Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa shilingi bilioni 1 kwa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu Tanzania (Taifa Stars) endapo itafanikiwa kutwaa ubingwa wa CHAN 2024 na kubeba kombe.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Palamagamba Kabudi, amesema hayo leo July 24,2025 wakati akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa ufunguzi wa fainali za CHAN 2024 Tanzania vs Burkina Faso utakaochezwa Auguts 2, 2025 uwanja wa Benjamin Mkapa.
"Katika kuchagiza hamasa kwa Timu yetu ya Tanzania, Rais Samia ametoa ahadi ya donge nono la fedha Tsh. bilioni, sio milioni ni bilioni yaani mabii, bilioni 1 kwa Vijana wetu wa Taifa Stars, iwapo watafanikiwa kutwa ubingwa wa mashindano haya ya CHAN 2024, Mcheza kwao hutunzwa na yeye ameamua kuwatunza"
Chanzo: Millard Ayo
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Palamagamba Kabudi, amesema hayo leo July 24,2025 wakati akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa ufunguzi wa fainali za CHAN 2024 Tanzania vs Burkina Faso utakaochezwa Auguts 2, 2025 uwanja wa Benjamin Mkapa.
"Katika kuchagiza hamasa kwa Timu yetu ya Tanzania, Rais Samia ametoa ahadi ya donge nono la fedha Tsh. bilioni, sio milioni ni bilioni yaani mabii, bilioni 1 kwa Vijana wetu wa Taifa Stars, iwapo watafanikiwa kutwa ubingwa wa mashindano haya ya CHAN 2024, Mcheza kwao hutunzwa na yeye ameamua kuwatunza"
Chanzo: Millard Ayo