Sura-ya-Kwanza
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 568
- 12
Hivi ameshaondoka U.A.E...En route to U of ES EI
AU is footing the bill!
Kula Breki!!!
AU is footing the bill!
Kula Breki!!!
Huo ni uzushi!Umesikia wapi?shirikisha chanzo cha habari!
Nakuunga mkono ka hilo na kwa kuongezea tu, si safari hii tu, safari zote za JK zina maana kwa nchi yetu na nadhani wengi wanalijuwa hilo.
Safari zote za Rais zina maana, may yes lakini za JK zinawalakini fulani Kama mmja ya kazi za rais ni kusafiri then JK hii anaiweza vizuri sana lakini kilio cha wananchi ndiyo kashindwa kukifanyia kazi. Nafikiri kisha gundua akiwa nje anapumzuika kidogo maana ngoma ni zito hajui kuicheza. Alifikiri urais ni rahisi sasa hajui cha kufanya. Mimi simjui raisi yeyeto zaid ya JK ambaye ansafiri kuliko mawaziri wake. Nafikiri hata Ma-PS amewazidi pia.
Mtu mzima mwenye afya tele ndiye mwenye uwezo wa kutimiza majukumu yake vema, yakiwamo yale yanayomtaka kusafiri. Ama ninyi mlitaka awe anakaa pale ikulu afanye kazi kwa remote control? Kumbe wapo wanaodhani tumemchagua rais ati awe "anakaa" nyumba ya magogoni? Si lazima mtu kuwa rais ndipo mtu "akae" ndani ya jengo hilo la ikulu, kule kuna wapishi, walinzi na wasaidizi kibao wote "wanakaa" huko. Kazi ya rais siyo "kukaa" ikulu, ni kutimiza majukumu ya urais popote anapohitajika, ndani ama nje ya nchi. Tumechagua rais achape kazi, siyo "kukaa ikulu"! Anastahili rais Kikwete kupewa hongera na pole kwa kazi, anachapa kazi huyu mtu. Kwa nini hatufikirii kuwa huko anakoenda anachoka kwa kuchapa kazi, badala yake watu mnawaza "matanuzi" tu, kumbe wengine mngepewa nafasi kama hiyo mngekuwa mnasafiri kwenda "kutanua" badala ya kuchapa kazi? Nimeshachoka kabisa na hizi blah blah za kuhoji kila safari anayofanya Kikwete, watu wanaendekeza ujuha na ulimbukeni, pengine hata na chuki binafsi zaidi kuliko masuala ya msingi. Upumbavu mtupu!
...Kwa hiyo uchapakazi wake ni lazima iwe trip za nje ya nchi siyo? Tumewawekea nini basi Mabalozi huko nchi za nje kumbe kila katripu kadogo tu ka 'kununua majani ya chai' Raisi anataka aende yeye? Hivi kulikuwa na ulazima gani wa yeye kwenda Marekani wiki mbili tu zilizopita na kumbe alijua kuwa wiki hii alitakiwa kuwa huko tena??Mara ya mwisho alitembelea lini vijiji kumi mfululizo vya nchi yake? Tutajie faida MOJA tu ambayo wewe kama KITHUKU unaamini kabisa kuwa imetokana na trip za nje zisizokwisha za mheshimiwa. MOJA tu na hatutaki bla bla.Halafu matusi ya nini? huna haja ya kuita unachopingana na wenzio kuwa ni ujuha, ulimbukeni na upumbavu. Mimi nadhani limbukeni ni yule mtu anayependa mtu ama kitu kitu mpaka haoni kasoro za wazi kabisa za kitu hicho na yuko tayari kutukana wenzake kwa hilo. Ni hayo tu mheshimiwa.
Sawa mkubwa. Na faida za kukaa ikulu ni zipi? Faida za kutembelea vijiji kumi mfululizo nchini ni zipi? Na katika faida hizo, ukilinganisha na zinazotokana na "trip za nje zisizokwisha", zipi faida kubwa au za maana zaidi kwa taifa? Kumbuka kueleza pia kipimo unachotumia katika kutathmini "faida" au "hasara" hizo.
Ahamie huko huko US bongo haimfai muungwana...Nchi amwachie Rostamu na Lowassa.
mkuu, hizo ndio blah blah nilizosema. wewe umesema kuwa trip za mheshimiwa
za nje zina faida nyingi
Hivi hamjajiuliza ni lini mara ya mwisho kwa Rais JK kukaa Ikulu for 2 weeks straight bila kuondoka kwenda mikoani au nje?
Heri umaskini wa mali kuliko wa fikra!
Mungu ibariki Tanzania
Hebu onesha mahali nilipotamka maneno hayo, vinginevyo kuwa tu mstaarabu unitake radhi!
