Rais Samia na Waziri Mkuu wanunua tiketi 4000 mchezo wa Tanzania vs Uganda

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,035
1679639542861.png

Picha: Rais Samia Suluhu Hassan

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa wamenunua jumla ya tiketi 4,000 za mechi ya kufuzu AFCON 2023 kati ya Tanzania na Uganda.

Tiketi hizo zitagawiwa kwa mashabiki ili waende kushuhudia mechi hiyo itakayochezwa uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam Machi 28 mwaka huu.

===
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hasaan na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa wamenunua tiketi 4,000 kwa ajili ya mashabiki kwenda uwanjani kuishangilia Taifa Stars itakapokuwa inacheza dhidi ya Uganda.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kupitia simu ya Meneja wa Habari wa Simba Ahmed Ally alitoa taarifa ya kununua tiketi hizo wakati wa kampeni ya kununua tiketi ili kuhamasisha mashabiki kwenda uwanjani kuishangilia timu ya Taifa.

Jumanne Machi 28,2023 Taifa Stars itacheza mechi ya marudiano dhidi ya Uganda kuwania kufuzu Fainali za AFCON 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.
 
Rais wa Tanzania DktSamia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa wamenunua jumla ya tiketi 4,000 za mechi ya kufuzu AFCON 2023 kati ya Tanzania na Uganda.
Tiketi hizo zitagawiwa kwa mashabiki ili waende kushuhudia mechi hiyo itakayochezwa uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam Machi 28 mwaka huu.
Hivi "WASHAMBULIAJI" wa ki Tanzania ni akina nani hasa ?!.

Maake naona team zinazocheza vizuri sasa, washambuliaji ni wageni watupu !!
 
Mechi ya marudiano tungeomba ichezewe huko huko Misri tu. Uwanja wenyewe kwanza unahitaji ukarabati mkubwa halafu kila leo mnautumia, huo ukarabati utafanyika saa ngapi?
 
Mechi ya marudiano tungeomba ichezewe huko huko Misri tu. Uwanja wenyewe kwanza unahitaji ukarabati mkubwa halafu kila leo mnautumia, huo ukarabati utafanyika saa ngapi?
Lakini Simba na Yanga walicheza pale, alafu kwanini Uganda wanachezea Misri?
 
Kina Samatta, kina Msuva na wengineo kama kina Kibu na Bocco
Labda !!

Sionipo mtu hapo wa kutuvusha. Simba & Yanga wanafanya vizuri sasa baada ya kugundua kuwa Petre Tino, Gibson Sembuli, Zamoyoni Mogella etc. hawakuwazalisha wanawake wengi Tanzania hii.
 
Lakini Simba na Yanga walicheza pale, alafu kwanini Uganda wanachezea Misri?
Simba na Yanga ina make sense kwa sababu kwanza wanaujaza uwanja, pili hawawezi wote kukubaliana kuacha kuutumia wakati anayeenda kufaidika ni mmoja. Ni kwenye mashindano ya Azam tu ndiyo naona busara imetumika wakakubaliana.

Hii timu ya taifa haitapata advantage yoyote ya kucheza nyumbani. Huo ndiyo ukweli. Simba na Yanga zinacheza ugenini bila mashabiki wao na zinapata matokeo.

Uganda hawana uwanja kwa sasa uliokidhi vigezo vya CAF.
 
Back
Top Bottom