Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Wanajamvi, Jana Kuna taarifa zilisambaa sana za kumtaka Rais Samia kutumia birthday yake Kumsaidia kada wa chama chake Thadei Ole Mushi aliyesimama moyo kufanya kazi.
Taarifa hizi zilisambazwa na kada wao Bollen Ngetti Mwandishi nguli za Uchunguzi hapa nchini. Hata humu taarifa hizo zilifika.
Mwandishi Ngetti ametoa taarifa tena huko kwenye magrupu akimshikuru Rais Samia kusikia kilio na wito huo. Amesema Samia tayari ametoa ndege maalumu (aircraft ambulance) itakayomsafiruaha Ole Mushi Hadi Nairobi kwa matibabu pamoja na gharama zote. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Samia ametumia vizuri birthday yake.
Nimpongeze pia Bollen Ngetti kwa kupaza sauti kubwa kwa matibabu ya Thadei Ole Mushi. Sasa tumuombee apone.
Taarifa hizi zilisambazwa na kada wao Bollen Ngetti Mwandishi nguli za Uchunguzi hapa nchini. Hata humu taarifa hizo zilifika.
Mwandishi Ngetti ametoa taarifa tena huko kwenye magrupu akimshikuru Rais Samia kusikia kilio na wito huo. Amesema Samia tayari ametoa ndege maalumu (aircraft ambulance) itakayomsafiruaha Ole Mushi Hadi Nairobi kwa matibabu pamoja na gharama zote. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Samia ametumia vizuri birthday yake.
Nimpongeze pia Bollen Ngetti kwa kupaza sauti kubwa kwa matibabu ya Thadei Ole Mushi. Sasa tumuombee apone.