Rais Samia: Serikali imempatia Mzee Mwinyi zawadi ya gari aina ya Benz ya chini

Watoto tu wa nyerere ndomana mpaka leo wanakula good time,ndomana hata kufanya kazi hawataki...mpunga wanaingiziwa,matatizo yao wanatatuliwa

Ova
Mbna hawapewi km hawa wengine, watoto wa nyerere wenyewe wamesahaulika.
 
Mbna hawapewi km hawa wengine, watoto wa nyerere wenyewe wamesahaulika.
Wanapewa huduma zote wale
Wenyewe akili zao wanazijua wenyw
We hujiulizi watoto wake yuko rubani
Yuko aliyesomea masuala ya fedha alipewa ajira bot,akaiachaa mwenyewe
Kuna mmoja hapo yeye kaamua kuwa kuwatembeza wageni wakienda butiama anakuonesha nyumba ya milele ya mzee
Ila hao serikali inawangalia mpk keshoo

Ova
 
Ninadhani ukisoma Political Service Retirement Benefit. Inatoa utaratibu kwa viongozi wa juu wa nchii hii kuhudumia baada ya kukoma kutumikia nyadhifa zao. Viongozi ambao ni Rais Mstaafu, Makamu wa Rais Mstaafu na Waziri Mkuu Mstaafu nadhani pia kwa upande wa mahakama viongozi wa muhimili huo wana stahili wanazopata wakistaafu. Stahili hizo ni pamoja na kupewa makazi, usafiri, wasaidizi, n.k.
Alichofanya mheshimiwa kiko ndani matakwa hayo, badala ya kumpa VX/V8 ambalo kwa mtazamo wa mheshimiwa linampa usumbufu wa safari kampa hiyo Ben. labda kama hoja itakuwa ulinganifu wa gharama za kununua Benz na VX/V8 hilo nitawaachia wengine wachangie.
 
Inaelekea wewe hukusikia alichosema mama au unataka tu kupotosha kwa makusudi.

Alisema hivi,.... anampa zawadi ya birthday gari ndogo (MB) kwakua lile jingine (V8) walilomnunulia liko juu sana na mzee hua anapata shida kulitumia.....
Nimemjibu mtu kwa muktadha fulani, kwa habari nilizokuwa nazo. Kwa kuanza na ku cover the basic.

Sikusikia alichosema rais verbatim kwa sababu niko mbali.

Nipotoshe kwa makusudi kwa sababu gani wakati hao viongozi wote nishawananga na sina tabia ya hagiography?

Huyo Mwinyi wamempa la chini kwa sababu la juu haliwezi, hilo la juu wamelichukua lifanye kazi nyingine au ndiyo kiendacho kwa mganga hakirudi ?
 
Marais, Makamu Rais na Mawaziri wakuu wastaafu wanachagua magari mapya kila baada ya miaka mitano If I am not mistaken na service wanafanyiwa bure. Na nyumba wanapewa, mpaka mpishi na mtunza bustani wanapewa.

Ni sehemu ya package kustaafu ya viongozi wa kitaifa wastaafu.

Sasa hapa wamefanya kutangaza tu, lakini hawa viongozi wastaafu wote wanachagua magari na wananunuliwa na serikali tangu wanastaafu.
Sasa kama kuna fursa hiyo hii Zawadi ilikuwa na umuhimu/ulazima gani?.
 
Kwahiyo unalinganisha Tausi na 450m?na akili yako ikaishia hapo?bado tunasafati ndefu Sana hapa Tz,sijui nani katuloga,
Mwanae ni Rais wa Zanzibar na kabla alikuwa waziri kwa miaka kibao huku Bara, kwamba hakuona baba anashindwa kupanda V8? Lakini mzee analipwa robo tatu ya mshahara wake kila mwezi Kama akiona shida kupakia V8 kwanini asinunue Gari?
Acha roho ya kichawi mf
 
Kwa maoni yangu zawadi sio jambo la msingi sana kujadiliwa, tunapoteza malengo na makusudio.

nadhani hata yeye mwenyewe Mzee wetu Babu yetu wa Taifa Mzee Ruksa atafarijika zaidi akiona tunajikita kujadili MAUDHUI ya kitabu chake alicho kiandika badala ya kujadili ZAWADI aliyo pewa.
 
Sioni umuhimu wa kutolea zawadi maelezo.

Lakini upo uwezekano pia kuwa hizo shuruba anazopata mzee Mwinyi wakati wa wa kupanda na kushuka kwenye hiyo V 8 ni zoezi mujarabu kwake katika umri mkubwa aliojaliwa ingawa kwa hili mama anaweza kuwa amepata ushauri kwa physiotherapist wa mzee.

Ni matumaini yangu kuwa mzee Mwinyi ambaye anaheshimika sana na watanzania wengi, na Rais Samia, ambaye anabeba matumaini makubwa ya watanzania hawatasongwa sana na mawazo juu ya huu mjadala ulioibuka sababu ya hii birthday gift.

Kwamba mama Samia ataliangalia hili katika mwanga chanya na kurekebisha pale panapostahili bila jazba ambayo inategemewa na baadhi ambao hawakutaka aiongoze Tanzania.
 
Hata ukishindwa kuzalisha utasema ccm
images (43).jpeg
CCM imekua ikijinasibu kuwa ni chama imara kilichobaki barani Africa na kimeshika dola yapata miongo 4 sasa!

CCM hiyo hiyo imeletea umasikini wananchi kwa kiwango kikubwa kutokana na sera mbovu mbovu!

