Rais Samia ana chaguo, ama kuwa na wanafiki au kuambatana na wakweli wanaopambania taifa lao

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,078
Katikati ya majonzi na masikitiko makubwa kutokana na baadhi ya watu wanafiki, waongo, wenye upeo na uwezo duni, wanaopigania matumbo yao; kuna faraja kubwa.

Sote tunajua wazi kuwa baadhi ya watu, ama kwa kusukumwa na tamaa ya kujinufaisha wao binafsi, au kwa kukosa maarifa na weledi, wameamua kuliangamiza Taifa.

Wataalam mbalimbali, wenye weledi na uelewa mkubwa lakini ambao hawajapungukiwa ukweli wa nafsi na mapenzi makubwa, wamechambua kwa kina, na kwa uwazi kabisa mkataba wa bandari, wakaainisha namna wenzetu wachache kutokana na tamaa zao, walivyolidhalilisha Taifa, kwanza kwa kukubali wageni ndio waliamlie Taifa. Watu hawa waovu, maadui wa Taifa letu, wamefanya yafuatayo (nayataja yale ya msingi tu, lakini TLS na wazazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameainisha yote kwa kina):

1) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP iwe juu ya sheria na katiba ya nchi. Kwenye hili, wakati katiba yetu ya nchi inatamka wazi kuwa ardhi yote ya nchi ni mali ya umma wa Watanzania, na msimamizi wake ni Rais, wao wamekubaliana na DP kuwa sehemu yoyote ya ardhi maeneo ya bandari, na sehemu nyingine yoyote atakayoitaka DP, Serikali italazimika kuwaondoa wananchi, taasisi au makampuni, kutoka kwenye hiyo ardhi anayoitaka DP, na ardhi hiyo itamilikishwa kwa DP.

2) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP atamilikishwa ardhi, kinyume na sheria za nchi. Sheria yetu ya ardhi hairuhusu mgeni kumiliki ardhi. Yeye anaruhusiwa kuitumia tu lakini siyo kumiliki. DP kwa kadiri ya IGA, ambayo haturuhusiwi kujitoa, atamilikishwa ardhi.

3) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa watu watakaoondoshwa kwenye ardhi anayoitaka DP, serikali ndiyo iwalipe fidia. Hii ni kinyume kabisa na sheria yetu ya ardhi kuhusiana na fidia ya ardhi, ambayo inatamka wazi kabisa kuwa mtu, taasisi au kampuni yoyote itakayohitaji ardhi kwa matumizi yoyote yale, ndiyo itakayolazimika kulipa fidia. Lakini kwa DP, serikali itawaondosha watu na taasisi zake, halafu yenyewe ndiyo iwalipe fidia.

4) Wamekula njama na DP kuiondolea nchi heshima yake ya kuwa Taifa huru linaloweza kufanya maamuzi yoyote wakati wowote kwa maslahi ya Taifa kwa kuzingatia katiba na sheria ambazo imeziweka. Kwenye mkataba wa DP, hata kama tukiwapata wawekezaji wengine ambao labda tunaona wana tija kwa Taifa letu, hata kwenye bandari ambazo DP watakuwa hawajawekeza chochote, hatutaruhusiwa mpaka DP aridhie.

5) Wamekula njama na DP kuwezesha uporaji wa bandari ya Dar es Salaam. Sheria zetu za nchi zinatoa haki ya mtu kutambulika kwa mali yake. Na hiyo ndiyo inakupa haki ya kuiuza mali hiyo au hata kuitumia mali yako hiyo kuingia kwenye ubia. Wenzetu hawa, kwa ujambazi wa ajabu, licha ya matrilioni ambayo tumewekeza bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine, wameamua DP apewe bure. Hatutapewa fidia ya uwekezaji tuliofanya, wala uwekezaji tulioufanya hautupi hata ile haki ya kuwa wabia ili nasi tufaidike na faida itakayopatikana, kama ambavyo hawa hawa DP wamefanya huko Uingereza.

6) Wamekula njama na DP, kudharau kabisa sheria yetu ya kodi, na kukubaliana kuwa hizi kodi zetu ambazo zipo kwenye sheria yetu ya kodi, hazitamhusu DP. Yeye atapewa msamaha au kupunguziwa kiwango.

