Rais Samia ashiriki Mkutano wa BRICS Nchini Afrika Kusini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Mkutano wa kilele wa BRICS umeingia siku ya 3 huko Johanesburg, Afrika Kusini. Nchi wanachama zinapania kuimarisha ushawishi kuukabili muundo wa uchumi wa dunia unaoongozwa na nchi za Magharibi.

Viongozi wa muungano wa BRICSwamegeukia ajenda kuu ya mkutano wao, siku moja baada ya Rais wa Urusi Vladimir Putin kuzikosoa nchi za magharibi. Muungano huo unajadili uwezekano wa utanuzi na kuruhusu wanachama wapya wajiunge, ikiwa ni zaidi ya muongo mmoja tangu ulipoasisiwa.

Zaidi ya nchi 20 zimewasilisha rasmi maombi ya kutaka uanachama ikiwemo Saudi Arabia.


1d66b6f5-d10c-41ba-8cf8-bde2cc587a8a.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa China Mhe. Xi Jinping kando ya Mkutano wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 24 Agosti, 2023.

9d527e32-7fba-45e4-82aa-de35c9e039a3.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Wakuu wa nchi na Serikali kwenye Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 24 Agosti, 2023.
 
Huyo Bibi anaangaika sana;Kuna deals walisaini na serikali ya Marekani ata hawajatekeleza karukia BRICS🤣.
Au wamemwambia Kuna mikopo nini maana nchi anaiendesha kama VICOBA!
 
Mkutano wa kilele wa BRICS umeingia siku ya 3 huko Johanesburg, Afrika Kusini. Nchi wanachama zinapania kuimarisha ushawishi kuukabili muundo wa uchumi wa dunia unaoongozwa na nchi za Magharibi.

Viongozi wa muungano wa BRICSwamegeukia ajenda kuu ya mkutano wao, siku moja baada ya Rais wa Urusi Vladimir Putin kuzikosoa nchi za magharibi. Muungano huo unajadili uwezekano wa utanuzi na kuruhusu wanachama wapya wajiunge, ikiwa ni zaidi ya muongo mmoja tangu ulipoasisiwa.

Zaidi ya nchi 20 zimewasilisha rasmi maombi ya kutaka uanachama ikiwemo Saudi Arabia.


View: https://www.youtube.com/watch?v=ADzHqoyX09I

Hii mikutano haitamaliza matatizo yetu ya uchumi, zaidi inatutia umasikini kwa kugharamia posho na nauli za viongozi.
 
Huyo Bibi anaangaika sana;Kuna deals walisaini na serikali ya Marekani ata hawajatekeleza karukia BRICS🤣.
Au wamemwambia Kuna mikopo nini maana nchi anaiendesha kama VICOBA!
Ulitaka ajifungie kama yule wa Jana, wa Zambia Zimbabwe na wengi mno wamealikwa kwenye mkutano huo!
 
Back
Top Bottom