Rais Samia: Serikali imempatia Mzee Mwinyi zawadi ya gari aina ya Benz ya chini

Gari aliopewe Mstaafu mwinyi Mercedes Benz haizidi hata milioni 100, ila nimeamini watu wanapenda kukuza mambo... na amepewa kwasababu mheshimiwa Rais ameona Mstaafu mwinyi anashindwa kuhudhuria hafla nyingi kutokana gari anayotumia kwasasa ni V8 inampa tabu kupanda kutokana na uzee.. Hivyo ameona si haba akamalizia maisha kwenye Benz saloon...
Kwani yeye mwinyi hana hiyo hela ya kununua Benz? Au hajui km anatakiwa kununua Benz imrahisishie ufasiri? Mambo mengine yanakera sana.
 
Mkuu gharama ya Hilo Benz Ni kituo cha afya kimoja chenye kila kitu ndani anapewa mtu mmoja kweli ?
Kama ametoa mfukoni mwake mbona. Haina shida ila Kama amtoa KWA walipa kodi Kuna shida,sababu babu ni mstahafu na kodi za watanzania zinaendelea kumhudumia na Kama haitoshi katika dunia ni marais wachache waliowai stahafu wakaishi maisha ya kifukara but Afrika sidhani Kama yupo tofauti na mwalim nyerere, so KWA KUA mwalim hayupo ila mama nyenyere yupo Basi Kama ni KWA hisan ya wananchi Basi Mama nyerere nae apewe benz labda Kama mh katoa mfukoni mwake vinginevyo moto kuwaka lazima ,tunasema hakuna Alie zaidi ya mwenzake katika taifa hili japo ni madaraka tu kwamba Kuna Rais na mwananchi ambae ndo mwajiri basi
 
Nadhani watu hawafuatilii.....yaani mama si mnunuzi wa gari bali mama ni mkabidhi wa zawadi.....
 
Kituo kimoja Cha Afya kinagharim Ml 400. Hii inajumuisha ujenzi was majengo 5 ambayo ni Jengo la Mama na mtoto(martenity ward), OPD, Maabara, Labor ward na Makazi ya Mgangu Mkuu.

Hivyo, Mwinyi amepewa Kituo Cha Afya Kimoja akaongezwa na Zahanati moja. Hii ingewezwa kujengwa kwa Wananchi wa Kijijini
 
Kwamba Hussein hawezi kumnunulia babake personally mzigo wa 450mil? Kweli aliyenacho huongezewa
 
Huyu Mzee Ali Hassan Mwinyi hata angepewa magari 5 kama hayo Mimi naona sawa tu. Kwa wenye umri wa miaka zaidi ya 45 watakumbuka kuwa huyu Mzee Mwinyi kwa kipindi cha 1985-1995 ndiye aliyefanya maamuzi makubwa sana kutuvusha kutoka kwenye lindi la umaskini uliokithiri.

Akiba ya fedha za kigeni baada ya Vita vya Uganda iliteremka, nchi ilikuwa haikopesheki na maahirika ya fedha kimataifa, Watanzania walikuwa wanakula mchele wa msaada wa kitumbo, unga wa yanga. Halafu vyote hivyo unavipata kwa foleni. Huko Mtwara wananchi walikuwa wanavaa mifuko ya visulphate kama mashati.

Mwinyi ndiye aliyeruhusu biashara huria, kuanzishwa kwa daladala, kuingizwa kwa mitumba kutoka Ulaya. Akaruhusu watu wafanye biashara mbali mbali.

Hata privatization ya maahirika Kama TBL na TCC ilianzia kipindi chake na uanzishwai wa TRA.

Muache babu afaidi nchi aliyosaidia kuijenga
 
Inachezewa sana kivipi we jamaa.. Mbona unakuwa na roho ya kimaskini sana?

Zawadi ya Ml 450 kwa mtu alie simamia ustawi wa taifa letu.. tena ukiangalia hata kwenye baadhi ya sarafu kuna sura yake hiyo tsh ml 450 bado ni ndogo sana Ndugu yangu
Mwanae pia n Rais angeweza kumnunulia.
 
Kama miaka 60 ya uhuru wetu bado hatujawahi kupata kiongozi bora kwa taifa hili, basi taifà halina watú bora. It's as simple as that, tusiendelee kulalamika, whether ni akili za kurithi, utapiamlo ama lishe duni, hatuwezi kulalamika tena. Taifa halina watu wenye uwezo...basi tena!
 
Majuzi hapa Magufuli kamjengea Mzee Mwinyi bonge la "Hekalu"

Leo Samia anatoa Zawadi ya Benz la Mamilioni

Hivi haya Mambo ndo yanatatua shida na kero za wananchi au?

Mwinyi ana pensheni ya Mamilioni ya fedha, Mwanae ni rais, watoto wake ni wabunge, Hivi bado anahitaji Mihela yote hiyo kodi za wananchi masikini kwa ajili ya mavituvitu kama hayo?

Naona tumeanza kutumia fedha za wananchi kama pesa za familia. Mambo ya ajabu sana haya!
You are begrudging a 96 year old man getting a car that he can conveniently use?
 
Ameshaanza na yeye kulewa madaraka. Kuna ulazima gani wa kumnunulia mzee mstaafu gari la mamilioni yote hayo ya shilingi na huku kuna changamoto lukuki kwa Watanzania maskini?

Yaani milioni 450 kirahisi tu!! Kuna ulazima wa kuiondoa ccm madarakani. Haya mambo ya kuchezea kodi zetu miaka nenda, yanachosha.
Yaani dah!
 
Inachezewa sana kivipi we jamaa.. Mbona unakuwa na roho ya kimaskini sana?

Zawadi ya Ml 450 kwa mtu alie simamia ustawi wa taifa letu.. tena ukiangalia hata kwenye baadhi ya sarafu kuna sura yake hiyo tsh ml 450 bado ni ndogo sana Ndugu yangu
Ashakula ngapi mzee? Bado tu ale?
 
Back
Top Bottom