Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,810
- 11,979
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki Jubilei ya Miaka 50 ya Utume na Huduma ya Kanisa la Waadventista wa Sabato leo Tarehe 19 Novemba, 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma
SAMIA SULUHU HASSAN - RAIS
Kwanini hajawahi kuhudhuria Mwaliko wa Kanisa hili kabla.
Kama mnavyojua nimekuwa nahudhuria mikutano mingi ya kidini, lakini sikuwa na bahati ya kukutana na waadiventista wa sabato.
Leo kwa ajili ya tukio hili muhimu nimepata nafasi hiyo, ni baraka na neema ya kipekee kwangu. Mwenyezi Mungu awabariki kwa ukarimu wenu.
Kwanini kaamua kuhudhuria Jubilei hii mapema asubuhi?
Nataka niruke niende kwenye majukumu Mengine huko Zanzibar, samahani kwa kuwaita mapema. Kama mnavyojua tumeita mabalozi wote wanaotuwakilisha dunia nzima, ili tuzungumze nao, tutoe sera na mwelekeo halafu tuwape ruhusa wakafanye kazi. Kwahiyo nimewaambia mabalozi subiribi nina shughuli nyingine asubuhi. Na nimefanya hivyo sababu Sikutaka kukosa baraka hizi, kwani baraka za Bwana ni za kung’ang’ania. Si mnafahamu Yakobo alivyomng’ang’ania malaika? Na akasema hatamuacha mpaka ambariki.
Nawashukuru kwa maombi yenu kwa serikali na nchi yetu, tumedumu katika umoja, amani na mshikamano.
Jambo linalonifurahisha kwenye makongamano haya ni namna mnavyowalea vijana wakue katika maadili mema. Hili ni jambo jema sana, mnasaidia serikali. Bila vijana waadilifu ingekuwa kazi kubwa sana kwa magereza, polisi na majaji. Nawashukuru kwa malezi na kukuza vijana wazalendo wema kwa taifa.
Akijibu maombi yaliyoelekezwa Kwake.
Nimesikia suala la mitihani na usaili kufanyika jumamosi ambayo ni siku ya ibada. Nilikuwa namtania baba Askofu, nikamwambia sasa kama mtu anaitwa kwenye usaili jumamosi au anafanya mtihani, anakwenda amemshiba Yesu Kristo moyoni, siku takatifu, hiyo ni dalili tosha kuwa huyo anayeenda siku hiyo anaenda kufaulu. Iwe usaili au mtihani, anakwenda kufaulu. Kwa hiyo hili la kusema jumamosi wasifanye mtihani au interview tutaliangalia vizuri, lakini naona kama waende na waende na ule moyo wa “nakwenda na nguvu za yesu” na watakwenda kushinda.
Kuhusu kufutiwa kodi kwa taasisi zinazohusika na elimu za kanisa ili kurahisisha utoaji wa huduma, uhitaji wa Madaktari bingwa kwenye hospitali zenu na kutambulika Serikalini kwa kanisa kuwa linajitegemea na halipo chini ya mwamvuli wowote wa umoja wa madhehebu ya Kikiristo kama vile CCT , TEC na CPCT.
Niseme kuwa baadhi ya maombi yanaweza kupatiwa majibu ya haraka na mengine yanahitaji majadiliano ya kina na wenzangu Serikalini. Maombi yote nimeyabeba na tutafanyia kazi, tutawapa mrejesho baada ya mashauriano na wenzangu Serikalini.
Kuhusu kutunza mazingira.
Tuendelee kutunza mazingira na vyanzo vya maji, kwa kiasi kikubwa adhabu tunayopata leo ni sababu tumeharibu mazingira. Tumeshuhudia makundi makubwa ya ng’ombe yanahama hama kutafuta vyanzo vya maji. Ng’ombe 2000-3000 wanavamia mto, ng’ombe mmoja anakunywa lita 45, ng’ombe 3000 watakunywa lita ngapi?
Miti inayokatwa miaka na miaka matokeo yake tunayaona leo, tuna upungufu wa vyanzo vya maji. Maji ni uhai, tunapokosa maji uhai unakuwa mashakani. Tupande miti kwa wingi ili turudishe hali tuliyo iharibu.
Maneno ya kufunga.