Mimi nimekuchagiza ueleze ni kwa nini unadhani rais kutembelea vijiji kumi au kukaa ikulu ni bora zaidi ukilinganisha na "trip za nje zisizokwisha", na unapotoa maelezo hayo utaje kipimo unachotumia katika tathmini hiyo ili na sisi wengine tutathmini halafu tukitumie kipimo hicho tuone kama tutafikia conclusion kama yako. Ni hilo tu na bado hujanipa jibu. Asante mkuu
tuanze na hili la kuonyesha ulipotamka maneo ya faida ya safari za mheshimiwa. Sijapaona. Nakuomba radhi.
Nimeishakupa mfano wa hali inavyokuwa pale mheshimiwa anapotembelea kijiji kimoja tu japo zinaweza kuonekana ndogo mno. Kuhusu hili la kulinganisha na faida za trip za nje zisizokwisha naomba nikuambie hivi.
Kuna mambo mengine yanataka common sense tu na sio lazima kutunga msahafu kuyafafanua. Iwapo wewe Kithuku wakati mheshimiwa anaingia madarakani ulikuwa unapokea mshahara wa shilingi Alfu kwa mwezi na ukaweza kununua sukari kilo moja shilingi mia tano (n9i mfano tu, samahani!), raisi wa nchi yako anaposafiri nje mara nyingi zaidi kuliko anavyokaa nchini unategemea faida za safari hizo zijiakisi katika maisha yako ya kila siku kwa maana ya zitawezesha ile kilo ya sukari uinunue kwa shilingi mia nne ama basi ibaki ile ile mia tano.
lakini iwapo baada ya safari zote hizo, ile kilo ya sukari unainunua shilingi 700 huku thamani ya mshahara wako imekuwa ni shilingi mia nane na sio alfu unayopokea na kila kitu kimekuwa worse off than alipoingia madarakani, ni nini sasa faida ya kutembea kwake nje???
Huu ni mfano rahisi kabisa kuliko yote ninaoweza kutumia ili kufafanua hoja yangu. natumaini utauelewa!
Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi basi tangu JK ateue Baraza lake jipya la mawaziri, baada ya Lowasa kung'atuka kumekuwa na kikao cha baraza la mawaziri mara moja tu!!!
Ndio maana mambo hayaendi kabisa, kila mtu anajiamua mambo yake kivyake, JK yuko bize na safari za nje, yaani kwa kifupi hakai ofisini kama alivyokuwa anafanya Mkapa.
Tunakwenda wapi? Mbona kila kitu shaghalabaghala tu???? At least Mkapa alikuwa mkali kwa mawaziri wake...Msije na issue ya EPA kwenye hili, kwani EPA zilikuwa ni pesa kwa ajili ya uchaguzi ila tu "watanzania wenye asili ya asia" wakaitumia hiyo nafasi kuchota pesa kupita kiasi!!!!
Nimeridhia mkuu, huu ndio ustaarabu, no grudge.
Ukisoma post zangu kuhusu hizi safari za muungwana, utaona ninachosema kimsingi ni kuwa safari hizo ni miongoni mwa majukumu yake kama rais. Sijapata yeyote aliyeweza kunithibitishia kuwa hayo si majukumu yake, ama anaingilia ya wengine, ama anatunga safari zisizo na msingi. Na kufanya kazi pale ikulu na mikoani pia ni majukumu yake kama rais. Lakini sijawahi kusikia kuwa kuna gauge inayoonesha kuwa katika majukumu yote ya rais ni yapi muhimu kuliko mengine, na ni yapi yenye msingi zaidi ama yasiyo na msingi. Ndiyo maana nasema rais anasafiri kutimiza majukumu yanayompasa, sasa kama yupo mwenye ushahidi kuwa anachofanya ni tofauti na hayo aweke hapa tuuchambue.
Kwenye tathmini ya mafanikio ya rais, kupanda ama kushuka kwa uchumi nk, bado hatuna tathmini huru inayoweka mahusiano (causal links) baina ya ufanisi wa kiuchumi na kazi mojamoja anayofanya rais, kwa mfano je alipotembelea Manyara au alipoteua makatibu tawala wapya imechangia kiasi gani kwenye uchumi, hatuna ripoti hizo kwa hiyo hatuwezi kuhukumu. Na hata atakapomaliza muda wake wa urais, ikatokea kuwa uchumi umepanda au umeshuka kuliko wakati alipoingia, bila tathmini huru hatutaweza kusema ni kipi hasa kilicholeta athari hiyo. Kwa hiyo kwa sasa tumwache rais afanye kazi yake, inapobidi tupige kelele pale anapokwenda kinyume na taratibu, sheria, kanuni na katiba ya nchi.