mwanamichakato
JF-Expert Member
- Mar 20, 2015
- 895
- 707
Rais umefanya mema na mazuri kupitia uongozi wako. Mungu mtakatifu ana kusudi la kukupa nafasi kuu ktk nchi yetu ktk mazingira uliopewa si Kwa mapenzi ya wanadamu Bali Mungu tu..Si Kwa wewe kutaka Bali neema tu.
Wengi sana walijitokeza (Watangaza nia)ili kupewa kijiti cha kupeperusha bendera ya CCM..Walilipa fedha, Walizunguka nchi nzima wakijinadi Kwa wanachama (Wajumbe) na wananchi. Mwenyezi Mungu hakuwapa nafasi kupitia michakato mbalimbali ya Chama na kitaifa..
Ilimpendeza Mungu Hayati JPM awe kiongozi Mkuu wa taifa hili tajiri na wewe kuwa Msaidizi wake au makamu wake. Mungu alimpangia Siku,saa,mazingira ya kutwaliwa ktk mwili..Mwili wake umefariki huku roho yake ikisubiri hukumu Kama ilivyo Kwa wanadamu wote Kwa mujibu wa maandiko..
Yamkini nia na makusudi ni njema kabisa Kwa mujibu wa upembuzi wa viongozi wetu haswaa ktk kukuletea taifa tija Kina endelea ELIMU, AFYA, MIUNDOMBINU, N.K. Kwa lilivyo hili jambo sio jepesi ni zito mnoo. Limeenea mnoo..Lina ukakasi mnoo,Halina amani. Halina furaha. Halina utulivu. Linachakata mioyo, roho, fahamu Za wananchi maskini, wenye kipato cha kati na wasomi (Elimu bure imeleta effect ktk fikra)..
Viongozi wetu, Mitihani ktk maisha ya Uongozi haina budi kuruhusiwa kuwapata..Fanyeni toba Kwa Mwenyezi Mungu. Ombeni hekima na busara. Fanyeni maamuzi magumu yenye kuleta amani,Utulivu na mshikamano..
Kwa Heshima na unyenyekevu mkubwa nikuombe Mh Rais ikikupendeza hutubia taifa Kwa muda utakaokufaa na Utoe ufafanuzi wa mapana,Omba radhi kwenye mapungufu, Elimisha itakapobidi,Wajibisha wanaopaswa kuwajibishwa ,Toa dira mahsusi, Kemea uzembe wote (Watumishi na Viongozi wote wa umma hutenda kazi Kwa niaba yako Mh Rais,..Huwezi kufika kila mahali. Huwezi soma kila kitu,Huwezi fuatilia kila jambo..Huwezi saini kila nyaraka.
Mwisho usisahau kuwasamehe wote wate waliokukosea,Kukuudhi,Kuumiza moyo,na kukukwaza sana ktk kipindi hiki..Ni mtihani kwako. Mwenyezi Mungu anatusamehe makosa yetu tunaposamehe wengine wanaotukosea.
Kwa kuwa watendaji wako na wasaidizi wako ni binadamu hivyo wana mapungufu Kwa namna moja au nyingine hivyo hawawezi kuwa sahihi Kwa kila jambo Kwa kuzingatia changamoto za kimazingira, elimu, Utandawazi na mengineo.
Nina imani Watanzania wana imani na uongozi wako na jitihada zote ufanyazo ktk kuimarisha na kujenga umoja wa kitaifa. Kwa hotuba yako mjadala utakoma na mengi mema yako na serikali yatatamalaki zaidi..
Wengi sana walijitokeza (Watangaza nia)ili kupewa kijiti cha kupeperusha bendera ya CCM..Walilipa fedha, Walizunguka nchi nzima wakijinadi Kwa wanachama (Wajumbe) na wananchi. Mwenyezi Mungu hakuwapa nafasi kupitia michakato mbalimbali ya Chama na kitaifa..
Ilimpendeza Mungu Hayati JPM awe kiongozi Mkuu wa taifa hili tajiri na wewe kuwa Msaidizi wake au makamu wake. Mungu alimpangia Siku,saa,mazingira ya kutwaliwa ktk mwili..Mwili wake umefariki huku roho yake ikisubiri hukumu Kama ilivyo Kwa wanadamu wote Kwa mujibu wa maandiko..
Yamkini nia na makusudi ni njema kabisa Kwa mujibu wa upembuzi wa viongozi wetu haswaa ktk kukuletea taifa tija Kina endelea ELIMU, AFYA, MIUNDOMBINU, N.K. Kwa lilivyo hili jambo sio jepesi ni zito mnoo. Limeenea mnoo..Lina ukakasi mnoo,Halina amani. Halina furaha. Halina utulivu. Linachakata mioyo, roho, fahamu Za wananchi maskini, wenye kipato cha kati na wasomi (Elimu bure imeleta effect ktk fikra)..
Viongozi wetu, Mitihani ktk maisha ya Uongozi haina budi kuruhusiwa kuwapata..Fanyeni toba Kwa Mwenyezi Mungu. Ombeni hekima na busara. Fanyeni maamuzi magumu yenye kuleta amani,Utulivu na mshikamano..
Kwa Heshima na unyenyekevu mkubwa nikuombe Mh Rais ikikupendeza hutubia taifa Kwa muda utakaokufaa na Utoe ufafanuzi wa mapana,Omba radhi kwenye mapungufu, Elimisha itakapobidi,Wajibisha wanaopaswa kuwajibishwa ,Toa dira mahsusi, Kemea uzembe wote (Watumishi na Viongozi wote wa umma hutenda kazi Kwa niaba yako Mh Rais,..Huwezi kufika kila mahali. Huwezi soma kila kitu,Huwezi fuatilia kila jambo..Huwezi saini kila nyaraka.
Mwisho usisahau kuwasamehe wote wate waliokukosea,Kukuudhi,Kuumiza moyo,na kukukwaza sana ktk kipindi hiki..Ni mtihani kwako. Mwenyezi Mungu anatusamehe makosa yetu tunaposamehe wengine wanaotukosea.
Kwa kuwa watendaji wako na wasaidizi wako ni binadamu hivyo wana mapungufu Kwa namna moja au nyingine hivyo hawawezi kuwa sahihi Kwa kila jambo Kwa kuzingatia changamoto za kimazingira, elimu, Utandawazi na mengineo.
Nina imani Watanzania wana imani na uongozi wako na jitihada zote ufanyazo ktk kuimarisha na kujenga umoja wa kitaifa. Kwa hotuba yako mjadala utakoma na mengi mema yako na serikali yatatamalaki zaidi..