7) Wamekula njama na DP kuhakikisha uhuru wa Taifa unafungwa. Wamekubaliana na DP kuwa kwa mazingira yoyote yale, hata kama DP atakuwa amekiuka mkataba wowote ule kati ya hiyo mikataba midogo itakayofungwa, ni marufuku sisi kama Taifa, kuuvunja mkataba huu, mpaka yeye aridhie (kwa kutufanya wajinga, wameandika kuwa mpaka pande zote zikubaliane. Yaani hata ikitokea DP amefanya makosa, hatuwezi kumfukuza mpaka yeye akubali).

Haya ni machache, wenzetu hawa wasiolitakia mema Taifa letu, wameyafanya. Na vinara kwenye uovu huu, yupo:
Waziri Mbarawa
Majaliwa Majaliwa
Eliezer Feleshi
Tulia Ackson
Wabunge wa bunge batili, wakiongozwa na Musukuma
Mzee Malechela
Wziri Nape

Kwa upande mwingine, unaotia faraja, ni upande wa watu wenye hekima, wenye weledi na upeo, wakweli wa nafsi, wanaolipigania Taifa lao la leo na kesho, wanaoamini kuwa katiba, sheria, mamlaka na uhuru wa Taifa ni lazima vilindwe, vidumishwe na kupiganiwa wakati wote. Zipo taasisi imara, kama vile viongozi wa dini, chama cha wanasheria na wanasheria mbalimbali, wanazuoni wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na watu mbalimbali, wamepaza sauti zao, na kuweka mwongozo wa wapi twende.

Wote wote wenye akili timamu, wanaoelewa, wenye uwezo wa kufundishika hata kama hawana elimu, wanatambua wazi jinsi mkataba kati ya Tanzania na DP World ulivyo wa hovyo na wa kishenzi, na jinsi unavyotweza utu wetu, utaifa wetu na Taifa letu kwa ujumla.

TLS imeuchambua kwa kina mkataba huo. Professor Shivji na wasomi wenzake wa UDSM, wameuchambua kwa kina mkataba huo. Wote wameorodhesha na kubainisha vifungu vyote vya hovyo, jinsi vinavyotubana, jinsi vinavyofuta haki za kikataba na za kisheria tulizoziweka, na namna mkataba huo ulivyo wa kinyonyaji na kutufanya kuwa ni watu tusiokuwa na akili hata ile ya kawaida. Wataalam hawa hawajaishia kuorodhesha tu vipengere vya hovyo, bali wameelezea madhara ya vipengere hivyo, na wametoa mapendekezo ya namna ya kuondoka mahali hapo.

Sasa ni maamuzi ya Rais Samia kuendelea na watu waovu, wanafiki, wanaompamba kwa rushwa ya sifa za kipuuzi, watu wanaopigania matumbo yao kufa na kupona, AU asimame na kuubali ushauri wa watu wenye mapenzi mema na Taifa letu, wenye upeo na uelewa mkubwa na walio wakweli wa nafsi.

Kwa upande mwingine, tunawaomba wote waliosimama kidete kutetea hadhi na rasilimali za Taifa letu, waandae mkutano wa pamoja, ili tutoke na azimio moja. Lakini kikubwa zaidi ni kukubaliana, nini kifanyike, kama waovu hawa wakaendelea na mipango yao ya uovu.

Taasisi hizi, na watu hawa hapa chini, mzidi kubarikiwa kwa dhamira yenu njema kwaajili ya kizazi hiki na wale watakaokuja huko mbeleni. Mungu wetu azidi kuwajalia ujasiri, kuwapeni ulinzi wa kutosha katika kazi hii takatifu mnayoitenda. Hawa hapa chini ni wachache niliowakumbuka. Ongezeni orodha yao.

Viongozi wa dini
Chama cha Wanasheria Nchini
Wanazuoni wa Chuo Kikuu Dare es Salaam
Jaji Stela Augustine
Dr. Wilbroad Slaa
Prof. Lipumba
Prof. Shivji
Prof. Tibaijuka
Wakili Alphonce Lusako
Mwanasheria Dr. Rugemeleza
Tundu Lisu
Freeman Mbowe

Na wengine wengi.
 
Mpigania tumbo namba moja Tanzania akihamasisha ufisadi nchini👇🐒🐒🐒
 
Katikati ya majonzi na masikitiko makubwa kutokana na baadhi ya watu wanafiki, waongo, wenye upeo na uwezo duni, wanaopigania matumbo yao; kuna faraja kubwa.

Sote tunajua wazi kuwa baadhi ya watu, ama kwa kusukumwa na tamaa ya kujinufaisha wao binafsi, au kwa kukosa maarifa na weledi, wameamua kuliangamiza Taifa.