Kuthibitisha hilo pigia gharama za ile misafara ya viongozi na magari yao yanayosindikiza utajua! Halafu ni nchi hiyo hiyo gari yenye kiyoyozi mwanana ni bora kuliko Dawa kuwepo hospitali wananchi nao wamekua blinded na fulana na kofia kuelekea uchaguzi huku wakiitwa "wanyonge"

Mwisho niseme tu ingekua bora kama hakukua na nyongeza ya mshahara kutokana na uchumi kudorora iwe kwa vitendo! Benz moja ingetosha kujenga madara mengi tu na yenye vifaa mazingira rafiki kwa hao watoto wa "wanyonge" maana "watetezi wa wanyonge" watoto wao utasikia anasoma London,Stockholm,Berlin , Ottawa, Newyork,Beijing, Wakishindwa sana utawapata Johannesburg ,Capetown au Pretoria....

images (43).jpeg
 
Sioni umuhimu wa kutolea zawadi maelezo.

Lakini upo uwezekano pia kuwa hizo shuruba anazopata mzee Mwinyi wakati wa wa kupanda na kushuka kwenye hiyo V 8 zoezi mujarabu kwake katika umri mkubwa aliojaliwa ingawa kwa hili mama anaweza kuwa amepata ushauri kwa physiotherapist wa mzee.

Ni matumaini yangu kuwa mzee Mwinyi ambaye anaheshimika sana na watanzania wengi, na Rais Samia, ambaye anabeba matumaini makubwa ya watanzania hawatasongwa sana na mawazo juu ya huu mjadala ulioibuka sababu ya hii birthday gift.

Kwamba mama Samia ataliangalia hili katika mwanga chanya na kurekebisha pale panapostahili bila jazba ambayo inategemewa na baadhi ambao hawakutaka aiongoze Tanzania.
Mwinyi kama anapata tabu, je yeye hawezi kununua kwa pesa yake?
 
Huyi mzee ana pensheni kubwa, mroto wake keshampatia urais Zanzibar wanae wengine kawapa ubunge wa east afrika kwa kifupi huyu mama ni bomu linalosubiri mida kulipuka
Halafu anatoa sababu za kipuuzi tu! Eti amempa gari dogo kwa sababu anapata tabu kupanda kwenye V8! Na baadae akishindwa kupanda hata hiyo Benz aliyo mnunulia itakuwaje?

Atamtafutia mtumwa wa kumbeba? Mama anazingua. Mtu ana familia yake, yeye anaona ni vyema kuchezea hela za Watanganyika kwa ajili tu ya birthday ya Rais Mstaafu! Yaani kasababisha mpaka mechi ya watani kuahirishwa!!

Kazi kweli kweli!!
 
Mwinyi kama anapata tabu, je yeye hawezi kununua kwa pesa yake?

Mkuu nadhani sio tabu, ni sehemu ya mazoezi yanayomwezesha kuwa fit kwenye huo umri alio nao.

A blessing in disguise so as to speak.

Kwa kweli siwezi jua kama anaweza nunua hiyo gari kwa pesa yake au la, lakini hata hivyo yeye ni mpewa zawadi tu na hivyo sio defendant kwenye hii issue.

Kama kuna mtu wa kulaumiwa hapa ni mama, kwa kujaribu ku rationalize zawadi na hivyo kuwapa wale ambao washatoa visu vyao kwenye ala na kuvinoa dhidi yake, nafasi ya kuli- blow hili suala zima out of proportions kiasi cha hata kuwateka wengine ambao walishaonesha imani kwake.
 
Mwinyi kama anapata tabu, je yeye hawezi kununua kwa pesa yake?
Nchi ina maajabu sana hii! Makosa ya 2015 bado yanaendelea tu kututesa kama Taifa! Mama ana miezi miwili tu, lakini ameshaanza kulewa madaraka kwa kasi ya ajabu! Sijui mpaka ifike 2025, itakuwaje!!
 
Mkuu nadhani ni sehemu ya mazoezi yanayomwezesha kuwa fit kwenye huo umri alio nao.

A blessing in disguise so as to speak.

Kwa kweli siwezi jua kama anaweza nunua hiyo gari kwa pesa yake au la, lakini hata hivyo yeye ni mpewa zawadi tu na hivyo sio defendant kwenye hii issue.

Kama kuna mtu wa kulaumiwa hapa ni mama, kwa kujaribu ku rationalize zawadi na hivyo kuwapa wale ambao washatoa visu vyao kwenye ala na kuvinoa dhidi yake, nafasi ya kuli- blow hili suala zima out of proportions kiasi cha hata kuwateka wengine ambao walishaonesha imani kwake.
Ndiyo maana tuna mlaumu sn huyu mama kwa matumizi mabaya ya fedha za umma
 
Ndiyo maana tuna mlaumu sn huyu mama kwa matumizi mabaya ya fedha za umma

Nakubali mkuu.

Viongozi wetu, hasa Rais wanapaswa kuwa sensitive sana kwenye masuala yote yanayohusu fedha za umma.

Lakini kuna wengine pia ambao wanalitumia tu hili tukio la zawadi kama kisingizio cha kumnanga mama yetu bila kuwa na hata chembe ya dhamira njema juu ya matumizi ya fedha za umma.

Najua kuwa wewe si mmoja wa hao.
 
Nakubali mkuu.

Viongozi wetu, hasa Rais wanapaswa kuwa sensitive sana kwenye masuala yote yanayohusu fedha za umma.

Lakini kuna wengine pia ambao wanalitumia tu hili tukio la zawadi kama kisingizio cha kumnanga mama yetu bila kuwa na hata chembe ya dhamira njema juu ya matumizi ya fedha za umma.

Najua kuwa wewe si mmoja wa hao.
Hakika umenena vyema mkuu, Rais akifanya vizuri tumpongeze japo ni wajibu wake na akikosea tumkosoe.
 
Back
Top Bottom