Habari wadau,
Ingawa ana muda mfupi madarakani lakini nimejaribu kumfuatilia Magufuli na kugundua kuwa itamchukua muda mrefu sana kutulia na kuanza mission za maendeleo ya nchi yetu.
Magufuli ni mtu mwenye kujiamini, lakini hadi sasa haamini kuwa yeye kachaguliwa kuwa RAIS wa nchi hii. Badala ya kukaa na kuwa makini na majukumu yake, bado anatumia muda kujionesha na kutangaza kuwa yeye ni Rais, wakati tayari ana wadhifa huo.
Zipo kauli kadhaa ambazo hazihitajiki kuzitamka, mfano;
1.Mimi ndio Rais nikihamia Dodoma watanifuata wote vinginevyo hawapati mishahara au waache kazi (Utadhani kuna aliembishia)
2. Siamini kama leo wewe Kikwete ungeniomba pesa za ukarabati wa chuo maana wewe ulikuwa Rais
3. Nikihamia Dodoma nyumba zote za serikali zilizoko Dar es salaam nitaziuza ( Utadhani za familia yake)
4. Mimi ndio mkuu wa Sumatra nchi nzima
Ukitizama kauli hizo chache utagundua kuwa bado Magufuli hajatulia, badala yake anatumia muda mwingi kuonesha Power yake, au kutaka sifa
Jambo lingine; Magufuli anaangaika na "audience", kwamba watu wanasemaje?, au nini kinawafurahia kusikia?, ndio maana mahamuzi mengi anafanya kwa pupa hili ashangiliwe na wananchi.
Mimi naamini kama hasipoacha tabia za kuonesha kuwa yeye ndie mwenye "POWER" na sifa ambazo hazina msingi atajikuta miaka 2 au 3 imepita na hakuna alilofanya. Matokeo yake itakuwa kama wakati ule ambapo wana wa Izrael walitamani kurudi Misri, kwamba bora kule tulikuwa watumwa lakini tulikuwa tunakula na kunywa. Yaani wananchi wataona bora turudi enzi za Kikwete.