Wataalam mbalimbali, wenye weledi na uelewa mkubwa lakini ambao hawajapungukiwa ukweli wa nafsi na mapenzi makubwa, wamechambua kwa kina, na kwa uwazi kabisa mkataba wa bandari, wakaainisha namna wenzetu wachache kutokana na tamaa zao, walivyolidhalilisha Taifa, kwanza kwa kukubali wageni ndio waliamlie Taifa. Watu hawa waovu, maadui wa Taifa letu, wamefanya yafuatayo (nayataja yale ya msingi tu, lakini TLS na wazazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameainisha yote kwa kina):

1) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP iwe juu ya sheria na katiba ya nchi. Kwenye hili, wakati katiba yetu ya nchi inatamka wazi kuwa ardhi yote ya nchi ni mali ya umma wa Watanzania, na msimamizi wake ni Rais, wao wamekubaliana na DP kuwa sehemu yoyote ya ardhi maeneo ya bandari, na sehemu nyingine yoyote atakayoitaka DP, Serikali italazimika kuwaondoa wananchi, taasisi au makampuni, kutoka kwenye hiyo ardhi anayoitaka DP, na ardhi hiyo itamilikishwa kwa DP.

2) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP atamilikishwa ardhi, kinyume na sheria za nchi. Sheria yetu ya ardhi hairuhusu mgeni kumiliki ardhi. Yeye anaruhusiwa kuitumia tu lakini siyo kumiliki. DP kwa kadiri ya IGA, ambayo haturuhusiwi kujitoa, atamilikishwa ardhi.

3) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa watu watakaoondoshwa kwenye ardhi anayoitaka DP, serikali ndiyo iwalipe fidia. Hii ni kinyume kabisa na sheria yetu ya ardhi kuhusiana na fidia ya ardhi, ambayo inatamka wazi kabisa kuwa mtu, taasisi au kampuni yoyote itakayohitaji ardhi kwa matumizi yoyote yale, ndiyo itakayolazimika kulipa fidia. Lakini kwa DP, serikali itawaondosha watu na taasisi zake, halafu yenyewe ndiyo iwalipe fidia.

4) Wamekula njama na DP kuiondolea nchi heshima yake ya kuwa Taifa huru linaloweza kufanya maamuzi yoyote wakati wowote kwa maslahi ya Taifa kwa kuzingatia katiba na sheria ambazo imeziweka. Kwenye mkataba wa DP, hata kama tukiwapata wawekezaji wengine ambao labda tunaona wana tija kwa Taifa letu, hata kwenye bandari ambazo DP watakuwa hawajawekeza chochote, hatutaruhusiwa mpaka DP aridhie.

5) Wamekula njama na DP kuwezesha uporaji wa bandari ya Dar es Salaam. Sheria zetu za nchi zinatoa haki ya mtu kutambulika kwa mali yake. Na hiyo ndiyo inakupa haki ya kuiuza mali hiyo au hata kuitumia mali yako hiyo kuingia kwenye ubia. Wenzetu hawa, kwa ujambazi wa ajabu, licha ya matrilioni ambayo tumewekeza bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine, wameamua DP apewe bure. Hatutapewa fidia ya uwekezaji tuliofanya, wala uwekezaji tulioufanya hautupi hata ile haki ya kuwa wabia ili nasi tufaidike na faida itakayopatikana, kama ambavyo hawa hawa DP wamefanya huko Uingereza.

6) Wamekula njama na DP, kudharau kabisa sheria yetu ya kodi, na kukubaliana kuwa hizi kodi zetu ambazo zipo kwenye sheria yetu ya kodi, hazitamhusu DP. Yeye atapewa msamaha au kupunguziwa kiwango.

7) Wamekula njama na DP kuhakikisha uhuru wa Taifa unafungwa. Wamekubaliana na DP kuwa kwa mazingira yoyote yale, hata kama DP atakuwa amekiuka mkataba wowote ule kati ya hiyo mikataba midogo itakayofungwa, ni marufuku sisi kama Taifa, kuuvunja mkataba huu, mpaka yeye aridhie (kwa kutufanya wajinga, wameandika kuwa mpaka pande zote zikubaliane. Yaani hata ikitokea DP amefanya makosa, hatuwezi kumfukuza mpaka yeye akubali).

