Rais Samia hakuna kurudi nyuma. Simamia hapo hapo, Hii nchi ukiwasikiliza watu haitaenda

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Kwanza kabisa nakupongeza kwa ukipofikia. 1. Kwenye chanjo
2. Kwenye Makato ya Kodi

Tanzania ilipokuwa imefikia ilikuwa ni pabaya sana. Watu waliaminishwa ujinga na wakaendelea kuishi kwenye ujinga. Tumepoteza watu wengi sana kutokana na kuaminishwa kuwa Tiba asili inatibu Corona badala ya njia za kisayansi. Mimi Pia nilipoteza rafiki yangu.

1. Kwenye Chanjo
Hapa usibadili msimamo. Aliyepita alidharau huu ugonjwa na kwa Kweli hata yeye mwenyewe ulimwondoa. Umeondoa wasaidizi wake na wananchi wengi Pia. Ni bora umeruhusu chanjo. Watu wachomwe wanaotaka na wasiotaka waachwe corona ideal nao. Mfano wa nchi zilizochukulia serious huu ugonjwa upo na sasa wameweza kuudhibiti na sasa wamerejea kwenye maisha yao na kuepusha vifo na kupoteza nguvu kazi

2. Kwenye Tozo
Hapa wala usirudi nyuma. Aliyepita hakupandisha wafanyakazi madaraja, hakuongeza mishahara. Wewe umepandisha wafanyakazi madaraja jambo lililosababisha mishahara yao kuongezeka. Aliyepita alikusanya kodi kwa nguvu na kukopa sana Hadi akawazidi maraisi wote kwa kukopa. Wewe hutaki kodi ya dhuruma na Pia unataka kupunguza kukopa sana.
Wewe unataka kufanya miradi kwa pesa za ndani kweli na sio kuwahadaa wananchi unafanya miradi kwa pesa za ndani kumbe unakopa sana na kuhatarisha uchumi kwa kuongeza deni la taifa.

Tunahitaji miradi ya kimkakati. Maji yawepo kwa wananchi wote, barabara za lami vijijini na mijini na Pia miradi mikubwa iliyoanza kukamilika.

Kwa malengo haya Mama Samia usirudi Nyuma. Zaidi naomba tu haya pia yafanyike

1. Wabunge nao waanze kutozwa kodi

2. Wale wote wasiotozwa kodi( Hasa kwenye utumishi) nao waanze kutozwa kodi.

Mama Samia, China unayoiona Leo ni kutokana na maamuzi magumu kwenye maendeleo yaliyofanywa na Mao Zedong na Deng Xiaoping.

Ulaya unayoiona Leo kuna kodi kwenye kila kitu na wananchi wanalipa Kweli.

Rais Samia namaliza kwa kukwambia, usife moyo wala usirudi nyuma. Hayo ndo maamuzi magumu.
 
Naungana na wewe ,kucheka Cheka na wapiga Domo hakuna kitu kitaenda na hii nchi ina watu wamejaaliwa mdomo Sana.

Tozo zibaki pale pale na napendekeza vyanzo vingine kama leseni za mafundi ujenzi wote,kuwe na register/ data base ya wamiliki wa nyumba,viwanja na mashamba na kuongeza udhibiti wa kuhakikisha watu wanadai risiti,hapa polisi na TRA wawe wakali kwa wanao nunua bidhaa bila risiti
 
Naungana na wewe ,kucheka Cheka na wapiga Domo hakuna kitu kitaenda na hii nchi ina watu wamejaaliwa mdomo Sana.

Tozo zibaki pale pale na napendekeza vyanzo vingine kama leseni za mafundi ujenzi wote,kuwe na register/ data base ya wamiliki wa nyumba,viwanja na mashamba na kuongeza udhibiti wa kuhakikisha watu wanadai risiti,hapa polisi na TRA wawe wakali kwa wanao nunua bidhaa bila risiti
Kweli kabisa. Tukicheka na ndani hatutafika popote. Nchi lazima ipate maendeleo kwa njia hizi hizi ambazo ndo nzuri
 
Kwenye kongole zako na nasaha ongeza na bunge litunge sheria, wale wote wanaokula "pesa" za umma wapigwe risasi hadharani. Maana tutachangia kwenye miamala, mwakani CAG atatuambia billion 500 hazijulikani zilipo.
 
My friend nakuchalenji hapo kwenye point No. 2 "Corona itadeal nao" sijui kama umefikiri mara mbili. This issue is very complex so mind your thought.
 
Hatupingi kulipa kodi, tunapinga kutozwa kodi mara tatu ya mwanzo.

Pia tunashangazwa na kauli zao eti Tanzania ni Tajiri wakati kila kukicha ni kubinya kidogo cha wanyonge
 
JamiiForums-1551552128.jpg
JamiiForums-1778541516.jpg
 
Hatupingi kulipa kodi, tunapinga kutozwa kodi mara tatu ya mwanzo.

