Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania,mama wa shoka,chuma cha reli, jasiri muongoza njia,shujaa wa Afrika,simba wa nyika amewasili salama nchini saudi Arabia ambako atashiriki mkutano unaozikutanisha nchi za Afrika na Saudi Arabia utakao fanyika November 10 mjini Riyadh,unaoangazia kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano katika sekta za biashara,kilimo,utalii,nishati,uwekezaji na madini.
Ikumbukwe na kueleweka ya kuwa mikutano ya aina hii ni muhimu kwa kuwa inawakutanisha wafanyabishara na wawekezaji wakubwa sana katika Secta hizo tajwa,ambapo ni fursa nzuri kwetu kama Taifa kupata wawekezaji wenye tija na manufaa kwa maslahi mapana ya Taifa letu na ustawi wa watanzania.
Ikumbukwe kuwa fursa zinatafutwa na kila mtu ,hivyo ukikaa tu pasipo kuzitafuta na kuzivutia nchini mwako usifikiri zitakuja tu zenyewe kana kwamba Tanzania tupo pekee yetu au tunavitu vya kipekee ambavyo havipo kwingineko. Ni kupitia fursa hizo ambapo tutatengeneza fursa za ajira kwa vijana, maendeleo ya viwanda,kilimo,utalii, uchumi,kuongeza mapato na kupanua wigo wa kodi.
Hakuna nchi isiyotaka au kuhitaji wawekezaji wakubwa.kila nchi inahitaji wawekezaji na ndio maana tuna ona kila nchi ikijaribu kuweka sera na sheria zitakazovutia wawekezaji wengi ,huku ikilinda na kuhakikishia kuwa wawekezaji wanaokuja ni wenye tija ,kwa kusaini mikataba yenye matokeo chanya yenye kuzingatia maslahi ya Taifa na usalama wake,yenye kuzingatia utamaduni wetu na uwekezaji usio pora uhuru wa Taifa letu lakini ambayo haitaliumiza Taifa wala kuleta maumivu kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho .
Kikubwa watanzania tuendelee kuchangamkia fursa ambazo mh Rais anazileta hapa Nchini.lakini pia serikali yetu ihakikishe ya kuwa kila itakapoweka wino wake kusaini mkataba wa aina yoyote ile basi uwe ni mkataba ambao hata vizazi vijavyo baada ya miaka mingi mbele vikija kuusoma vitikise kichwa kwa Tabasamu na kusema kuwa kwa hakika mkataba huu ulisainiwa na wazalendo wa kweli na wenye upendo na Taifa letu na haya ndio matunda yake.
Serikali ihakikishe kwa kila namna wafanyabiashara wetu hapa nchini wanapata nafasi ya kushirikiana na wawekezaji wa nje ili hata siku wageni wakitaka kuondoka basi tusiteteleke na tubakiwe na ujuzi na maarifa ya namna ya uendeshaji.tuzoe fursa zote popote pale Duniani zenye kulifaidisha Taifa na zile zenye kulinyonya Taifa tuziache na kuzipa kisogo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania,mama wa shoka,chuma cha reli, jasiri muongoza njia,shujaa wa Afrika,simba wa nyika amewasili salama nchini saudi Arabia ambako atashiriki mkutano unaozikutanisha nchi za Afrika na Saudi Arabia utakao fanyika November 10 mjini Riyadh,unaoangazia kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano katika sekta za biashara,kilimo,utalii,nishati,uwekezaji na madini.
Ikumbukwe na kueleweka ya kuwa mikutano ya aina hii ni muhimu kwa kuwa inawakutanisha wafanyabishara na wawekezaji wakubwa sana katika Secta hizo tajwa,ambapo ni fursa nzuri kwetu kama Taifa kupata wawekezaji wenye tija na manufaa kwa maslahi mapana ya Taifa letu na ustawi wa watanzania.
Ikumbukwe kuwa fursa zinatafutwa na kila mtu ,hivyo ukikaa tu pasipo kuzitafuta na kuzivutia nchini mwako usifikiri zitakuja tu zenyewe kana kwamba Tanzania tupo pekee yetu au tunavitu vya kipekee ambavyo havipo kwingineko. Ni kupitia fursa hizo ambapo tutatengeneza fursa za ajira kwa vijana, maendeleo ya viwanda,kilimo,utalii, uchumi,kuongeza mapato na kupanua wigo wa kodi.
Hakuna nchi isiyotaka au kuhitaji wawekezaji wakubwa.kila nchi inahitaji wawekezaji na ndio maana tuna ona kila nchi ikijaribu kuweka sera na sheria zitakazovutia wawekezaji wengi ,huku ikilinda na kuhakikishia kuwa wawekezaji wanaokuja ni wenye tija ,kwa kusaini mikataba yenye matokeo chanya yenye kuzingatia maslahi ya Taifa na usalama wake,yenye kuzingatia utamaduni wetu na uwekezaji usio pora uhuru wa Taifa letu lakini ambayo haitaliumiza Taifa wala kuleta maumivu kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho .
Kikubwa watanzania tuendelee kuchangamkia fursa ambazo mh Rais anazileta hapa Nchini.lakini pia serikali yetu ihakikishe ya kuwa kila itakapoweka wino wake kusaini mkataba wa aina yoyote ile basi uwe ni mkataba ambao hata vizazi vijavyo baada ya miaka mingi mbele vikija kuusoma vitikise kichwa kwa Tabasamu na kusema kuwa kwa hakika mkataba huu ulisainiwa na wazalendo wa kweli na wenye upendo na Taifa letu na haya ndio matunda yake.
Serikali ihakikishe kwa kila namna wafanyabiashara wetu hapa nchini wanapata nafasi ya kushirikiana na wawekezaji wa nje ili hata siku wageni wakitaka kuondoka basi tusiteteleke na tubakiwe na ujuzi na maarifa ya namna ya uendeshaji.tuzoe fursa zote popote pale Duniani zenye kulifaidisha Taifa na zile zenye kulinyonya Taifa tuziache na kuzipa kisogo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.