Rais Magufuli awakabidhi waislamu mchango wa fedha za ujenzi wa msikiti, Shekhe wa Wilaya amshukuru

Hao waliomshauri rais mpaka kufukiza hatua ya kujenga msikiti hapo Chamwino ni waislam kama wewe sasa usijidai wewe kuwa unaujua uislam kuliko wao.

Wasaidizi wa karibu kabisa wa Rais ni waislam na wanayo haki ya kuswali wakiwa eneo Lao la kazi.
Hivi aliekwambia hawana haki ya kuswali nani? Mbona unabadilika? Mara Ijumaa sahv tena umebadilika mara kuswali, usiwe kinyonga! Nimekuuliza unazijua sharti za kuswali Ijumaa unakuja na hoja nyingine, acha kujifanya unaujua Uislam, waachie wenyewe waislam.
كلب واحد!
 
Hivi aliekwambia hawana haki ya kuswali nani? Mbona unabadilika? Mara Ijumaa sahv tena umebadilika mara kuswali, usiwe kinyonga! Nimekuuliza unazijua sharti za kuswali Ijumaa unakuja na hoja nyingine, acha kujifanya unaujua Uislam, waachie wenyewe waislam.
كلب واحد!
Sihitaji kujua sharti la kuswali ijumaa kwani maishani mwangu sitegemei kuja kuswali ijumaa.

Ninachokwambia ni logic ya kawaida tu ya hao wanaomsaidia rais kuwa na msikiti hapo Chamwino kama ambavyo kanisa lipo.

Waelewe waislam wenzako wengi wenye kuhitaji msikiti, mengineyo unayoongea ni mbwembwe tu zisizo na kichwa wala miguu.
 
shs ngapi zilizokabidhiwa mbona mtoa taarifa hasemi ,basi ni majungu .Taja kiwango na weka picha mtu ana pokea.
 
Waislamu wanajidharirisha sana yaani kanisa limepewa kazi ya kujenga msikiti hivi wanajielewa kweli hawa watu? Je Yale mafundisho wa mtume s.a.w wanayaelewa kweli au ndio lugha ya kiarabu imewafanya kukariri tu bila kureason

NAUSIKITIKIA UMMA WA KIISLAMU kama viongozi hawata paza sauti juu ya hili IPO siku nguruwe atauzwa msikitini na waislamu watamuogopa huyu mungu mtu
Kwa hili hakuna ubaya ni vile wa tz wengi exposure ni zero,kwa sie tulioishi nchi za kiarabu wala hatulishangai sana maana huko nako mjue yapo makanisa na kuna waarabu wakristu...
Nakumbuka mfalme wa Oman hayati Quabos miaka ya 2000 hapo alijenga kanisa na kulitia samani za gharama kubwa ndabi ili tu watu wake wote nchini mle tukiwemo sie ma expart tumwabudu mungu!
Ukaribu wa dini hizi ni mkubwa ukianzia Israel,Palestine,Iraq,Egypt,Siria,Lebanon...huko hutokea hata watu wa pande hizi mbili kuabudu pamoja
Kazi ipo kwetu huku kuanzia sudan kushuka chini
 
Kwa hili hakuna ubaya ni vile wa tz wengi exposure ni zero,kwa sie tulioishi nchi za kiarabu wala hatulishangai sana maana huko nako mjue yapo makanisa na kuna waarabu wakristu...
Nakumbuka mfalme wa Oman hayati Quabos miaka ya 2000 hapo alijenga kanisa na kulitia samani za gharama kubwa ndabi ili tu watu wake wote nchini mle tukiwemo sie ma expart tumwabudu mungu!
Ukaribu wa dini hizi ni mkubwa ukianzia Israel,Palestine,Iraq,Egypt,Siria,Lebanon...huko hutokea hata watu wa pande hizi mbili kuabudu pamoja
Kazi ipo kwetu huku kuanzia sudan kushuka chini
Walau wewe una hoja mkuu

Ila binafs sijapendezewa na hili la pesa kuchangishwa kanisani kama Rais angechukua fungu lake kutoka serikalini na s kuchangisha kanisani mkuu hizi n dharau pia kikanuni haipo sawa

Mfalme Qabous yeye alichukua pesa toka fungu la serikal ambayo hata wewe kama expert ulichangia pato la taifa hilo hvyo hakuna ubaya wowote
 
Rais Magufuli leo amekabidhi mchango wa fedha za ujenzi wa msikiti zilizochangishwa jana katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Immakulata.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwa Shekhe wa Wilaya Suleiman Matitu na Katibu wa Rais ndugu Ngusa.

