Rais Samia aduwaza wachumi nchini

Rais Samia aduwaza wachumi nchini

Kwa kusifia hatujambo badae mnabaki mdomo wazi wazee wa kupika data.
 
Iongezeke reserve isiongezeke wananchi wanataka kuona direct impact on improving social welfare. Hata kipindi cha mwendazake ngonjera za uchumi kupanda mpaka kufikia uchumi wa kati zilikuwa nyingi sana. Yale yale yanajirudia kuwa "HAKUNA RAIS ALIYEWAHI KUIFIKISHA NCHI MAHALI HAPA"
Wananchi hawataki ngonjera hizo maana hazina msaada wowote katika kuboresha maisha yao. Let's be results oriented people
 
Kazi kubwa na nzuri anazozifanya Rais Samia Suluhu Hassan zimewaduwaza wachumi,

Hii ni baada ya akiba ya fedha za kigeni ( Gross official foreign reserves ) kuongezeka zaidi ndani ya miezi miwili tu nakufikia $6.7BL sawa na TZS 15.41 kutoka $5.9BL sawa na TZS 13.57 mwezi Septemba,

Ongezeko hili ni karibu TZS 2 trilioni linalomfanya Rais Samia ndani ya kipindi chake hiki kifupi kuongeza Jumla ya TZS 4Trilion kwenye hifadhi ya fedha za kigeni,rekodi ambayo haijawahi kufikiwa na Rais yeyote wa awamu yeyote,

Ongezeko hili linachangizwa zaidi na uuzaji nje ( Exports ) wa bidhaa pamoja na huduma hasa mazao ya Chakula kama mchele, Mahindi, maharagwe na mboga mboga,

Kwamsiojua,ongezeko hili ni mbali ya ongezeko la gharama za uagizaji mafuta nje zilizokua kwa 18.3% nakufikia $1.7BL

Jambo la Pili ni Uwekezaji mkubwa kutoka inje Foreign Direct Investments ( FDIs ) uliofikia $2.9BL sawa na TZS 6.7Trilioni,

Ukuaji huu wa uwekezaji ni sawa na mara sita zaidi ya uwekezaji wote uliofanywa mwaka uliopita katika kipindi kama hicho cha kati ya Mwezi Machi na Agosti,

Ongezeko hili linaweza kuagiza bidhaa na huduma nje kwa kipindi kisichopungua karibu miezi saba rekodi ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuwako wa Taifa hili miaka sitini ( 60 ) iliyopita,

Tanzania kwa sasa ndio nchi inayokuza hifadhi yake kwa kasi Ukanda mzima wa Africa Mashariki na Tumevuka lengo la EAC lakuwa na akiba ya kuagiza bidhaa na huduma nje kwa kipindi kisichopungua miezi 4.5

View attachment 2018173
Ndio hivyo hamna haja ya kusoma siku hizi sijui sayansi uchumi , sheria n.k
 
Inapendeza na ahsante kwa taarifa...

Kwenye hizo tozo zinahesabika pia...
 
Mimi nahisi lazima kutakuwa na Tanzania mbili , ya wanao nufaika na wanao sota
Na wanaoziona na kufurahia hiyo mi-US$ watakuwa wale wa Tanzania ya pili a.k.a Dola tena exemption ya kulipa kodi hata wakiagiza magari toka nje.
 
Na hiyo Tanzania ya pili hawafiki hata laki moja mzee...ni kakikundi flani kama kale ka kina Pablo escoba.
 
Walioongoza nchi kwa kutegemea kudra za Mungu ni awamu ya 5,,sasa hivi awamu ya 6 tunaweka mipango ambayo haitategemea kudra za Mungu huku tukimuomba Mungu Hali itengamae tupate mda wa kujitayarisha..
Mmea wa Arusha katika ubora wake !
 
Hayo mahela waga ni ya nini kama kila siku tunaenda kukopa, maji umeme full mgao na plus hakuna ajira wala dalili za watu kuajiriwa huwa kuna point gani ya kuwa na hizo hela sasa
Akikujibu nitag
 
Wewe nawe sijui mmea wa Njombe unakuendesha. Watu mtaani wanalia maisha magumu unakuja na maelezo ya ajabu ajabu.
Hayo maisha magumu kayaleta Samia? Meno vyuma kukaza likianza lini? Je viliwahi kulegea? Ugumi wa maisha ni muendelezo tuu wa side effects za sera mbovu za Jiwe..

Mama anafanya kila kitu kuhakikisha fedha zinarudi mtaani kwa kuleta programu za kuchochea uchumi,ajira mpya na kufuta/ kupunguza tozo mbalimbali..

Kuharibu ni rahisi Sana kujenga haijawahi kuwa rahisi,kwa mwendo wa ukuaji wa uchumi na uwekezaji unaozidi kukua itachukua mda uchumi ku trickle down Ili watu wa chini kabisa waone manufaa yake ingawa watakuwa wanaona kwenye huduma za jamii na miundombinu but income poverty bado itachukua mda.

Go Samia go 👇

Screenshot_20211121-070752.png


Screenshot_20211121-070612.png


Screenshot_20211121-070819.png


Screenshot_20211121-070907.png


Screenshot_20211112-093702.png


Screenshot_20211110-085639.png


Screenshot_20211108-204642.png


Screenshot_20211111-174547.png


Screenshot_20211113-135336.png
 
Ujinga huu mliufanya miaka mitano iliyopita sasa hivi mnaponda jiwe kwamba alikua hashauriki.
 
Baada ya kukwapua pesa benki kuu sasa mmeanza na lopolopo za kihuni, serikali mufilisi itabwaka na kubwaka ila ukweli uchumi zero, miradi ya kimkakati imesimama.
 
wewe ni zaidi ya mpumbavu, sikulaumu yawezekana unataka cheo au unakula kupitia kwake.Kiufupi tu hali ni mbaya mbaya sana
 
Tozo hizo sio mchezo,tarehe 2 November numenunua umeme wamekata,leo 21 November Tena numenunua wamekata Tena,kwa Nini kusiwe na mpunga wa kutakata
 
Hawataki kubadilika na visheria monopoly walivyoweka ambavyo badala ya kurekebisha matatizo vimetufanya tumekuwa watumwa na maskini, TANESCO haina uwezo wa kuhudumia watu milioni 60, waruhusu watu binafsi wafanye biashara ya umeme, imagine TTCL au UDA ndio zingekuwa ndio kampuni pekee za kutoa hizo huduma
Angalia utaambiwa umetumwa na Makamba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom