Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,327
- 24,209
Nimefarijika na moyo wa Mama Samia, kweli moyo wake una Bwana Mungu ndani yake.
Jana wakati wa kumuaga Eng. Patrick Mfugale alitumia Neno toka Biblia Takatifu, Neno liloleta faraja kwa waombolezaji wengi pale Karimjee.
Alisoma kutoka kitabu cha Joshua 1:9
"Je, si mimi niliyekuamuru uwe jasiri na imara? Basi uwe jasiri na imara. Usitetemeke wala kuogopa, kwa maana mimi Yehova Mungu wako nipo pamoja nawe mahali popote utakapoenda.”
Neno hili la kumsindikiza Eng Mfugale limepoza wengi katika utekelezaji wa kazi za serikali, kwamba na Bwana Mungu yuko pamoja nao.
Amen.