Haya ni machache, wenzetu hawa wasiolitakia mema Taifa letu, wameyafanya. Na vinara kwenye uovu huu, yupo:
Waziri Mbarawa
Majaliwa Majaliwa
Eliezer Feleshi
Tulia Ackson
Wabunge wa bunge batili, wakiongozwa na Musukuma
Mzee Malechela
Wziri Nape

Kwa upande mwingine, unaotia faraja, ni upande wa watu wenye hekima, wenye weledi na upeo, wakweli wa nafsi, wanaolipigania Taifa lao la leo na kesho, wanaoamini kuwa katiba, sheria, mamlaka na uhuru wa Taifa ni lazima vilindwe, vidumishwe na kupiganiwa wakati wote. Zipo taasisi imara, kama vile viongozi wa dini, chama cha wanasheria na wanasheria mbalimbali, wanazuoni wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na watu mbalimbali, wamepaza sauti zao, na kuweka mwongozo wa wapi twende.

Wote wote wenye akili timamu, wanaoelewa, wenye uwezo wa kufundishika hata kama hawana elimu, wanatambua wazi jinsi mkataba kati ya Tanzania na DP World ulivyo wa hovyo na wa kishenzi, na jinsi unavyotweza utu wetu, utaifa wetu na Taifa letu kwa ujumla.

TLS imeuchambua kwa kina mkataba huo. Professor Shivji na wasomi wenzake wa UDSM, wameuchambua kwa kina mkataba huo. Wote wameorodhesha na kubainisha vifungu vyote vya hovyo, jinsi vinavyotubana, jinsi vinavyofuta haki za kikataba na za kisheria tulizoziweka, na namna mkataba huo ulivyo wa kinyonyaji na kutufanya kuwa ni watu tusiokuwa na akili hata ile ya kawaida. Wataalam hawa hawajaishia kuorodhesha tu vipengere vya hovyo, bali wameelezea madhara ya vipengere hivyo, na wametoa mapendekezo ya namna ya kuondoka mahali hapo.

Sasa ni maamuzi ya Rais Samia kuendelea na watu waovu, wanafiki, wanaompamba kwa rushwa ya sifa za kipuuzi, watu wanaopigania matumbo yao kufa na kupona, AU asimame na kuubali ushauri wa watu wenye mapenzi mema na Taifa letu, wenye upeo na uelewa mkubwa na walio wakweli wa nafsi.

Kwa upande mwingine, tunawaomba wote waliosimama kidete kutetea hadhi na rasilimali za Taifa letu, waandae mkutano wa pamoja, ili tutoke na azimio moja. Lakini kikubwa zaidi ni kukubaliana, nini kifanyike, kama waovu hawa wakaendelea na mipango yao ya uovu.

Taasisi hizi, na watu hawa hapa chini, mzidi kubarikiwa kwa dhamira yenu njema kwaajili ya kizazi hiki na wale watakaokuja huko mbeleni. Mungu wetu azidi kuwajalia ujasiri, kuwapeni ulinzi wa kutosha katika kazi hii takatifu mnayoitenda. Hawa hapa chini ni wachache niliowakumbuka. Ongezeni orodha yao.

Viongozi wa dini
Chama cha Wanasheria Nchini
Wanazuoni wa Chuo Kikuu Dare es Salaam
Jaji Stela Augustine
Dr. Wilbroad Slaa
Prof. Lipumba
Prof. Shivji
Prof. Tibaijuka
Wakili Alphonce Lusako
Mwanasheria Dr. Rugemeleza
Tundu Lisu
Freeman Mbowe

Na wengine wengi.
It's too late!! Tayari tawala zimetengeneza circle ya uchawa na praise and worship!!
 
Katikati ya majonzi na masikitiko makubwa kutokana na baadhi ya watu wanafiki, waongo, wenye upeo na uwezo duni, wanaopigania matumbo yao; kuna faraja kubwa.

Sote tunajua wazi kuwa baadhi ya watu, ama kwa kusukumwa na tamaa ya kujinufaisha wao binafsi, au kwa kukosa maarifa na weledi, wameamua kuliangamiza Taifa.

