Rais Samia Ondoa hiki kikokotoo kinawaumiza wastaafu

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,505
51,111
Mheshimiwa Rais.

Nakuandikia waraka maalum juu ya hali ya mfanyakazi, hususan anayestaafu.

Nataka nikueleze kuwa, hiki kikotowo ulichokiweka hakina masilahi kwa mfanyakazi anayestaafu. Kiufupi ni dhuluma ya wazi.

Hali ya maisha imekuwa ngumu, gharama za maisha zinazidi kupanda. Kiufupi , hii 33% lumpsum unayotoa kupitia kikotowo, haitoshi, haikidhi, na ni dhulma kubwa mno kwa mfanyakazi.

Ndugu Rais, Jasho la mtu halipaswi kupangiwa masharti magumu. Haiwezekani Mfanyakazi afanye kazi miaka 30 au 35 kisha aje akutane na vijisent vya milioni 50 kama mafao ya kustaafu. Hivi ni vihela vidogo sana na siku hizi havitoshi hata kununua kiwanja na hapohapo kujenga nyumba ya vyumba vitatu.

Ndugu Rais, Hicho chama unachokiongoza kina alama ya jembe na nyundo. Nyundo ikiwakilisha wafanyakazi. Haiwezekani serikali unayoiongoza ikawa ni ya kuwagandamiza wafanyakazi.

Juzi hapa mbunge Heche kaeleza jinsi Wabunge wanavyopata lumpsum ya milioni 272 kwa kazi ya miaka Mitano. Wewe Rais hukatwi kodi katika mshahara wako na Ukistaafu unaendelea kupata 80% ya mshahara wa rais aliyeko madarakani na bado unaenda kupata mabenefit kibao ikiwemo kujengewa nyumba na Pensheni.

Rais hebu Muogope Mungu. Wafikirie watu wa chini. Kikokowa cha 33% ni dhulma kubwa, iondoe mara moja.

Wako katika ujenzi wa Taifa

Missile of the Nation
 
Tatizo ni TUCTA

Kumbukeni kilitaka anza mapema kabla ya hapa ila Magufuli akasogeza muda hadi 2023.

Nawaonea huruma wataostaafu muda huu, mfano Mstaafu alikuwa akipata Milioni 70+ ila kwa sasa atapata chini ya hapo.
 
Tatizo ni TUCTA

Kumbukeni kilitaka anza mapema kabla ya hapa ila Magufuli akasogeza muda hadi 2023.

Nawaonea huruma wataostaafu muda huu, mfano Mstaafu alikuwa akipata Milioni 70+ ila kwa sasa atapata chini ya hapo.
Magufuli angetusaidia sana kipindi kile kama hiyo sheria ya Kikotowo angeachana nayo mazima badala ya kuiahirisha ili kuacha upepo kwanza.

Samia naye badala ya kurekebisha kosa naye kaongeza viasilimia vichache ambavyo bado havitoshi
 
Kikotoo hakina faida yoyote kwa mfanyakazi aliyekatwa pesa zikatumika na mifuko jamii kufanyia biashara lakini lakini yeye anaambulia 1% riba kila mwisho wa mwaka kwa kiasi alichokiweka na inafanyiwa kazi riba hiyo kwa si zaidi ya miaka 10 ya utumishi hata kama kafanya zaidi ya hiyo.

Kikokotoo kiondolewe na mfanyakazi anapoacha kazi yake apewe pesa zake zote ili afanyie biashara au mradi atakaouanzisha mwenyewe sio kupangiwa haki yake namna atakavyoitumia.
 
Wafanyakazi wenyewe hawajitambui acha waendelee kupigwa, haiwezekani watu zaidi ya laki 6 manazidiwa akili na kikundi cha watu wasiozidi elfu 1, wafanyakazi wa umma wajitambue kwanza
Adhabu ya kutojitambua ni kuibiwa jasho lao kisheria (Kandamizi) baada ya Serikali kukopa/kuchota kinyemela fedha za wastaafu wetu na kujengea miradi isiyokuwa na tija bali sifa kwa wanasiasa?

Miradi kama UDOM, Dege Eco Project au daraja la Kigamboni imejengwa kwa fedha za mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Je, hii mifuko ni Benki na inaruhusiwa kukopesha?Madeni ya Serikali yameshalipwa kwa mifuko husika?
 
Ninachojua.
Take home imeshushwa ili kuongeza pensheni ya kila mwezi.
Zamani take home ilikuwa kubwa halafu pensheni ya kila mwezi ilikuwa ndogo sana.
Kitu kilicho waumiza baadhi ya wafanyakazi ambao humaliza take home yao haraka na kuteseka muda mrefu.
Wengine wanaibiwa au kuisha kwenye ujenzi na kujikuta wanashindwa kukabiliana na maisha.

