Gulio Tanzania
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 2,154
- 4,520
Mpaka sasa tumeachwa gizani hatujui mustakabali wa nchi yetu swala la mkataba wa bandari upande wa utetezi ukimsikiliza Mheshimiwa waziri mkuu ,waziri wa ujenzi na uchukuzi,na msemaji wa serikali hawa wote nimewasikiliza kauli zao kila mtu kila mtu anasema lake lakini bado hawakati kiu ya Watanzania wengi na ndio mana mkataba huu umeendelea kubaki na maswali mengi bila kupata muafaka.
Kauli ya Waziri Mkuu
"Bandari imepewa DP-World kwa kuwa utendaji wa TICTS ni mdogo
Kauli ya waziri wa ujenzi na uchukuzi
"Mkataba huu utakuwa hai mpaka pale ambapo shughuli za miradi zitasitishwa au kuisha kwa muda wa mikataba ya nchi mwenyeji na mikataba ya miradi
Kauli ya msemaji wa serikali
"hakuna mpango wa kuuza bandari lengo ni kuongeza ufanisi
Kauli ya mwisho tuliyokuwa tunaisubiri ni kutoka kwa mwanasheria mkuu serikali kutokana na ukimya wake tulitegemea aje na hitimisho sataka hili la bandari lakini naye bado katuacha na maswali mengi tulitegemea moja kwa moja aje na majibu vifungu vya mkataba ambavyo vina utata katika mkataba huo.
Anasema hakuna mkataba tulioingia na dubai yale ni makubaliano.
Swali ambalo wengi wanabaki wanahoji sasa bungeni walikuwa wanajadili nini kama hakuna mkataba
Mpaka hapa tulipofika tumtupie mpira Mheshimiwa rais atutoe hofu watanzania najua siku anaapishwa aliapa kwa vitabu vitakatifu ni muda sasa ajitokeze asizibe pamba masikioni atuambie ukweli nini kinaendelea kwenye mkataba huu.
Mpaka lini hii nguvu ya kuendelea kushambulia wanaopinga mkataba itakoma wanaopinga mkataba wanaambiwa wapotoshaji.
Kauli ya Waziri Mkuu
"Bandari imepewa DP-World kwa kuwa utendaji wa TICTS ni mdogo
Kauli ya waziri wa ujenzi na uchukuzi
"Mkataba huu utakuwa hai mpaka pale ambapo shughuli za miradi zitasitishwa au kuisha kwa muda wa mikataba ya nchi mwenyeji na mikataba ya miradi
Kauli ya msemaji wa serikali
"hakuna mpango wa kuuza bandari lengo ni kuongeza ufanisi
Kauli ya mwisho tuliyokuwa tunaisubiri ni kutoka kwa mwanasheria mkuu serikali kutokana na ukimya wake tulitegemea aje na hitimisho sataka hili la bandari lakini naye bado katuacha na maswali mengi tulitegemea moja kwa moja aje na majibu vifungu vya mkataba ambavyo vina utata katika mkataba huo.
Anasema hakuna mkataba tulioingia na dubai yale ni makubaliano.
Swali ambalo wengi wanabaki wanahoji sasa bungeni walikuwa wanajadili nini kama hakuna mkataba
Mpaka hapa tulipofika tumtupie mpira Mheshimiwa rais atutoe hofu watanzania najua siku anaapishwa aliapa kwa vitabu vitakatifu ni muda sasa ajitokeze asizibe pamba masikioni atuambie ukweli nini kinaendelea kwenye mkataba huu.
Mpaka lini hii nguvu ya kuendelea kushambulia wanaopinga mkataba itakoma wanaopinga mkataba wanaambiwa wapotoshaji.