Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Imebidi niulize hili swali. Jamani JK ni raisi au bado waziri wa mambo ya nje? Inavyo onekana jamaa yupo more interested in public relations na mahusiano yake na viongozi wa nje badala ya yanayo tokea nchini kwake. Ana safiri kuliko hata Membe aliye muweka kushugulikia mambo ya nje. Inaelekea ali faidi kweli uwaziri wa mambo ya nje mpaka leo hii anaona aendelee.

Ina sikitisha mambo yote haya yanaendelea nchini lakini kiongozi wa taifa hamalizi wiki kashaenda nje. Hata Obama anaye ongoza taifa kubwa ali subiri miezi kadhaa kabla ya kusafiri kwenda nchi za nje na hiyo ilikuwa kuhudhuria mkutano wa G20 na siyo kutalii kama JK anavyo fanya. Hizo safari za kila siku nje ana sema nazo zina manufaa kwa taifa lakini bado hatuja ona manufaa yake. Ni kama vile ana taka kushindana umaarufu na viongozi wa magharibi na kutaka kuonekana kwenye vyombo ya habari vya kimataifa.

Raisi yoyote jukumu lako la kwanza na wajibu wako wa kwanza ni kwa wananchi walio kuchagua. Jukumu la JK ni kwa watanzania milioni 40 wanao tegemea kuongozwa. Lakini inavyo onekana JK ana priorities zingine. ALi kimbilia kuchukua uwenyekiti wa AU wakati wizara yenyewe ya mambo ya nje ilikua haina bajeti ya kutosha kufanya hivyo. Aka chukua uwenyekiti AU wakati taifa lilikua lina hitaji ajikite zaidi kwenye home affairs.

Kikatiba raisi ni raisi akiwa ndani ya nchi yake. Akisha ondoka na kuvuka mipaka ana achia asilimia kubwa ya nguvu alizo nazo kwa anaye mfuatia kwa cheo. Raisi akiondoka kutoka ardhi ya Tanzania nchi inakua na raisi mwingine temporarily hata kama hamtangaziwi fulani ata chukua majukumu ya raisi kwa muda fulani. Sasa kama JK mara nyingi hayupo nchini si sahihi kusema kuwa watanzania hatuongozwi na JK bali watu waliyo chini yake? Je si sahihi kusema raisi anakua mzivu na kuacha kazi ambazo alipaswa kufanya yeye kwa wengine?

Wamarekani wana kifurushi fulani sikumbuki jina vzuri nadhani wanaiita "football" ambalo hubebwa na mwanajeshi kila raisi anapo enda. Hiko kifurushi kina msaidia raisi kuendesha nchi hata awe nje ya nchi. Kifurushi hiki kina mrufusu kutoa maamuzi yoyote hata akiwa ndani ya dege la Air Force. Hata Warusi wana kitu kama hicho. Ninacho jaribu kuonyesha hapa ni kwamba hata wenzetu wanajua nguvu za raisi ni akiwa nchini kwake ndiyo maana wakawa na kitu kama hicho ili kum saidia raisi walau kutoa maamuzi akiwa hayupo nchini. Tanzania tuna kitu kama hicho? SIDHANI!

Inavyo onekana sasa kazi kubwa ya Jk aliyo fanya tokea aingie madarakani ni kuteua tu watu katika nafasi mbali mbali. Akijiuzulu huyu akistaafu yule basi yeye ana chagua na kuapisha huyo anachukua bakuli lake na kwenda zake nje.

Sioni ubaya JK akaachia baadhi ya safari aende waziri wake wa mambo ya nje au manaibu wake. Si kawa teua kwa ajili hiyo? Sasa kwa nini ana fanya kazi zao zote? Hata Makamu wa raisi anaweza kwenda kwenye baadhi ya mambo kama kuna hitajika cheo kikubwa zaidi ya waziri. Kuna safari amabazo ndiyo ni lazima mkuu atu wakilishe lakini siyo zote Kuna mikutano ya kimataifa ambayo ni vuzuri akaenda mkuu wa nchi lakini siyo zote.

JK tulia nyumbani. Nyumba ina waka moto baba mwenye nyumba kila siku una kimbia kwenda kuomba msaada badala ya kuchota maji uzime moto. Tume kuchagua kama raisi wetu siyo waziri ya mambo ya nje.

Kwa anayeona nimemuonea JK sawa lakini haya ni maoni yangu mimi.
 
Labda anataka avunje record ya kusafiri nje ya papa John Paul wa Pili.
 
Labda anataka avunje record ya kusafiri nje ya papa John Paul wa Pili.

Unasema ukweli mwana. Lakini anabidi atambue papa alikaa kwenye upapa kwa takriban miak 25 sasa yeye anatak kuivunja hiyo rekodi ndani ya miaka mitano. Pili wakatoliki duniani ni billioni moja which means sadaka zinaingiza hela nyingi zaidi Tz watu milioni 40.
 
Nimejiuliza mara nyingi kazi ya Membe ni nini? Kama ni kupenda trips si the guy was once a foreign minister so he's probably been to most of these places already? Washauri wake ni naniiiii?
 
Nimejiuliza mara nyingi kazi ya Membe ni nini? Kama ni kupenda trips si the guy was once a foreign minister so he's probably been to most of these places already? Washauri wake ni naniiiii?

Ndiyo cha ajabu hicho. Mtu alisha kua waziri wa mambo ya nje ila ni kama vile "ushamba" wa kusafiri bado hauja mtoka. Huyu Membe nadhani sasa ni care taker to wa ile wizara ionekane ina mtu. Sana sana asafiri na JK.
 
Ndiyo maana mafisadi wanaendesha nchi maana aliye takiwa kuwa kemea kila siku yupo angani.
 
Mazee MwanaFalsafa1 kile kifurushi ama football kina codes zinazomuwezesha Rais kuidhinisha Nuclear Attacks incase of an attack, ndio njia yake ya kuweza kuwasiliana na Central Command ili watu waanze shughuli nzito.

Wakati JK utakuta vi-football vyake ni totoz tu za kumwaga teh teh teh.
 
Matatizo ya viongozi wetu ukiyafuatilia sana yatakupa kichaa.

labda tukubali yaishe.
 
Mazee MwanaFalsafa1 kile kifurushi ama football kina codes zinazomuwezesha Rais kuidhinisha Nuclear Attacks incase of an attack, ndio njia yake ya kuweza kuwasiliana na Central Command ili watu waanze shughuli nzito.

Wakati JK utakuta vi-football vyake ni totoz tu za kumwaga teh teh teh.

Ni kweli ile football ni kuwasiliana na central command which means bado ana uwezo wa kufanya maamuzi fulani akiwa nje au huko angani. Nilionaga documentary ya hicho kifurushi siku moja kwenye History Channel. Sasa sijui mwenzetu JK kama ndege hata ina simu hahaha maana ndege yenyewe ime nunuliwa kifisadi hahaha.
 
Matatizo ya viongozi wetu ukiyafuatilia sana yatakupa kichaa.

labda tukubali yaishe.

Ni kweli matatizo ya viongozi yana umiza kichwa ila usipo yaongelea ndiyo matatizo yanazidi nchini. Watanzania tume nyamaza kwa muda gani na ona ukimywa ulipo tufikisha sasa hivi.
 
Nimejiuliza mara nyingi kazi ya Membe ni nini? Kama ni kupenda trips si the guy was once a foreign minister so he's probably been to most of these places already? Washauri wake ni naniiiii?

Nyani ngabu alisema huyu mkuu anatakiwa kufokewa akae nyumbani kwake. Mi nadhani hili likifanywa na Obama pia wakati akienda kumtembelea labda ataona aibu. Maana watu anaowatembelea wakimkoromea kuwa anafuja pesa kwa safari zisizo mhimu kwake huenda akaona aibu japo hana soni mkwere huyu
 
Nyani ngabu alisema huyu mkuu anatakiwa kufokewa akae nyumbani kwake. Mi nadhani hili likifanywa na Obama pia wakati akienda kumtembelea labda ataona aibu. Maana watu anaowatembelea wakimkoromea kuwa anafuja pesa kwa safari zisizo mhimu kwake huenda akaona aibu japo hana soni mkwere huyu

Washaona ana jipendekeza sasa. Nadhani huyu mtu shida yake umaarufu na kutaka kuonekana. Sijui ndiyo kutaka kuwa "Obama" wa Afrika hata sielewi.
 
WAKATI haya yakiendelea, kuna habari kwamba JK amesafiri tena, hata akashindwa kumzika rafiki yake mkubwa, Sheikh Suleiman Gorogosi na hakika atashindwa kumzika Prof Haroub Othman.


Bajeti ya safari za Kikwete nje yapaa

bul2.gif
Vinywaji, vitafunio Ikulu Sh. mil 201

bul2.gif
Pesa za mavazi, mashuka na viatu zabanwa


Juni 24, 2009
Mwandishi Wetu, Dodoma

MCHANGANUO wa mgao wa fedha katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2009/2010 unaonyesha kuwa Ikulu imetengewa Shilingi milioni 115 kwa ajili ya safari za nje ikilinganishwa na Sh. mil 82 ilizotengewa kipindi kilichopita.
Hiyo maana yake ni kwamba, bajeti ya safari za nje za Ikulu imeongezeka kwa takriban Sh. milioni 34.

Bajeti ya Ikulu ya safari za ndani ya nchi nayo imeongezeka kutoka Sh. 608,419,000 kwa bajeti ya mwaka 2008/2009 hadi Sh 723,360,000 kwa mwaka 2009/2010, ikiwa ni ongezeko la Sh. milioni 114.9.

Miongoni mwa mambo ambayo Rais Kikwete amekuwa akishutumiwa nayo na wananchi, ni wingi wa safari zake za nje ambapo inadaiwa kwamba zinachota mapesa mengi ya walipakodi; ilhali manufaa yake hayaonekani wazi.

Rais Kikwete ameingia katika rekodi ya kuwa rais wa kwanza wa Tanzania kusafiri mara nyingi kwenda Marekani katika kipindi kifupi tu cha utawala wake. Mpaka sasa ameshakwenda Marekani mara sita. Aidha ni nadra kumaliza mwezi mmoja bila kufanya safari ya nje; huku wananchi wakilalamika pia kwamba msafara wake mara nyingi unakuwa mkubwa.

Wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Nje na na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliliambia Bunge kwamba serikali inaangalia uwezekano wa kupunguza idadi ya watu wanaosafiri na viongozi wa juu kwenda nje ya nchi baada ya kupata maelekezo kwa Rais Kikwete mwenyewe, jambo linalodhihirisha ujumbe kumfikia.

Mchanganuo unaonyesha pia kwamba bajeti ya Ikulu kwa ajili ya ununuzi wa mavazi, mashuka na viatu, imepunguzwa kutoka Sh. milioni 127,400,000 kwa mwaka wa fedha 2008/2009 hadi Sh. 116,400,000 mwaka wa fedha wa 2009/2010, ikiwa ni punguzo la Sh. milion 11.

Lakini Ikulu imeongezewa takriban Sh. milioni 201.6 katika bajeti yake ndogo ya vinywaji, vitafunio na huduma nyingine za malazi (hospitality supplies and services), ikilinganishwa na bajeti inayokwisha ya mwaka 2008/2009 kwa upande wa masuala ya utawala.

Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2008/2009, Ikulu ilipangiwa kutumia Sh 242,710,000 kwa ajili ya vinywaji na huduma nyingine za namna hiyo, lakini katika bajeti ya safari hii, yaani 2009/2010, imetengewa Sh 444,350,000 za huduma hizo.

Kwa mujibu wa mchanganuo wa Bajeti Kuu ya Serikali, matumizi katika kipengele hicho yanaonyesha kuongezeka kila mwaka wa bajeti, kuanzia mwaka wa fedha 2007/2008, ambapo matumizi halisi yalikuwa Sh. milioni 190.44, ikiwa ni ongezeko la Sh milioni 51.3.

Hali ni tofauti kidogo kwa Makamu wa Rais ambako gharama kwa ajili ya ununuzi wa mavazi, mashuka na viatu ni Sh 30,296,000, ikiwa kuna ongezeko ikilinganishwa na mwaka jana, ambako Sh. 22,840,000 zilitengwa. Hapa ni ongezeko la Sh. milioni 7.5 hivi.

Kwenye safari za ndani pia fungu la fedha limeongezwa na katika mwaka huu zimepangwa kutumika Sh. 344,200,000, ikilinganishwa na mwaka jana ambapo zilitengwa Sh. 256,970,000, ikiwa ni ongezeko la takriban Sh. milioni 87.2.

Safari za nje ya nchi za Makamu wa Rais zimetengewa Sh. milioni 25, tofauti na mwaka unaokwisha wa bajeti ambao zilitengwa Sh. milioni 2 ikiwa ni ongezeko la Sh. milioni 23.

Kwa upande wa bajeti ya Makamu wa Rais kuhusu vinywaji na vitafunio, zimetengwa kutumika Sh. milioni 214, ikiwa kuna ongezeko kwa kulinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha unaokwisha ambayo ni Sh. milioni 137, hapa kukiwa na ongezeko la Sh. milioni 77.

Wakati takwimu hizo zikiwa kwa ajili ya Makamu wa Rais, kwa upande wa ofisi yake (Ofisi ya Makamu wa Rais) fedha zilizotengwa kwa ajili ya vinywaji baridi na moto, chai na vitafunio, ni Sh. milioni 12.5, tofauti na mwaka jana ambako hapakuwa na bajeti ya aina hiyo.

Maofisa katika ofisi hiyo wamepangiwa kutumia Sh 331,270,000 kwa ajili ya safari za nchini, fedha ambazo ni zaidi ya walizopangiwa mwaka uliopita Sh. 273,215,000, kukiwa na nyongeza ya kitita cha Sh. milioni 58.

Lakini wakati hesabu zikiwa hivyo kwa ajili ya safari za ndani, mambo ni tofauti kwa upande wa safari za nje za maofisa wa ofisi hiyo zikiwa zimepangwa kutumika Sh. milioni 331, ikiwa ni tofauti ya Sh. 270,000 na kiasi kilichotengwa kwa ajili ya safari za ndani ya nchini, lakini pia ni kiasi kikubwa zaidi kwa kulinganisha na fedha zilizotengwa kwa ajili ya shughuli hiyo kwa mwaka jana ambazo ni takriban Sh. milioni 145.6.

Kwenye mavazi (mfano sare), viatu na mashuka zimetengwa Sh milioni 37.5, ikilinganishwa na Sh milioni tano za mwaka uliokwisha.

Kwa Waziri Mkuu, safari za ndani ya nchi zimepangwa kutumika Sh. milioni 636.6 ikiwa ni pungufu ya kiasi kilichotengwa mwaka jana ambacho ni Sh. milioni 842.34, kukiwa na upungufu wa Sh. milioni 205.7.

Kwa ufupi, Ikulu ni moja ya taasisi za serikali zilizoongezewa fedha za matumizi kama ya vinywaji na vitafunio, mambo ambayo yanapingwa na baadhi ya wabunge.

Wabunge hao wanaopinga ni pamoja na wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa ambaye aliliambia bunge, juzi jioni, kuwa matumizi hayo si kipaumbele cha matatizo mengi yanayoikabili nchi kwa sasa, kauli ambayo ilipata upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa CCM.

Spika wa Bunge Samuel Sitta, aliingilia kati kwa kuwataka wabunge wenzake wa CCM kumuacha Dk. Slaa aendelee kutoa maoni yake na kwamba ana haki ya kufanya hivyo na hakuwa amevunja kanuni yoyote hadi hapo Bunge litakapokaa kama kamati kupitisha vifungu vya bajeti hiyo.

Kwa ujumla Ikulu imepangiwa matumizi ya Sh. bilioni 7.23 katika bajeti iliyopitishwa na bunge wiki iliyopita itakayoanza kutumika Julai mosi hadi Juni 30 mwakani.



Source: Bajeti ya safari za Kikwete nje yapaa
 
WAKATI haya yakiendelea, kuna habari kwamba JK amesafiri tena, hata akashindwa kumzika rafiki yake mkubwa, Sheikh Suleiman Gorogosi na hakika atashindwa kumzika Prof Haroub Othman.


Bajeti ya safari za Kikwete nje yapaa

bul2.gif
Vinywaji, vitafunio Ikulu Sh. mil 201


bul2.gif
Pesa za mavazi, mashuka na viatu zabanwa


Juni 24, 2009
Mwandishi Wetu, Dodoma

MCHANGANUO wa mgao wa fedha katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2009/2010 unaonyesha kuwa Ikulu imetengewa Shilingi milioni 115 kwa ajili ya safari za nje ikilinganishwa na Sh. mil 82 ilizotengewa kipindi kilichopita.
Hiyo maana yake ni kwamba, bajeti ya safari za nje za Ikulu imeongezeka kwa takriban Sh. milioni 34.

Bajeti ya Ikulu ya safari za ndani ya nchi nayo imeongezeka kutoka Sh. 608,419,000 kwa bajeti ya mwaka 2008/2009 hadi Sh 723,360,000 kwa mwaka 2009/2010, ikiwa ni ongezeko la Sh. milioni 114.9.

Miongoni mwa mambo ambayo Rais Kikwete amekuwa akishutumiwa nayo na wananchi, ni wingi wa safari zake za nje ambapo inadaiwa kwamba zinachota mapesa mengi ya walipakodi; ilhali manufaa yake hayaonekani wazi....

......

Mchanganuo unaonyesha pia kwamba bajeti ya Ikulu kwa ajili ya ununuzi wa mavazi, mashuka na viatu, imepunguzwa kutoka Sh. milioni 127,400,000 kwa mwaka wa fedha 2008/2009 hadi Sh. 116,400,000 mwaka wa fedha wa 2009/2010, ikiwa ni punguzo la Sh. milion 11.


.........

Maofisa katika ofisi hiyo wamepangiwa kutumia Sh 331,270,000 kwa ajili ya safari za nchini, fedha ambazo ni zaidi ya walizopangiwa mwaka uliopita Sh. 273,215,000, kukiwa na nyongeza ya kitita cha Sh. milioni 58.

....

Kwenye mavazi (mfano sare), viatu na mashuka zimetengwa Sh milioni 37.5, ikilinganishwa na Sh milioni tano za mwaka uliokwisha.

....

Kwa ufupi, Ikulu ni moja ya taasisi za serikali zilizoongezewa fedha za matumizi kama ya vinywaji na vitafunio, mambo ambayo yanapingwa na baadhi ya wabunge.

.....................


Source: Bajeti ya safari za Kikwete nje yapaa

Nahisi kuna makosa ya uandishi katika hii habari. Ninavyojua hizo pesa (milioni 115) hazitoshi hata kwa safari moja tu ya JK kwenda nje ya nchi, labda kama anaenda Kenya na kukaa siku 2 na kurudi na si marekani kwa kukaa wiki 1.

Halafu mwandishi anasema milioni 127, 400,000? Hii maana yake ni Trilioni 127.4? Pesa nyingi sana hizi haiwezekani.
 
Last edited:
Hapana Haja ya kushangaa na Pesa hizo maana ndio wao wanapanga na kupitisha vitu vyote na aje na list ya nchi atazosafiri
 
Juni 24, 2009
Mwandishi Wetu, Dodoma

MCHANGANUO wa mgao wa fedha katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2009/2010 unaonyesha kuwa Ikulu imetengewa Shilingi milioni 115 kwa ajili ya safari za nje ikilinganishwa na Sh. mil 82 ilizotengewa kipindi kilichopita...

...hizo ni sawa na USD $ 88,462 tu.

Jambo la kujiuliza zinatumikaje? mfano; Ticket za ndege au gharama za mafuta wakitumia ndege yake, malazi na chakula kwa wote wataokuwa kwenye msafara incl walinzi na wasaidizi wake, allowances nk...
 
Pengine mzee wetu wa kaya atakuwa Vasco Dagama wa Bongo maana huwezi kuongeza mara zote kama hivi
 
Rais J.Kikwete alikuwa waziri wa mambo ya nje; kwa hiyo anajua jinsi gani ya kupata misaada kutoka nje. Ni rais wa kwanza kutoka Africa kuonana na Obama. Halafu hizo hela za matumizi si nyingi sana, kulingalinisha na faida ya safari zake.
 
Back
Top Bottom