Wataalam mbalimbali, wenye weledi na uelewa mkubwa lakini ambao hawajapungukiwa ukweli wa nafsi na mapenzi makubwa, wamechambua kwa kina, na kwa uwazi kabisa mkataba wa bandari, wakaainisha namna wenzetu wachache kutokana na tamaa zao, walivyolidhalilisha Taifa, kwanza kwa kukubali wageni ndio waliamlie Taifa. Watu hawa waovu, maadui wa Taifa letu, wamefanya yafuatayo (nayataja yale ya msingi tu, lakini TLS na wazazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameainisha yote kwa kina):

1) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP iwe juu ya sheria na katiba ya nchi. Kwenye hili, wakati katiba yetu ya nchi inatamka wazi kuwa ardhi yote ya nchi ni mali ya umma wa Watanzania, na msimamizi wake ni Rais, wao wamekubaliana na DP kuwa sehemu yoyote ya ardhi maeneo ya bandari, na sehemu nyingine yoyote atakayoitaka DP, Serikali italazimika kuwaondoa wananchi, taasisi au makampuni, kutoka kwenye hiyo ardhi anayoitaka DP, na ardhi hiyo itamilikishwa kwa DP.

2) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP atamilikishwa ardhi, kinyume na sheria za nchi. Sheria yetu ya ardhi hairuhusu mgeni kumiliki ardhi. Yeye anaruhusiwa kuitumia tu lakini siyo kumiliki. DP kwa kadiri ya IGA, ambayo haturuhusiwi kujitoa, atamilikishwa ardhi.

3) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa watu watakaoondoshwa kwenye ardhi anayoitaka DP, serikali ndiyo iwalipe fidia. Hii ni kinyume kabisa na sheria yetu ya ardhi kuhusiana na fidia ya ardhi, ambayo inatamka wazi kabisa kuwa mtu, taasisi au kampuni yoyote itakayohitaji ardhi kwa matumizi yoyote yale, ndiyo itakayolazimika kulipa fidia. Lakini kwa DP, serikali itawaondosha watu na taasisi zake, halafu yenyewe ndiyo iwalipe fidia.

4) Wamekula njama na DP kuiondolea nchi heshima yake ya kuwa Taifa huru linaloweza kufanya maamuzi yoyote wakati wowote kwa maslahi ya Taifa kwa kuzingatia katiba na sheria ambazo imeziweka. Kwenye mkataba wa DP, hata kama tukiwapata wawekezaji wengine ambao labda tunaona wana tija kwa Taifa letu, hata kwenye bandari ambazo DP watakuwa hawajawekeza chochote, hatutaruhusiwa mpaka DP aridhie.

5) Wamekula njama na DP kuwezesha uporaji wa bandari ya Dar es Salaam. Sheria zetu za nchi zinatoa haki ya mtu kutambulika kwa mali yake. Na hiyo ndiyo inakupa haki ya kuiuza mali hiyo au hata kuitumia mali yako hiyo kuingia kwenye ubia. Wenzetu hawa, kwa ujambazi wa ajabu, licha ya matrilioni ambayo tumewekeza bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine, wameamua DP apewe bure. Hatutapewa fidia ya uwekezaji tuliofanya, wala uwekezaji tulioufanya hautupi hata ile haki ya kuwa wabia ili nasi tufaidike na faida itakayopatikana, kama ambavyo hawa hawa DP wamefanya huko Uingereza.

6) Wamekula njama na DP, kudharau kabisa sheria yetu ya kodi, na kukubaliana kuwa hizi kodi zetu ambazo zipo kwenye sheria yetu ya kodi, hazitamhusu DP. Yeye atapewa msamaha au kupunguziwa kiwango.

7) Wamekula njama na DP kuhakikisha uhuru wa Taifa unafungwa. Wamekubaliana na DP kuwa kwa mazingira yoyote yale, hata kama DP atakuwa amekiuka mkataba wowote ule kati ya hiyo mikataba midogo itakayofungwa, ni marufuku sisi kama Taifa, kuuvunja mkataba huu, mpaka yeye aridhie (kwa kutufanya wajinga, wameandika kuwa mpaka pande zote zikubaliane. Yaani hata ikitokea DP amefanya makosa, hatuwezi kumfukuza mpaka yeye akubali).

Haya ni machache, wenzetu hawa wasiolitakia mema Taifa letu, wameyafanya. Na vinara kwenye uovu huu, yupo:
Waziri Mbarawa
Majaliwa Majaliwa
Eliezer Feleshi
Tulia Ackson
Wabunge wa bunge batili, wakiongozwa na Musukuma
Mzee Malechela
Wziri Nape

Kwa upande mwingine, unaotia faraja, ni upande wa watu wenye hekima, wenye weledi na upeo, wakweli wa nafsi, wanaolipigania Taifa lao la leo na kesho, wanaoamini kuwa katiba, sheria, mamlaka na uhuru wa Taifa ni lazima vilindwe, vidumishwe na kupiganiwa wakati wote. Zipo taasisi imara, kama vile viongozi wa dini, chama cha wanasheria na wanasheria mbalimbali, wanazuoni wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na watu mbalimbali, wamepaza sauti zao, na kuweka mwongozo wa wapi twende.