Bila neema ya Mwenyezi Mungu, sisi binadamu hatuwezi kitu. Nawatakia wote neema na baraka za Mwenyezi Mungu.
SAMIA SULUHU HASSAN - RAIS
Kwanini hajawahi kuhudhuria Mwaliko wa Kanisa hili kabla.
Kama mnavyojua nimekuwa nahudhuria mikutano mingi ya kidini, lakini sikuwa na bahati ya kukutana na waadiventista wa sabato.
Leo kwa ajili ya tukio hili muhimu nimepata nafasi hiyo, ni baraka na neema ya kipekee kwangu. Mwenyezi Mungu awabariki kwa ukarimu wenu.
Kwanini kaamua kuhudhuria Jubilei hii mapema asubuhi?
Nataka niruke niende kwenye majukumu Mengine huko Zanzibar, samahani kwa kuwaita mapema. Kama mnavyojua tumeita mabalozi wote wanaotuwakilisha dunia nzima, ili tuzungumze nao, tutoe sera na mwelekeo halafu tuwape ruhusa wakafanye kazi. Kwahiyo nimewaambia mabalozi subiribi nina shughuli nyingine asubuhi. Na nimefanya hivyo sababu Sikutaka kukosa baraka hizi, kwani baraka za Bwana ni za kung’ang’ania. Si mnafahamu Yakobo alivyomng’ang’ania malaika? Na akasema hatamuacha mpaka ambariki.
Nawashukuru kwa maombi yenu kwa serikali na nchi yetu, tumedumu katika umoja, amani na mshikamano.
Jambo linalonifurahisha kwenye makongamano haya ni namna mnavyowalea vijana wakue katika maadili mema. Hili ni jambo jema sana, mnasaidia serikali. Bila vijana waadilifu ingekuwa kazi kubwa sana kwa magereza, polisi na majaji. Nawashukuru kwa malezi na kukuza vijana wazalendo wema kwa taifa.
Akijibu maombi yaliyoelekezwa Kwake.
Nimesikia suala la mitihani na usaili kufanyika jumamosi ambayo ni siku ya ibada. Nilikuwa namtania baba Askofu, nikamwambia sasa kama mtu anaitwa kwenye usaili jumamosi au anafanya mtihani, anakwenda amemshiba Yesu Kristo moyoni, siku takatifu, hiyo ni dalili tosha kuwa huyo anayeenda siku hiyo anaenda kufaulu. Iwe usaili au mtihani, anakwenda kufaulu. Kwa hiyo hili la kusema jumamosi wasifanye mtihani au interview tutaliangalia vizuri, lakini naona kama waende na waende na ule moyo wa “nakwenda na nguvu za yesu” na watakwenda kushinda.
Kuhusu kufutiwa kodi kwa taasisi zinazohusika na elimu za kanisa ili kurahisisha utoaji wa huduma, uhitaji wa Madaktari bingwa kwenye hospitali zenu na kutambulika Serikalini kwa kanisa kuwa linajitegemea na halipo chini ya mwamvuli wowote wa umoja wa madhehebu ya Kikiristo kama vile CCT , TEC na CPCT.
Niseme kuwa baadhi ya maombi yanaweza kupatiwa majibu ya haraka na mengine yanahitaji majadiliano ya kina na wenzangu Serikalini. Maombi yote nimeyabeba na tutafanyia kazi, tutawapa mrejesho baada ya mashauriano na wenzangu Serikalini.
Kuhusu kutunza mazingira.
Tuendelee kutunza mazingira na vyanzo vya maji, kwa kiasi kikubwa adhabu tunayopata leo ni sababu tumeharibu mazingira. Tumeshuhudia makundi makubwa ya ng’ombe yanahama hama kutafuta vyanzo vya maji. Ng’ombe 2000-3000 wanavamia mto, ng’ombe mmoja anakunywa lita 45, ng’ombe 3000 watakunywa lita ngapi?
Miti inayokatwa miaka na miaka matokeo yake tunayaona leo, tuna upungufu wa vyanzo vya maji. Maji ni uhai, tunapokosa maji uhai unakuwa mashakani. Tupande miti kwa wingi ili turudishe hali tuliyo iharibu.
Maneno ya kufunga.
Bila neema ya Mwenyezi Mungu, sisi binadamu hatuwezi kitu. Nawatakia wote neema na baraka za Mwenyezi Mungu.