Sasa hivi take home imeshushwa lakini pensheni ya kila mwezi imeongezwa kwa kiasi kikubwa sana ambacho mstaafu anaweza kukidhi mahitaji yake vizuri baada ya kustaafu kazi.

Labda ningeshauri mfanyakazi apewe uhuru wa kuchagua.
Achukue take home kubwa na alipwe pensheni kidogo au kinyume chake.
 
Ninachojua.
Take home imeshushwa ili kuongeza pensheni ya kila mwezi.
Zamani take home ilikuwa kubwa halafu pensheni ya kila mwezi ilikuwa ndogo sana.
Kitu kilicho waumiza baadhi ya wafanyakazi ambao humaliza take home yao haraka na kuteseka muda mrefu.
Wengine wanaibiwa au kuisha kwenye ujenzi na kujikuta wanashindwa kukabiliana na maisha.

Sasa hivi take home imeshushwa lakini pensheni ya kila mwezi imeongezwa kwa kiasi kikubwa sana ambacho mstaafu anaweza kukidhi mahitaji yake vizuri baada ya kustaafu kazi.

Labda ningeshauri mfanyalazi apewe uhuru wa kuchagua.
Achukue take home kubwa na alipwe pensheni kidogo au kinyume chake.
Mtu mzima hutakiwi kumpangia matumizi ya pesa yake.

Wewe mpe pesa yake, atajijua mbele kwa mbele
 
Mtu mzima hutakiwi kumpangia matumizi ya pesa yake.

Wewe mpe pesa yake, atajijua mbele kwa mbele
Kuanza kupangia watu wazima namna ya kutumia pesa ni kujipa kazi nyingine, kwa nini wabunge nao wasipangiwe namna ya kutumia ile milioni 272, wawe wanawapa kidogo kidogo.......watu walipwe stahili zao matumizi mara zote ni swala binafsi.​
 
Kikotoo hakina faida yoyote kwa mfanyakazi aliyekatwa pesa zikatumika na mifuko jamii kufanyia biashara lakini lakini yeye anaambulia 1% riba kila mwisho wa mwaka kwa kiasi alichokiweka na inafanyiwa kazi riba hiyo kwa si zaidi ya miaka 10 ya utumishi hata kama kafanya zaidi ya hiyo.

Kikokotoo kiondolewe na mfanyakazi anapoacha kazi yake apewe pesa zake zote ili afanyie biashara au mradi atakaouanzisha mwenyewe sio kupangiwa haki yake namna atakavyoitumia.
Unadhani watu wote wanaweza kufanya biashara?hivi watu wangapi wanapoteza mafao yao sasa assume wapewe asilimia 100 halafu wapoteze ni bora hata kuwapa 50%, 50% itoke kama pensheni.
 
Mheshimiwa Rais.

Nakuandikia waraka maalum juu ya hali ya mfanyakazi, hususan anayestaafu.

Nataka nikueleze kuwa, hiki kikotowo ulichokiweka hakina masilahi kwa mfanyakazi anayestaafu. Kiufupi ni dhuluma ya wazi.

Hali ya maisha imekuwa ngumu, gharama za maisha zinazidi kupanda. Kiufupi , hii 33% lumpsum unayotoa kupitia kikotowo, haitoshi, haikidhi, na ni dhulma kubwa mno kwa mfanyakazi.

Ndugu Rais, Jasho la mtu halipaswi kupangiwa masharti magumu. Haiwezekani Mfanyakazi afanye kazi miaka 30 au 35 kisha aje akutane na vijisent vya milioni 50 kama mafao ya kustaafu. Hivi ni vihela vidogo sana na siku hizi havitoshi hata kununua kiwanja na hapohapo kujenga nyumba ya vyumba vitatu.

Ndugu Rais, Hicho chama unachokiongoza kina alama ya jembe na nyundo. Nyundo ikiwakilisha wafanyakazi. Haiwezekani serikali unayoiongoza ikawa ni ya kuwagandamiza wafanyakazi.

Juzi hapa mbunge Heche kaeleza jinsi Wabunge wanavyopata lumpsum ya milioni 272 kwa kazi ya miaka Mitano. Wewe Rais hukatwi kodi katika mshahara wako na Ukistaafu unaendelea kupata 80% ya mshahara wa rais aliyeko madarakani na bado unaenda kupata mabenefit kibao ikiwemo kujengewa nyumba na Pensheni.

Rais hebu Muogope Mungu. Wafikirie watu wa chini. Kikokowa cha 33% ni dhulma kubwa, iondoe mara moja.

Wako katika ujenzi wa Taifa

Missile of the Nation
HEBU WATUMISHI KUWENI NA SHUKURANI MAGUFULI ALITAKA MLIPWE 28% lakini MAMA SAMIA ANALIPA 33% shukuruni kwa hiyo NYONGEZA
 
Back
Top Bottom