Wote wote wenye akili timamu, wanaoelewa, wenye uwezo wa kufundishika hata kama hawana elimu, wanatambua wazi jinsi mkataba kati ya Tanzania na DP World ulivyo wa hovyo na wa kishenzi, na jinsi unavyotweza utu wetu, utaifa wetu na Taifa letu kwa ujumla.

TLS imeuchambua kwa kina mkataba huo. Professor Shivji na wasomi wenzake wa UDSM, wameuchambua kwa kina mkataba huo. Wote wameorodhesha na kubainisha vifungu vyote vya hovyo, jinsi vinavyotubana, jinsi vinavyofuta haki za kikataba na za kisheria tulizoziweka, na namna mkataba huo ulivyo wa kinyonyaji na kutufanya kuwa ni watu tusiokuwa na akili hata ile ya kawaida. Wataalam hawa hawajaishia kuorodhesha tu vipengere vya hovyo, bali wameelezea madhara ya vipengere hivyo, na wametoa mapendekezo ya namna ya kuondoka mahali hapo.

Sasa ni maamuzi ya Rais Samia kuendelea na watu waovu, wanafiki, wanaompamba kwa rushwa ya sifa za kipuuzi, watu wanaopigania matumbo yao kufa na kupona, AU asimame na kuubali ushauri wa watu wenye mapenzi mema na Taifa letu, wenye upeo na uelewa mkubwa na walio wakweli wa nafsi.

Kwa upande mwingine, tunawaomba wote waliosimama kidete kutetea hadhi na rasilimali za Taifa letu, waandae mkutano wa pamoja, ili tutoke na azimio moja. Lakini kikubwa zaidi ni kukubaliana, nini kifanyike, kama waovu hawa wakaendelea na mipango yao ya uovu.

Taasisi hizi, na watu hawa hapa chini, mzidi kubarikiwa kwa dhamira yenu njema kwaajili ya kizazi hiki na wale watakaokuja huko mbeleni. Mungu wetu azidi kuwajalia ujasiri, kuwapeni ulinzi wa kutosha katika kazi hii takatifu mnayoitenda. Hawa hapa chini ni wachache niliowakumbuka. Ongezeni orodha yao.

Viongozi wa dini
Chama cha Wanasheria Nchini
Wanazuoni wa Chuo Kikuu Dare es Salaam
Jaji Stela Augustine
Dr. Wilbroad Slaa
Prof. Lipumba
Prof. Shivji
Prof. Tibaijuka
Wakili Alphonce Lusako
Mwanasheria Dr. Rugemeleza
Tundu Lisu
Freeman Mbowe

Na wengine wengi.
Na hapo ndo anaogopa kurudi nyuma .kww hiyo nguvu iliyopo ni kuonyesha kwa nguvu zote kuww kile kilichosainiwa kuwa eti ni cha kweli na kina maslahi kwa umma na kuwa rais anafanya kazi nzuri
 
Naamini mjinga siku zote lazima aambatane na wajinga wenzake, ndio maana wakitokea werevu kuwaonesha njia wanawaona maadui.

Wanawaona maasui kwasababu wanakoaa hoja za maana kupinga wanachoambiwa, hivyo wanaona suluhisho ni kuleta chuki za aina yoyote ilimradi wafiche ujinga wao, bahati nzuri werevu wanawatambua na ujinga wao kuupuuza.
 
..hili suala ni rahisi kulitatua lakini sielewi kwanini Ssh analifanya kuwa gumu.

..nashangazwa sana na kampeni za hila na kilaghai kutetea maamuzi yaliyofanyika kuhusu bandari.

..nashangazwa pia na Ssh kukubali kutetewa na kuhusishwa na watu wa hovyohovyo ktk suala hili.

..nadhani njia sahihi ni Bunge kutengua azimio lake. Na liandaliwe azimio jipya lisiloitia nchi kitanzi.

..pia maadamu wameshaamua kwenda na DP basi uandaliwe mkataba wa kuwa-replace Ticts ktk kuendesha container terminal.

..pia wanaweza kuwapa Dp mkataba wa kuwa management company wa bandari ya Dsm kama tulivyowaajiri Netgroup kusimamia Tanesco wakati wa Mkapa.
 
Katikati ya majonzi na masikitiko makubwa kutokana na baadhi ya watu wanafiki, waongo, wenye upeo na uwezo duni, wanaopigania matumbo yao; kuna faraja kubwa.

Sote tunajua wazi kuwa baadhi ya watu, ama kwa kusukumwa na tamaa ya kujinufaisha wao binafsi, au kwa kukosa maarifa na weledi, wameamua kuliangamiza Taifa.

Wataalam mbalimbali, wenye weledi na uelewa mkubwa lakini ambao hawajapungukiwa ukweli wa nafsi na mapenzi makubwa, wamechambua kwa kina, na kwa uwazi kabisa mkataba wa bandari, wakaainisha namna wenzetu wachache kutokana na tamaa zao, walivyolidhalilisha Taifa, kwanza kwa kukubali wageni ndio waliamlie Taifa. Watu hawa waovu, maadui wa Taifa letu, wamefanya yafuatayo (nayataja yale ya msingi tu, lakini TLS na wazazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameainisha yote kwa kina):

1) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP iwe juu ya sheria na katiba ya nchi. Kwenye hili, wakati katiba yetu ya nchi inatamka wazi kuwa ardhi yote ya nchi ni mali ya umma wa Watanzania, na msimamizi wake ni Rais, wao wamekubaliana na DP kuwa sehemu yoyote ya ardhi maeneo ya bandari, na sehemu nyingine yoyote atakayoitaka DP, Serikali italazimika kuwaondoa wananchi, taasisi au makampuni, kutoka kwenye hiyo ardhi anayoitaka DP, na ardhi hiyo itamilikishwa kwa DP.

2) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa DP atamilikishwa ardhi, kinyume na sheria za nchi. Sheria yetu ya ardhi hairuhusu mgeni kumiliki ardhi. Yeye anaruhusiwa kuitumia tu lakini siyo kumiliki. DP kwa kadiri ya IGA, ambayo haturuhusiwi kujitoa, atamilikishwa ardhi.

3) Wamekula njama na kukubaliana na DP kuwa watu watakaoondoshwa kwenye ardhi anayoitaka DP, serikali ndiyo iwalipe fidia. Hii ni kinyume kabisa na sheria yetu ya ardhi kuhusiana na fidia ya ardhi, ambayo inatamka wazi kabisa kuwa mtu, taasisi au kampuni yoyote itakayohitaji ardhi kwa matumizi yoyote yale, ndiyo itakayolazimika kulipa fidia. Lakini kwa DP, serikali itawaondosha watu na taasisi zake, halafu yenyewe ndiyo iwalipe fidia.

4) Wamekula njama na DP kuiondolea nchi heshima yake ya kuwa Taifa huru linaloweza kufanya maamuzi yoyote wakati wowote kwa maslahi ya Taifa kwa kuzingatia katiba na sheria ambazo imeziweka. Kwenye mkataba wa DP, hata kama tukiwapata wawekezaji wengine ambao labda tunaona wana tija kwa Taifa letu, hata kwenye bandari ambazo DP watakuwa hawajawekeza chochote, hatutaruhusiwa mpaka DP aridhie.

5) Wamekula njama na DP kuwezesha uporaji wa bandari ya Dar es Salaam. Sheria zetu za nchi zinatoa haki ya mtu kutambulika kwa mali yake. Na hiyo ndiyo inakupa haki ya kuiuza mali hiyo au hata kuitumia mali yako hiyo kuingia kwenye ubia. Wenzetu hawa, kwa ujambazi wa ajabu, licha ya matrilioni ambayo tumewekeza bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine, wameamua DP apewe bure. Hatutapewa fidia ya uwekezaji tuliofanya, wala uwekezaji tulioufanya hautupi hata ile haki ya kuwa wabia ili nasi tufaidike na faida itakayopatikana, kama ambavyo hawa hawa DP wamefanya huko Uingereza.

6) Wamekula njama na DP, kudharau kabisa sheria yetu ya kodi, na kukubaliana kuwa hizi kodi zetu ambazo zipo kwenye sheria yetu ya kodi, hazitamhusu DP. Yeye atapewa msamaha au kupunguziwa kiwango.

7) Wamekula njama na DP kuhakikisha uhuru wa Taifa unafungwa. Wamekubaliana na DP kuwa kwa mazingira yoyote yale, hata kama DP atakuwa amekiuka mkataba wowote ule kati ya hiyo mikataba midogo itakayofungwa, ni marufuku sisi kama Taifa, kuuvunja mkataba huu, mpaka yeye aridhie (kwa kutufanya wajinga, wameandika kuwa mpaka pande zote zikubaliane. Yaani hata ikitokea DP amefanya makosa, hatuwezi kumfukuza mpaka yeye akubali).