Pia tunashangazwa na kauli zao eti Tanzania ni Tajiri wakati kila kukicha ni kubinya kidogo cha wanyonge
Lazima tuchangie kwa ujenzi imara wa Taifa letu. Masikini na tajiri, lazima wote tuchangie.
 
Kwenye kongole zako na nasaha ongeza na bunge litunge sheria, wale wote wanaokula "pesa" za umma wapigwe risasi hadharani. Maana tutachangia kwenye miamala, mwakani CAG atatuambia billion 500 hazijulikani zilipo.
Hahahahaha! Naunga mkono hoja
 
My friend nakuchalenji hapo kwenye point No. 2 "Corona itadeal nao" sijui kama umefikiri mara mbili. This issue is very complex so mind your thought.
Hapana! Watanzania wana ujuaji mwingi sana, alafu wanajifanya wanamjua sana Mzungu kuliko hata hao waliowaletea hizo dini.

Kupenda kwao ujinga kunawafanya waamini sana ujinga. Sasa acha wanaotaka chanjo wachome wasiotaka wamfuate yule jamaa yao aliyeleta kiburi hadi ikamuondoa
 
Tatizo sio Kodi ila ni matumizi mengi ya serikali hataendi kwenye maendeleo Kama wwanavyotuambia
Hao China unaowaona unajua ratio kati ya tajiri na masikini. Gap kati ya tajiri na masikini unajua wewe
 
Hoja ya mama ya kutegeneza barabara vijijini haina mashiko kama soko la hayo mazao halipo hizo barabara ndo zitakuwa soko? kama nia ni kuwasaidia wakulima wenyewe wanataka pembejeo na soko imara la mazao yao kuliko kuwaachia madalali wacontrol soko la mazao, cjui wakivuna mazao wanaenda kuyamwaga barabarani!, ila CCM ni tatizo katika nchi hi.
 
La Corona umechemka nchi gani imetokomeza Corona kwa approach unayo mshauri?
Sana Sana wameamua kuishi na Corona Kama alivyotuasa Mwendazake,tuishi nayo Kama magonjwa mengine.
 
MH.RAIS SSH SIMAMIA HAPOHAPO

HII NCHI UKIWASIKILIZA "SANA" WATU HAITOENDA

#KaziIendelee
#JMTMilele
 
Kwanza kabisa nakupongeza kwa ukipofikia. 1. Kwenye chanjo
2. Kwenye Makato ya Kodi

Tanzania ilipokuwa imefikia ilikuwa ni pabaya sana. Watu waliaminishwa ujinga na wakaendelea kuishi kwenye ujinga. Tumepoteza watu wengi sana kutokana na kuaminishwa kuwa Tiba asili inatibu Corona badala ya njia za kisayansi. Mimi Pia nilipoteza rafiki yangu...
Kuna anayepinga makato basi, tunapinga makato yako juu sana, yanafanya maisha yawe magumu!

Kulazimisha watu walipe anaweza kulazimisha ila atapata kidogo maana uwezo wa watu kumudu makato hayo si mzuri

Hata zamani tulikuwa tunakatwa, inamaana walishindwa kujenga shule kwa makato yale?, kama walishindwa fedha walizipeleka wapi?
 
Hoja ya mama ya kutegeneza barabara vijijini haina mashiko kama soko la hayo mazao halipo hizo barabara ndo zitakuwa soko? kama nia ni kuwasaidia wakulima wenyewe wanataka pembejeo na soko imara la mazao yao kuliko kuwaachia madalali wacontrol soko la mazao, cjui wakivuna mazao wanaenda kuyamwaga barabarani!, ila CCM ni tatizo katika nchi hi.
Umefika kwenye vijiji vingapi vya Tanzania?? Umeona adha ya barabara wanayopata wananchi tena wanaozalisha chakula kwa wingi??
 
Kuna anayepinga makato basi, tunapinga makato yako juu sana, yanafanya maisha yawe magumu!

Kulazimisha watu walipe anaweza kulazimisha ila atapata kidogo maana uwezo wa watu kumudu makato hayo si mzuri

Hata zamani tulikuwa tunakatwa, inamaana walishindwa kujenga shule kwa makato yale?, kama walishindwa fedha walizipeleka wapi?
Kwenye miamala wanayofanya wananchi wengi wa kawaida makato ni ya kawaida tu. miamala mikubwa ndo makato ni makubwa
 
La Corona umechemka nchi gani imetokomeza Corona kwa approach unayo mshauri?
Sana Sana wameamua kuishi na Corona Kama alivyotuasa Mwendazake,tuishi nayo Kama magonjwa mengine.
Hujui China wamefanikiwa kuicontrol baada ya kuchanja watu wengi??

hujui Taiwan, Singapore, Israel nao wamefanikiwa baada ya kuchanja watu wao wengi sana??? Sasa hivi wana cases chache sana ambazo zote zinahimilika!
 
Back
Top Bottom