Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Mkuu mbona uantoa hukumu na huku ukisema wazi kuwa hunauhakika kama ziara ni chama au serikali, labda ungethibitisha hilo kwanza kabla ya kutoa hukumu au?

Filed hii kitu kinanichanganya sana... naona uelewa wa utawala wa sheria na civic education ya hawa watu haijatulia!!!!! tunaonekana wajinga tunavyozidi kukaa kimya... wewe unasemaje kuhusu hili?
 
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda jana alikuwa na wakati mgumu bungeni wakati alipobanwa na wabunge kwa kutumia fedha za walipa kodi kufanya shughuli za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kulazimika kukiri kutumia ziara za serikali kwa shughuli za chama hicho tawala.

Hiyo ilitokea wakati kipindi cha maswali ya papo kwa papo ambacho wabunge hupata nafasi ya kumuuliza waziri mkuu, ambaye ni mkuu wa shughuli za serikali bungeni kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu utendaji wa serikali.

Aliyeanzisha sakata hilo alikuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe aliyehoji sababu za Waziri Pinda kutumia ziara ambayo iligharamiwa na fedha za walipa kodi ambao ni Watanzania wote, kufanya shughuli za kugawa kadi kwa wanachama wapya wanaojiunga na CCM.

Katika swali lake la msingi na la nyongeza, Zitto alisema katika kipindi chake chote cha uongozi, Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa, hakuwahi kutumia ziara za kiserikali kufanya shughuli za chama kama hiyo ya kugawa kadi za wanachama wapya wa chama chake.

“Mheshimiwa, katika kipindi kifupi cha kuwa waziri mkuu, umetumia ziara zako za kiserikali kufanya kazi za chama… unapofanya ziara hizi unatumia fedha zetu za wanachama wa Chadema, CUF, CCM na vyama vingine,” alisema Kabwe.

Mbunge huyo, ambaye pia ni waziri kivuli wa Wizara ya Miundombinu, alimtaka Waziri Mkuu kueleza kama kuanzia sasa hatatumia ziara za kiserikali kufanya shughuli za CCM.

Ingawa Kabwe hakufafanua maeneo ambayo waziri mkuu alichanganya shughuli hizo, mojawapo ya sehemu alizochanganya mambo ni katika ziara yake wilayani Siha mkoani Kilimanjaro ambako alipokea wanachama wapya zaidi ya 1,000 baadhi yao wakitokea Chadema.

Akijibu swali hilo, Waziri Pinda alijitetea kuwa ni vigumu kutofautisha shughuli hizo mbili, hasa ikizingatiwa kuwa yeye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM.

Kwanza Pinda alianza kwa kusema hakumbuki kama waziri mkuu aliyemtangulia, Lowassa alikuwa hafanyi hivyo ingawa akaongeza kuwa kuna uwezekano kukawa na ukweli katika hoja ya mbunge huyo machachari wa upinzani.

”Unalolisema linaweza kuwa na ukweli,, lakini haya ni mambo yanayojitokeza wakati mwingine hata hujui kwa sababu yanaandaliwa huko mikoani... sasa unaombwa na wakati mwingine unashindwa kukataa kwa sababu ya mazingira,” alisema waziri huyo wa zamani wa Tamisemi.

Huku akipigiwa chapuo na baadhi ya wabunge wa CCM, Pinda alisema huko mikoani pia anakwenda kufuatilia utekelezaji wa ilani ya CCM na kwamba chama kilichopo madarakani ni CCM hivyo ni mambo ambayo ni vigumu kuyatenganisha.

“Lakini, hivi kweli Mheshimiwa Kabwe unaacha kuona shughuli kubwa ya kukagua miradi ya maendeleo ya wananchi unaona tatizo kubwa ni kupokea kadi za wanachama 10 tu,” alihoji Waziri Pinda na kuwaacha baadhi ya wabunge wakitabasamu.

Manung’uniko ya waziri mkuu kutumia rasilimali za serikali kuimarisha CCM, ikiwa ni pamoja na magari ya serikali, ziliwahi kumkumba waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye mwaka 2000 akiwa katika ziara ya kiserikali katika mkoa wa Kilimanjaro.

Mara ya kwanza ilitokea wakati Sumaye alipozindua tawi jipya la wakereketwa la Temba Watch katikati ya mji wa Moshi na kuwataka wafanyabiashara ambao wanataka mambo yawanyookee, wajiunge na CCM.

Mara ya pili ilikuwa ni katika mkutano mkuu wa wadau wa zao la kahawa mkoani Kilimanjaro, ambako mara baada ya kufungua mkutano huo alikwenda kufungua matawi ya wakereketwa licha ya ratiba kuonyesha kuwa alitakiwa ashiriki mkutano huo.

Mwingine aliyechangia kumchachafya Waziri Pinda alikuwa mbunge wa Chambani kwa tiketi ya CUF, Salim Hemed Khamis aliyehoji sababu zinazoifanya Zanzibar isiruhusiwe kuwa mwanachama kamili wa Shirikisho la Afrika Mashariki (EAC).

Khamisi alisema kabla ya kuvunjika kwake, EAC iliundwa na nchi nne ambazo ni Uganda, Kenya, Tanzania na Zanzibar, lakini baada ya kuanza kwa mchakato wa kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki, Zanzibar haimo na akahoji kama itakuwa hasara kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuiacha Zanzibar kuingia kwenye jumuiya hiyo mpya.

Akijibu swali hilo, Waziri Pinda alikiri kuwa kabla ya kuvunjwa kwa jumuiya hiyo, Zanzibar ilikuwa mwanachama, lakini wakati jumuiya hiyo mpya inarejea, Tanzania ilirejea kwa sura tofauti kwa sababu tayari ilikuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbunge huyo alionekana kutoridhishwa na jibu hilo na kuuliza swali la nyongeza akihoji kama serikali itakuwa tayari kuiruhusu Zanzibar kujiunga na jumuiya hiyo endapo itaombwa, ikizingatiwa kuwa nchi nyingine wanachama wa EAC hazina pingamizi.

“Kwa kuwa hakuna pingamizi kutoka nchi nyingine wanachama, je serikali itakubali ombi la Zanzibar kujiunga na jumuiya hii kama itaombwa au itatukatalia kama ilivyofanya kwa Fifa (shirikisho la kimataifa la soka),” alihoji mbunge huyo.

Waziri mkuu alisema si jukumu la nchi nyingine kuiamulia Tanzania mfumo gani wa kujiunga na kwamba, kwa kuwa Zanzibar na Tanganyika zinakubali kuwa ni nchi moja, haoni sababu kwa nini Tanzania irudishwe nyuma katika suala hilo.

Naye mbunge wa Mtera, John Samwel Malecela aliiomba serikali kuangalia uwezekano wa kukasimu madaraka yake ya uandikishaji vijiji na ugawaji wa kata kwa Halmashauri na ofisi za wakuu wa mikoa ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa suala hilo.

Akijibu maswali hayo, waziri Mkuu alisema uandikishwaji wa vijiji na ugawaji wa kata mpya ni mambo yanayokwenda sambamba na matumizi ya fedha, hivyo suala hilo bado litaendelea kubakia serikali kuu kwa lengo la kuangalia bajeti kama inaruhusu.

Waziri mkuu alisema utaratibu wa sasa hauna matatizo yoyote kwani baadhi ya matatizo yapo kwa Halmashauri ambazo zimekuwa zikipitisha maombi hayo, lakini mengi ya maombi hayo yanakuwa hayajakidhi vigezo vilivyoainishwa.

Mathalani, waziri mkuu alisema kati ya maombi ya vijiji vipya 225 nchi nzima, ni maombi 42 tu ndio ambayo yamekidhi vigezo hivyo na kwamba suala hilo bado litaendelea kuamuliwa na Serikali kuu ikiwa ni pamoja na kujiridhisha kuwepo kwa bajeti ya kazi hiyo.
 
Hata kwenye mikutano ya hadhara ya serikali wana-ccm, wakiwa katika mavazi yao ya kijani, hujipanga na kufanya kazi ya polisi ya kupanga watu kwenye mikutano hiyo. Huenda gharama za shughuli hiyo hulipwa na kodi za wananchi. Nafikiri ni vyema kutengaanisha shughuli za chama na za serikali. Ziara za kiserikali ziwe za kiserikali na za chama ziwe za chama. "After all" chama chenyewe kimejichokea na kilishapoteza busara zote.
 
Hakuna tofauti kati ya shughuli za serikali na chama katika nchi hii. Haya yamekuwa yakitendeka kwa enzi. Inakuwaje CCM wanakuwa wanamiliki maeneo kadha ya kadha ambayo yalitolewa na wananchi kwa ajili ya shughuli za nchi miaka ile ya Ujamaa?

Mara kwa mara, magari ya serikali yanaonekana yakifanya kazi za chama. Inauma lakini maadamu mimi mnyonge na sina cha kufanya, acha tu niumie kivyanguvyangu.
 
Hii itabidi iwe thread ya kukeep count on JK's trips za 2008 maana mwaka jana tulishindwa kuweka count hivyo wengine tukakosa hoja. Mwisho wa 2008 kama tutakuwa wazima tutajua safari vipi zilikuwa na ulazima na zipi siyo za muhimu

Evaluation yetu itaangalia msafara wake huwa anachukua watu wangapi

Anafikia hoteli gani

Emuhimu wa hiyo safari

Estimation ya gharama za kila safari

Gharama ambazo ubalozi husika huzipata

KISHA

tutaoanisha na repoti ya PUBLIC ACCOUNTS COMMETEE

na auditing reports za Foreign na Ikulu

kisha tutajua kama IKULU iko fot for purpose

sioni sababu gani hili lisiwezekane afterall wana JF mnajua itinerary ya JK ya mwezi ujao kabla hata hao watu wake ikulu hawajaijua


Mwaka unakaribia kuisha hebu tupe mahesabu mpaka sasa

Asha
 
600 million madafu in one trip, sasa akifanya trip 10 kwa mwaka? si tosha kulipia wanafunzi wote wa vyuo vikuu Tanzania?


Hivi ni nani anahusika kupanga gharama za ziara za Raisi?Maanake ni kama sielewi elewi?
 
Vasco da gama anapaa lini tena?

Sitashangaa nikisikia anaingia USA in January 2009 ili kuhudhuria uapishwaji wa Rais-mteule Obama, whether amealikwa au hakualikwa. Huyu Kiwete halitakii mema Taifa letu.
 
JAMANI eeh, nini tulichovuna toka Mwalimu alipoanza kutumia nusu ya bajeti yetu ili kukamilisha ndoto yake kwamba Tanzania haitakuwa huru mpaka Afrika nzima itakapokuwa huru.

Ninadhani siasa yetu ya nje ina walakini. Tukubaliane kwanza kwamba siasa za nje lazima kuwa na maslahi kwa Watanzania (na sio viongozi wao na waunga misafara tu!).

Mimi nisingelikuwa na tatizo kama wanajeshi wetu ndio wangelikuwa wamesafiri kwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenda kuweka amani huku lakini kutuletea pia sehemu ya utajiri wa huko.

Lakini kwa hizi safari nyingine mimi naona ni ulaji kwa waliomo kwenye serikali na angalia magari yao ya kifahari na nyumba wanazoporomosha hao wanaokuwa katika msafara wa rais, makamu wake na sijui kama Bw. Pinda keshatoka nje toka aingie madarakani???
 
Sitashangaa nikisikia anaingia USA in January 2009 ili kuhudhuria uapishwaji wa Rais-mteule Obama, whether amealikwa au hakualikwa. Huyu Kiwete halitakii mema Taifa letu.

I hear he is good when it comes to party crashing!
 
Ile Ziara ya Mkuu wa kaya huko America ya kusini na baadaye US imeahirishwa,Ifuatayo chini ni Taarifa kutoka Adis Ababa inayoripoti kuahirishwa kwa Mkutano wa Marais wa Africa na wenzao wa America ya kusini.


African Union / The second Africa-South America Summit postponed
ADDIS ABABA, Ethiopia, October 30, 2008/African Press Organization (APO)/ - The Chairperson of the Commission wishes to announce that, after consultation with the African Union, the Government of the Bolivarian Republic of Venezuela has postponed the second Africa-South America Summit scheduled to take place in that country from 24 to 29 November 2008.

The postponement is at the request of a number of African Leaders who would like to participate in the Follow-up International Conference on Finalizing for Development being organized by the United Nations in Doha, Qatar and which is to take place from 29 November to 2
December 2008.

Although the exact dates for the Summit will be determined after due consultation with all parties concerned, it is expected that it will now take place within the 1st quarter of 2009.


The Government of the Bolivarian Republic of Venezuela and the Commission regret any inconvenience the postponement might have caused but consider that it is for a good cause. They hope that the pace of preparations will continue so as to ensure a successful Summit in 2009.

SOURCE : African Union Commission (AUC)
 
Mkuu Mwawado asante.. naona unachosema ni kuwa vyovyote vile bado wiki hiyo atakuwa nje ya nchi.. jamani nani ana namba ya Itatiro
 
Vasco da gama anapaa lini tena?

Mnamsema sana siku hizi, kaamua kuuchuna Dar ili kutuliza mawimbi ndani ya chama. Atapaa tena si muda mrefu kwenda mashariki ya Kati kwenye shopingi oops samahani "mikutano".
 
N i kweli inavyoonekana hatakuwepo nchini wiki ijayo Mzee Mwanakijiji.Taaria niliyonayo ni kwamba atakwenda Addis Ababa Ethiopia na baada ya hapo ataelekee Libya,.Yetu macho tusubiri wadanganyika
 
Vasco da gama anapaa lini tena?