Haya ni machache, wenzetu hawa wasiolitakia mema Taifa letu, wameyafanya. Na vinara kwenye uovu huu, yupo:
Waziri Mbarawa
Majaliwa Majaliwa
Eliezer Feleshi
Tulia Ackson
Wabunge wa bunge batili, wakiongozwa na Musukuma
Mzee Malechela
Wziri Nape

Kwa upande mwingine, unaotia faraja, ni upande wa watu wenye hekima, wenye weledi na upeo, wakweli wa nafsi, wanaolipigania Taifa lao la leo na kesho, wanaoamini kuwa katiba, sheria, mamlaka na uhuru wa Taifa ni lazima vilindwe, vidumishwe na kupiganiwa wakati wote. Zipo taasisi imara, kama vile viongozi wa dini, chama cha wanasheria na wanasheria mbalimbali, wanazuoni wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na watu mbalimbali, wamepaza sauti zao, na kuweka mwongozo wa wapi twende.

Wote wote wenye akili timamu, wanaoelewa, wenye uwezo wa kufundishika hata kama hawana elimu, wanatambua wazi jinsi mkataba kati ya Tanzania na DP World ulivyo wa hovyo na wa kishenzi, na jinsi unavyotweza utu wetu, utaifa wetu na Taifa letu kwa ujumla.

TLS imeuchambua kwa kina mkataba huo. Professor Shivji na wasomi wenzake wa UDSM, wameuchambua kwa kina mkataba huo. Wote wameorodhesha na kubainisha vifungu vyote vya hovyo, jinsi vinavyotubana, jinsi vinavyofuta haki za kikataba na za kisheria tulizoziweka, na namna mkataba huo ulivyo wa kinyonyaji na kutufanya kuwa ni watu tusiokuwa na akili hata ile ya kawaida. Wataalam hawa hawajaishia kuorodhesha tu vipengere vya hovyo, bali wameelezea madhara ya vipengere hivyo, na wametoa mapendekezo ya namna ya kuondoka mahali hapo.

Sasa ni maamuzi ya Rais Samia kuendelea na watu waovu, wanafiki, wanaompamba kwa rushwa ya sifa za kipuuzi, watu wanaopigania matumbo yao kufa na kupona, AU asimame na kuubali ushauri wa watu wenye mapenzi mema na Taifa letu, wenye upeo na uelewa mkubwa na walio wakweli wa nafsi.

Kwa upande mwingine, tunawaomba wote waliosimama kidete kutetea hadhi na rasilimali za Taifa letu, waandae mkutano wa pamoja, ili tutoke na azimio moja. Lakini kikubwa zaidi ni kukubaliana, nini kifanyike, kama waovu hawa wakaendelea na mipango yao ya uovu.

Taasisi hizi, na watu hawa hapa chini, mzidi kubarikiwa kwa dhamira yenu njema kwaajili ya kizazi hiki na wale watakaokuja huko mbeleni. Mungu wetu azidi kuwajalia ujasiri, kuwapeni ulinzi wa kutosha katika kazi hii takatifu mnayoitenda. Hawa hapa chini ni wachache niliowakumbuka. Ongezeni orodha yao.

Viongozi wa dini
Chama cha Wanasheria Nchini
Wanazuoni wa Chuo Kikuu Dare es Salaam
Jaji Stela Augustine
Dr. Wilbroad Slaa
Prof. Lipumba
Prof. Shivji
Prof. Tibaijuka
Wakili Alphonce Lusako
Mwanasheria Dr. Rugemeleza
Tundu Lisu
Freeman Mbowe

Na wengine wengi.
yeye samia mwenyewe yupo kundi gani kati ya hayo mawili? Choice pekee aliyonayo ni kutuachia nchi yetu aondoke
 
Namkumbuka Mzee Bulembo alivyokuwa akimsifia Magufuli wakati akiwa hai na jinsi alivyokuja kumkandia baada ya kufariki. Likewise kwa Nape, Mwigulu, Makamba na Mbarawa.

Mama hawa viongozi wa CCM hakuna atakayekukosoa zaidi ya kukusifia hata kama unakwenda shimoni.

Kama vikao vya kamati kuu na NEC vimekubariki na huu mzimu wa world basi una janga na zengwe wanakutengenezea mbele.
 
Back
Top Bottom