Baada ya ukimya na kutoonekana kwa JPM kama ilivyo kawaida yake, Waziri Mkuu Kasim Majaliwa amewatoa hofu Watanzania, "Rais ni mzima bukheri wa afya na anachapa kazi Ikulu".
Naye Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akasema, "nchi iko salama, tushikamane kuliko wakati wowote."
Kwa kauli hizi ninaamini Mkulu yuko bize Ikulu akipiga kazi kama ilivyo slogan yake "hapa kazi tu".
Kama mwananchi wake namshauri katika hizo kazi anazochapa basi aivunje Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto. Hii wizara ni kubwa mno.
Napendekeza, kutokana na unyeti wa suala la Afya, Afya ibaki peke yake na Waziri wake. Hayo mengine yabaki kama Wizara ya Jamii.
Popote duniani wizara ya Afya ni sekta nyeti mno. Vita hii ya Covid-19 imethibitisha unyeti wa wizara hii. Ni vigumu yule mama kujigawa kushughulika na afya na hapo hapo ashughulike ni wazee, kina mama na watoto. Tunaweza kuona alivyofeli kuongoza wizara hii lakini kimsingi ni ukubwa na upana wake.
Hizo kazi unazochapa Ikulu, chapa na hili. Ahsante.
Au nasema uongo ndugu zangu!
Naye Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akasema, "nchi iko salama, tushikamane kuliko wakati wowote."
Kwa kauli hizi ninaamini Mkulu yuko bize Ikulu akipiga kazi kama ilivyo slogan yake "hapa kazi tu".
Kama mwananchi wake namshauri katika hizo kazi anazochapa basi aivunje Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto. Hii wizara ni kubwa mno.
Napendekeza, kutokana na unyeti wa suala la Afya, Afya ibaki peke yake na Waziri wake. Hayo mengine yabaki kama Wizara ya Jamii.
Popote duniani wizara ya Afya ni sekta nyeti mno. Vita hii ya Covid-19 imethibitisha unyeti wa wizara hii. Ni vigumu yule mama kujigawa kushughulika na afya na hapo hapo ashughulike ni wazee, kina mama na watoto. Tunaweza kuona alivyofeli kuongoza wizara hii lakini kimsingi ni ukubwa na upana wake.
Hizo kazi unazochapa Ikulu, chapa na hili. Ahsante.
Au nasema uongo ndugu zangu!