...mwekeeni kiwete wetu kile kibao cha ..king kiki double o ochestra..."mimi msafiri bado nipo njiani......sijui lini nitafikaa..naulizia watu kule ninakoenda..sijui lini nitafika ...naambiwa bado ni mbali...sijui lini nitafikaaaaaaaaaaaaaa"

katika mambo ambayo rais wetu ni hodari ni safari....na kuhudhuria misiba.....hata kama itabidi kuaga mara tatu kwenye mikoa tofauti...atapenda aonekane kote...badala ya kuchagua kuonekana sehemu moja ya hizo........nahisi kwamba kuhudhuria misibani ni sehemu ya siasa......na hawa marais waliompa ukuu wa AU ...kweli wamempatia..........na WAMETUWEZA...maana hakosi sababu!!!
 
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini leo,
Jumanne, Novemba 18, 2008 kwenda Libya na Ethiopia kwa ziara fupi za kikazi.

Nchini Libya, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na kiongozi wa nchi hiyo,
Kanali Mummar Gaddafi juu ya jitihada za kupatanisha mgogoro kati ya nchi za Chad na
Sudan.

Libya pamoja na Congo (Brazzaville) ziliombwa na AU kuzipatanisha nchi jirani za
Chad na Sudan ambazo uhusiano wao umekuwa siyo mzuri kwa muda sasa. Nchi hizo mbili
zimekuwa na mzozo wa kisiasa unaotokana kwa upande mmoja na vita ya Darfur, lakini
pia kutokana na kila moja ya nchi hizo kumtuhumu mwenzake kwa madai ya kusaidia
waasi wa nchi nyingine.

Rais Kikwete ataondoka Libya kwenda Addis Ababa, Ethopia kuhudhuria Mkutano wa Pili
wa Kamisheni ya Afrika Kuhusu Ajira kwa Vijana iliyoanzishwa na Waziri Mkuu wa
Denmark, Bw. Fogh Ramussen. Waziri Mkuu huyo alimwomba Rais Kikwete kuwa mjumbe wa
Kamisheni hiyo inayoshughulikia masuala hayo ya ajira kwa vijana barani Afrika.

Mheshimiwa Rais alikubali kuwa mjumbe wa Kamisheni hiyo ambayo pia mwenyekiti wake
ni Mheshimiwa Rasmussen mwenyewe.

Imetolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano
Ikulu.
Dar es Salaam.
18/11/2008




Mail From Ikulu.go.tz
 
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini leo,
Jumanne, Novemba 18, 2008 kwenda Libya na Ethiopia kwa ziara fupi za kikazi.

Nchini Libya, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na kiongozi wa nchi hiyo,
Kanali Mummar Gaddafi juu ya jitihada za kupatanisha mgogoro kati ya nchi za Chad na
Sudan.

Libya pamoja na Congo (Brazzaville) ziliombwa na AU kuzipatanisha nchi jirani za
Chad na Sudan ambazo uhusiano wao umekuwa siyo mzuri kwa muda sasa. Nchi hizo mbili
zimekuwa na mzozo wa kisiasa unaotokana kwa upande mmoja na vita ya Darfur, lakini
pia kutokana na kila moja ya nchi hizo kumtuhumu mwenzake kwa madai ya kusaidia
waasi wa nchi nyingine.

Rais Kikwete ataondoka Libya kwenda Addis Ababa, Ethopia kuhudhuria Mkutano wa Pili
wa Kamisheni ya Afrika Kuhusu Ajira kwa Vijana iliyoanzishwa na Waziri Mkuu wa
Denmark, Bw. Fogh Ramussen. Waziri Mkuu huyo alimwomba Rais Kikwete kuwa mjumbe wa
Kamisheni hiyo inayoshughulikia masuala hayo ya ajira kwa vijana barani Afrika.

Mheshimiwa Rais alikubali kuwa mjumbe wa Kamisheni hiyo ambayo pia mwenyekiti wake
ni Mheshimiwa Rasmussen mwenyewe.

Imetolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano
Ikulu.
Dar es Salaam.
18/11/2008




Mail From Ikulu.go.tz

Kuna wakati niliomba kwa mods kuwa hii thread iwe "sticky", naona ombi langu halijafanyiwa kazi.
Hope ujumbe umefika.
 
Ndugu zangu, lini AU chairmanship inakwisha?? I'm tired of this nonsense which bleeds our coffers money that can be used to build schools. Safari haziishi kisa AU.

JK ebu tulia mjini utafute ufumbuzi wa umaskini.

Can't U see President elect Obama toka asubuhi mpaka jioni yuko Chicago tu anasoma vitabu na kudiscuss namna ya kusolve matatizo, wewe kutwa hewani.
 
Back
Top Bottom