGR itaunganisha bandari ya Dar, DRC kupitia bandari ya Kigoma, hivyo katika miji mikubwa ndani ya DRC tutakuwa tumefikia miji mitatu yenye idadi kubwa ya watu, hiyo ni fursa kwa wafanyabiashara.
Ujenzi wa Tabora-Kigoma una kilometa 506, tutakuwa na station 10, vituo vikubwa vya miziko Uvinza na Katosho.
Thamani ya mkataba ni Dola bilioni 2.21 bila kodi, ukijumuisha kodi inakuwa Dola bilioni 2.7 sawa na Tsh. Trilioni 6.34 na ujenzi huu unatarajiwa kutuchukua miezi 48.
Kwa kusaini kipande hiki, Serikali itakuwa imewekeza Dola Bilioni 10.04, sawa na Tsh, Trilioni 23.3 kwa maana ya awamu ya Dar-Mwanza na Tabora-Kigoma.
Mikataba yote tuliyosaini haitakuwa na mabadiliko ya bei, mfano bei ya vitu vya ujenzi ikibadilika na bei ibadilike, hiyo haitakuwepo. Kama tukekubali hilo inamaanisha kuwa kungekuwa na nyongeza ya zaidi ya Dola Bilioni 1.304.
Hii inamaana kungekuwa na ongezeko la 30.3%, kwa maana ya thamani ya fedha.
Serikali inaendelea na ununuzi wa vitendea kazi, tumenunua mabehewa 59, ambapo tayari mabehewa 14 mapya yameingia, kuna mabehewa 30 na vichwa viwili 'used' vitaingia Machi – Aprili 2023.
Tulikuwa na matatizo na msambazaji wa kwanza wa Uturuki, tuliamua kuvunja mkataba baada ya kushauriana Serikalini, tukampa mtu mwingine aliye Ujerumani kwa ajili ya kumalizia kazi, tulifanya maamuzi hayo kwa nia njema.
Pia tuna vichwa vya treni 17 kutoka Korea Kusini, vitaanza kuingia Juni 2023, tuna seti 10 ya treni za kisasa (EMU), ambapo seti mbili za kwanza zinaingia Juni 2023.
Tuna mabehewa ya mizigo 1430 kutoka China, yataingia Nchini Septemba 2023, kuna vifaa kutoka Korea Kusini, hivyo uwekezaji huu kwa jumla unafanya kuwa na thamani ya jumla Dola milioni 557.731 sawa na Tsh. Trilioni 1.29
Niweke wazi pia tenda ya ununuzi ilitangazwa mara mbili lakini hatukupata mtu wa uhakika, tukaamua kwenda kwa mzalishaji moja kwa moja.
Kuna kampuni kutoka Urusi, Korea Kusini, Japan, Ujerumani, Uholanzi, Malaysia ambazo zilifuata taratibu zote na mwisho tukapata 'lowest evaluated bidder' lakini kwa kujali ubora na kujali mahitaji yetu tuliyowaambia.
Hivyo, yanayozungumzwa kuhusu bei ni mambo ya mitandaoni tu.
Pamoja na ujenzi wa miundombinu, TRC kwa kushirikiana na TANESCO tunajenga line ya umeme wa kujitegemea, kwa maana tutakuwa na line ya kwetu haitaingiliana na line yoyote kwa ajili ya kupata umeme wa uhakika.
Tunafurahi kwa kuwa ndani ya siku mbili hizi tutakuwa na mchakato wa kujaza maji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere, na sisi tutaenda.
Rais Samia Suluhu Hassan anazungumza:
Namshukuru Mungu kutupa idhini ya kukutana hapa kushuhudia utiaji saini kati ya TRC na kampuni zilizotajwa za kichina, na tuombe Mungu atupe idhini ya kushuhudia kukamilika kwa mradi huu.
Mabehewa tumeyaona na mengine tumeambiwa yanakuja. Hii inafanya gharama za uwekezaji kufikia Bilioni 10.04. Fedha hizo zote ni mikopo, wanaosema awamu hii imekopa sana, waseme pia awamu hii imejenga sana, wasijifanye kama wanaume wa kiislamu, Quran inaruhusu waoe wanawake wanne lakini hawaendelei mbele kusoma inasemaje?
Mfano mwezi huu kuna vijimaneno serikalini hakuna pesa, ni kweli. Mikopo imechelewa kuja, na mikopo miwili ime mature kwa pamoja ilibidi tulipe.
Mikopo hii lazima tulipe, huo ndiyo uungwana. Kuna wakati tutaomba msamaha, bado hatujawa wa kuomba msamaha. Lazima tulipe.
Uvinza kwenda msongati kwenye nickel napo mambo yakiwa tayari tutasaini.
Ndugu wananchi, serikali kwa upande wake itaendelea kujenga miradi hii ya kimkakati ili kuendelea kukuza uchumi. Uwekezaji unakwenda pande zote, kwenye SGR pia tunafufua reli za zamani ili kuunganisha bandari zote na reli zote.
Lengo la serikali ni kufanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara. Nawataka wote wanaohusika na usimamanizi wa ujenzi wa miradi hii kufanya wajibu wao kama inavyotakiwa.
Mradi huu wa SGR umetoa ajira zaidi ya watu 20,000, pia serikali imekusanya kodi bilioni 949 kutoka local content.
Tanzania tumewekwa pahali pazuri na Mwenyezi Mungu, tuna bahari, maziwa makubwa, mito na nchi yetu inapakana na nchi 8. Nataka kusisitiza kwamba fursa hii haiwezi kunufaisha taifa kama hatutaitumia vyema. Tutumie fursa yety hii kijografia.
Niendelee kuitaka wizara, bodi ya wakurugenzi na TRC kuendelea kusimamia miradi hii ikamilike kwa wakati unaotakiwa.
Tumeoneshwa mabehewa hapa, hata kama ya kukarabati, si mabehewa yanayotumika sasa hivi. Niliwahi kupanda treni daraja la kwanza, mabehewa hayo siyo hata hadhi ya tatu ya mabehewa ya sasa. Niwaahidi kwamba serikali yenu tutaendelea kufanya mambo mazuri zaidi.
Nawashukuru, namuomba Mungu aibariki nchi yetu.