Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,462
- 29,158
Kwema Wakuu?
Kwa sasa MAIN TOPIC au AGENDA nchini ni swala la Bandari. Kuanzia ma ofisini, majumbani, vijiweni, kwenye daladala, bar hizi story zimetapakaa.
Kila mmoja anazungumzia issue za bandari kwa muktadha wake. Wapo wanaoihusisha Bandari na dini, utanganyika v/s uzanzibar, kuibiwa, kuuzwa, u chama, maendeleo etc.
Katika wale wanaopinga huu mkataba, wapo waliokata tamaa kwa maana ya liwalo na liwe, wapo ambao hawajakata tamaa wakijaribu kuelezea huku na kule ikiwamo kuupinga mahakamani, wapo ambao wana matumaini utakuja kubadilishwa baadae.
Ukiacha huku mitaani au mitandaoni tunakojibishana kila Leo, pande zote mbili hazijawahi kukutana pamoja kuulezea au kuelezana why wanaona uko au hauko sawa. Utaona tu viongozi wa Serikali wakiutetea wakiwa wao peke Yao, vivyo hivyo wanaoupinga nao hua peke Yao.
Kwa ukubwa na wingi wa hii mijadala ni wazi kua haitoisha leo wala kesho. Na Serikali Kwa upande mmoja ikiamua kuutekeleza huu mkataba basi upande wa pili utabaki na kinyongo.
Sasa mimi nilikua nina wazo au ushauri. Itafutwe siku moja au mbili, ufanyike mdahalo wa wazi, Serikali v/s Watu kadhaa hivi wanaopinga, labda, kumi kumi kila upande. Mdahalo huu urushwe live kwenye television wananchi tuone au tusikilize kila pande tuuelewe.
Kama hadidu za rejea zitoke kwenye huo mkataba ambao sio Siri tena maana upo mitandaoni. Kijadiliwe kifungu kimoja baada ya kingine. Wanaoona kifungu kina walakini waelezee walikini wao upo wapi na wanaoona kifungu kiko sawa wajibu hoja hizo.
Iwe ni DEBATE ambayo watu watachangia Kwa staha na ustaarabu, sio jazba, vijembe au mihemuko. Isiwe DEBATE kama vile tuko bungeni kwamba wenye kelele nyingi za "ndio" ndo wanakua wameshinda. Bali watu waende point kwa point, neno kwa neno mpaka wafikie muafaka.
Pale upande mmoja utakaposhindwa kwa hoja basi usisite kukubali ili kutopoteza muda waende kwenye kifungu kingine. Mfano wanaoutetea kwamba mkataba unao kikomo wakifanikiwa kuonyesha ukomo ulipo basi wale wanaoupinga wakubali tu.
Debate hii itasaidia hata wale ambao ambao hawaelewi in details bali bendera fuata upepo kuelewa kilichomo humo, kinachopingwa au kutetewa ni kipi. Sababu wako wengine huamua kubisha sababu tu wamemsikia fulani akisema hivi au vile.
Washiriki wa kila upande wapewe taratibu, ratiba na hadidu za rejea za debate hiyo siku kadhaa kabla ili waweze kujiandaa. Isiwe kama ni kesi mahakamani kwamba nani mwenye maswali ya kubana zaidi bali points, data na facts ndio ziongee zaidi.
Tukifanya haya basi tutakua tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuzima hii mijadala ili watu waendelee na mambo yao mengine, wanaopinga waweze kuukubali ikitokea ni mzuri au wanaoutetea waweze kuurekebisha ikitokea una walakini.
Yangu ni hayo tu Kwa Leo.
Kwa sasa MAIN TOPIC au AGENDA nchini ni swala la Bandari. Kuanzia ma ofisini, majumbani, vijiweni, kwenye daladala, bar hizi story zimetapakaa.
Kila mmoja anazungumzia issue za bandari kwa muktadha wake. Wapo wanaoihusisha Bandari na dini, utanganyika v/s uzanzibar, kuibiwa, kuuzwa, u chama, maendeleo etc.
Katika wale wanaopinga huu mkataba, wapo waliokata tamaa kwa maana ya liwalo na liwe, wapo ambao hawajakata tamaa wakijaribu kuelezea huku na kule ikiwamo kuupinga mahakamani, wapo ambao wana matumaini utakuja kubadilishwa baadae.
Ukiacha huku mitaani au mitandaoni tunakojibishana kila Leo, pande zote mbili hazijawahi kukutana pamoja kuulezea au kuelezana why wanaona uko au hauko sawa. Utaona tu viongozi wa Serikali wakiutetea wakiwa wao peke Yao, vivyo hivyo wanaoupinga nao hua peke Yao.
Kwa ukubwa na wingi wa hii mijadala ni wazi kua haitoisha leo wala kesho. Na Serikali Kwa upande mmoja ikiamua kuutekeleza huu mkataba basi upande wa pili utabaki na kinyongo.
Sasa mimi nilikua nina wazo au ushauri. Itafutwe siku moja au mbili, ufanyike mdahalo wa wazi, Serikali v/s Watu kadhaa hivi wanaopinga, labda, kumi kumi kila upande. Mdahalo huu urushwe live kwenye television wananchi tuone au tusikilize kila pande tuuelewe.
Kama hadidu za rejea zitoke kwenye huo mkataba ambao sio Siri tena maana upo mitandaoni. Kijadiliwe kifungu kimoja baada ya kingine. Wanaoona kifungu kina walakini waelezee walikini wao upo wapi na wanaoona kifungu kiko sawa wajibu hoja hizo.
Iwe ni DEBATE ambayo watu watachangia Kwa staha na ustaarabu, sio jazba, vijembe au mihemuko. Isiwe DEBATE kama vile tuko bungeni kwamba wenye kelele nyingi za "ndio" ndo wanakua wameshinda. Bali watu waende point kwa point, neno kwa neno mpaka wafikie muafaka.
Pale upande mmoja utakaposhindwa kwa hoja basi usisite kukubali ili kutopoteza muda waende kwenye kifungu kingine. Mfano wanaoutetea kwamba mkataba unao kikomo wakifanikiwa kuonyesha ukomo ulipo basi wale wanaoupinga wakubali tu.
Debate hii itasaidia hata wale ambao ambao hawaelewi in details bali bendera fuata upepo kuelewa kilichomo humo, kinachopingwa au kutetewa ni kipi. Sababu wako wengine huamua kubisha sababu tu wamemsikia fulani akisema hivi au vile.
Washiriki wa kila upande wapewe taratibu, ratiba na hadidu za rejea za debate hiyo siku kadhaa kabla ili waweze kujiandaa. Isiwe kama ni kesi mahakamani kwamba nani mwenye maswali ya kubana zaidi bali points, data na facts ndio ziongee zaidi.
Tukifanya haya basi tutakua tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuzima hii mijadala ili watu waendelee na mambo yao mengine, wanaopinga waweze kuukubali ikitokea ni mzuri au wanaoutetea waweze kuurekebisha ikitokea una walakini.
Yangu ni hayo tu Kwa Leo.