Chanzo: East Africa Radio
WaTz tujiongeze, tunaleta taarifa hata haisemi ni wapi?!
 
Rais Magufuli leo amekabidhi mchango wa fedha za ujenzi wa msikiti zilizochangishwa jana katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Immakulata.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwa Shekhe wa Wilaya Suleiman Matitu na Katibu wa Rais ndugu Ngusa.

Chanzo: East Africa Radio
Hapa rais wetu moendwa alidobanga,but nia yake ni njema
 
Kwan kuna tatizo gani,mbona mambo mengine mnashirikiana na waislam,huyu ni rahisi wa wote lazima ahakikishe anaowatawala wawe na service wanzoziitaji.mtajuta sana mwaka huu
Mchango wa ujenzi wa msikiti ukachangwe kanisani?how!!!!

Sijaelewa....au mleta mada ni typing error?weka nyama kidogo!
 
Uanze usianze bado hauniongezei wala kunipunguzia kitu, imani inakaa ndani ya mtu na sala sio lazima kwenye jengo.
Unapoteza muda kutunza kinyongo ndani ya nafsi yako wakati huna uwezo wa kubadilisha chochote katika maamuzi yanayofanywa na mtu wa ngazi ya rais.
 
Unapoteza muda kutunza kinyongo ndani ya nafsi yako wakati huna uwezo wa kubadilisha chochote katika maamuzi yanayofanywa na mtu wa ngazi ya rais.
Unasema nini?
قَالَ: اتَّقِ اللَّهَ حَيْثُمَا كُنْتَ وأَتْبِعِ السَّيِّئَةَ الْحسنةَ تَمْحُهَا، وخَالقِ النَّاسَ بخُلُقٍ حَسَنٍ
 
Kwa hili hakuna ubaya ni vile wa tz wengi exposure ni zero,kwa sie tulioishi nchi za kiarabu wala hatulishangai sana maana huko nako mjue yapo makanisa na kuna waarabu wakristu...
Nakumbuka mfalme wa Oman hayati Quabos miaka ya 2000 hapo alijenga kanisa na kulitia samani za gharama kubwa ndabi ili tu watu wake wote nchini mle tukiwemo sie ma expart tumwabudu mungu!
Ukaribu wa dini hizi ni mkubwa ukianzia Israel,Palestine,Iraq,Egypt,Siria,Lebanon...huko hutokea hata watu wa pande hizi mbili kuabudu pamoja
Kazi ipo kwetu huku kuanzia sudan kushuka chini
Nafikiri kitu kisichoeleweka na kufanya watu wajiulize maswali bila kupata majibu ni kitu gani kinamvutia Rais, Mkristo, kujihusisha na ujenzi wa Misikiti? Mfalume wa Moroko alipotembelea Tanzania kitu cha kwanza Rais wetu mpendwa kuomba ulikuwa Msikiti ukifuatiwa na Uwanja wa Mpira. Watu wengi walijiuliza kama hayo mawili ndo yalikuwa matatizo ya kipaumbele kwa Tanzania, Msikiti umejengwa na Uwanja unajengwa Chato, hakuna tatizo. Kitu kisicho cha kawaida alichofanya Rais, labda kwa utashi wake, ni kukusanya pesa kanisani na kukabithi kwa Waislam kujenga Msikiti bila ombi rasmi toka uongozi wa Wahitaji kwenda kwa Wafadhili. Hata maisha ya kila siku Mhitaji hupeleka ombi la msaada wowote kwa jirani ili atatue matatizo yake siyo jirani aone Mhitaji anahitaji nyama akapelekewa ya nguruwe kumbe jirani ni Muislam atatupa. Baada ya uongozi wa Msikiti jirani kuona umuhimu wa kujenga Msikiti mwingine mkubwa zaidi lakini watahitaji pesa zaidi kukamilisha kazi hiyo kwa hiyo wataomba msaada toka kwa waumini na majirani ikiwa ni pamoja na Makanisa ya karibi. Baada ya kupata ombi, kanisa lingeitisha harambee siku Rais yupo kanisani hata ateuliwe kuwa MC ili mchango uwe mkubwa ikiwa ni pamoja na toka Serikalinim.
 
Back
Top Bottom