Rais Samia ashiriki Maadhimisho ya Siku ya kupambana na Rushwa Afrika, leo Julai 11, 2023

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akishiriki Maadhimisho ya Siku ya kupambana na Rushwa Afrika, leo Julai 11, 2023 jijini Arusha.



===

IMG_7967.jpeg


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema moja ya vikwazo vikubwa vya maendeleo barani Afrika ni pamoja na janga la rushwa ambalo linadhoofisha mifumo ya kitaasisi na kuathiri mipango na mikakati ya kujikomboa kiuchumi.

Rais Samia amesema hayo leo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi va Rushwa Barani Afrika na maadhimisho va utekelezaji wa miaka 20 ya Mkataba wa Umoja wa Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa yaliyofanyika AICC.

Aidha, Rais Samia amesema viongozi wote barani Afrika hawana budi kuimarisha ushirikiano katika mapambano dhidi ya rushwa.

Vile vile, Rais Samia amewataka viongozi kutafakari na kuchambua kwa dhati masuala ya rushwa ili kubainisha changamoto au vikwazo vya mapambano hayo na kuchukua hatua muafaka.

Kwa upande mwingine, Rais Samia amesema Serikali inaendelea kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kibajeti na kimfumo ikiwemo kuanzisha taasisi zinazosimamia utawala bora na haki za binadamu nchini

Rais Samia pia amesema Serikali imewekeza zaidi katika matumizi va mifumo va

TEHAMA inayosaidia kupunguza mawasiliano ya ana kwa ana katika kutoa huduma kama michakato ya zabuni, usajili wa biashara na namba ya mlipa kodi ili kupunguza mianya ya rushwa.

Kupitia Divisheni ya Mahakama Kuu inayosikiliza kesi za washtakiwa wa makosa ya rushwa kubwa, Serikali imeokoa na kudhibiti matumizi va fedha vasivostahili va zaidi ya Shilingi bilioni 139 kuanzia mwaka wa fedha 2019/ 20 hadi 2021/ 22

F0wNmFCWAAAMjT9.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi wa Taasisi mbalimbali, Wanafunzi pamoja na Wananchi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika

F0wO6ZGWAAEp-bm.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna wa Polisi (CP) Salum Hamduni kuhusu kazi mbalimbali ambazo Taasisi hiyo inafanya kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika.

F0wWZ-cXoAASPYy.jpg

Wasanii wa Kikundi cha ngoma za asili kutoka Zanzibar Kibati wakitumbuiza kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika tarehe 11 Julai, 2023.

F0wVSELWAAA2-5r.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo kutoka Bodi ya Ushauri ya Kupambana na Rushwa Afrika iliyowasilishwa na Makamu Mwenyekiti wa AUABC Mhe. Pascoal Antonio Joaquim

F0wV9bVWAAEB86i.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akinyanyua juu Tuzo kutoka Bodi ya Ushauri ya Kupambana na Rushwa Afrika mara baada ya kukabidhiwa wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika
 
Viongozi vilaza wa bara la kiza wakutana kwenye kikao Cha vikoba kujadili akidi rejea na rejea akidi ya ujinga wao napo utasikia chanzo Cha Afrika kuto endelea ni mabeberu na wakati huo huo pesa walizo kwiba kwenye nchi zao zikiwa kwenye ma-bank ya mabeberu.

Huku honorable causa akiuza bandari za Tanganyika kwa wavaa kobazi wa Dubai.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akielekea mkoani Arusha kwa ajili ya kufunga Maadhimisho ya Siku ya Kupambana na Rushwa Afrika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC)
WhatsApp Image 2023-07-11 at 10.35.25 (1).jpeg

WhatsApp Image 2023-07-11 at 10.35.26 (1).jpeg

WhatsApp Image 2023-07-11 at 10.35.28 (1).jpeg

WhatsApp Image 2023-07-11 at 10.35.30 (2).jpeg

WhatsApp Image 2023-07-11 at 10.35.31.jpeg
 
Ngoja tusikie Ana jipya gani maana naona ruti kila uchwao, Kama vp avunje tu hiyo TAKUKURU Kama Hainan msaada na Nchi yetu.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akielekea mkoani Arusha kwa ajili ya kufunga Maadhimisho ya Siku ya Kupambana na Rushwa Afrika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC)View attachment 2684684
View attachment 2684685
View attachment 2684686
View attachment 2684687
View attachment 2684688
Hivi hawa viongozi wa serikali huwa wanapata muda wa kufanya kazi saa ngapi. Imagine kwa mtindo huu wa Rais kila second day yuko kwenye Ufunguzi,, Kuapisha, Ziara au Sherehe ......!!
 
Mama afanye changes TAKUKURU ya Dr Hosseah ndiyo ilifanya kazi na kuonekana hawa Polisi wala rushwa Shida tupu hawajui lolote Mara Mia Mjeshi Mbung'o alifanya mazuri kiasi Fulani ila Polisi hakuna jipya ni ukuda na upigaji mama lione hili maana utawala bora hayupo coz of corruption
 
Mimi niseme ukweli akili ndogo haiwezi endesha akili kubwa, Hamduni Hana guts kuiendesha PCCB at all, Polisi na rushwa wapi na wapi jamani?

Mama aangalie watu wa kuteua wawe na uzalendo wa juu siyo tu kuwa kamishna au Jaji this is big NOOOOO!!!.

PCCB ifumuliwe iundwe upya tena kuanzia ngazi ya Kata Kama vyombo vingine hapo itakuwa sawa.
 
Changamoto iliyopo ni jinsi jamii na raia kwa ujumla wanavyotafsiri rushwa.
Wengi wanafikiri ni kutoa na kupokea pesa au mali na zaidi siku hizi kuna ngono (ambayo ni vigumu kudhibiti mtoaji).
Kwa ujumla wake, rushwa ni kutumia vishawishi visivyokubalikaau visivyofaa kimaadili (use of improper influence). Ni zaidi ya kutoa au kupokea pesa, mali au ngono.
Haya ni mambo yanayofanyika kila siku kwa sababu tu ya kukosa uelewa.
 
Changamoto iliyopo ni jinsi jamii na raia kwa ujumla wanavyotafsiri rushwa.
Wengi wanafikiri ni kutoa na kupokea pesa au mali na zaidi siku hizi kuna ngono (ambayo ni vigumu kudhibiti mtoaji).
Kwa ujumla wake, rushwa ni kutumia vishawishi visivyokubalikaau visivyofaa kimaadili (use of improper influence). Ni zaidi ya kutoa au kupokea pesa, mali au ngono.
Haya ni mambo yanayofanyika kila siku kwa sababu tu ya kukosa uelewa.
Umenena vyema shida watu wanataka short cuts kupata mahitaji bila vigezo. Nipe nikupe hizi ni petty corruption hata watoto wanafanya mashuleni daily sasa kwenye manunuzi ktk Halmashauri zetu na mawizara huko ndo nux mikataba hewa Mkuu rushwa imezagaa
 
Hivi hawa viongozi wa serikali huwa wanapata muda wa kufanya kazi saa ngapi. Imagine kwa mtindo huu wa Rais kila second day yuko kwenye Ufunguzi,, Kuapisha, Ziara au Sherehe ......!!
ndio majukumu yake hayo..na ndio kazi zenyewe hizo..
 
Saa100 anaroho ngumu ,serikali yake imejaa wala rushwa na yeye anashiriki hilo zoezi jamani
Mkuu bila ammendments ya Sheria za rushwana kuifumua PCCB ikiwemo kubadili uongozi tutadidimia zaidi na kuingia kwenye umaskini mkubwa
 
Back
Top Bottom