Mimi huwaga napenda tusijadili wingi wa safari... nadhani tujadili safari ipi ya Mh. Rais haikuwa/haina/haitakuwa na umuhimu. Ni muhimu pia wakati tunajadili tusijekumpa Rais majukumu ya Waziri Mkuu!
1. India - Muhimu (Kama mwenyekiti wa AU, kama hamuitaki hii safari,,, mungekataa asiwe Mwenyekit wa AU). Kwa maana nyingine tatizo sio safari bali kuwa mwenyekiti wa AU.
2. China - Muhimu (Mahusiano ya Kiuchumi na China ni muhimu kwa taifa letu, Nimesoma biashara kati ya TZ na china imekuwa kwa asilimia 48.x kati ya 2006 na 2007 iko kwenye... mil. 800$ kwa mwaka kama sikosei.)
3. Zambia - Muhimu (Mahusiano yetu na Zimbwabwe, SADC)
4.Marekani; mimi sijui anaenda kufanya nini? Tukijua anaenda kufanya nini? Ndio tuta-hukumu; zaidi ya hapo... itakuwa ni ile saratani ya kitaifa ya kutojadili hoja, badala yake kujadili watu...
5. Analogy; Nikimfananisha Rais wa Nchi kama CEO wa Kampuni, sioni tatizo la Kikwete, CEO anaye-delegate shughuli zake vizuri hana sababu ya kutotembea na kuona wengine wanafanya nini? Anaenda kwenye masoko n.k. CEO yoyote ambaye anafanya kazi za COO ni CEO ambaye hawezi kuwa-successfull!
Katika nchi kama ya kwetu,, COO ni Waziri mkuu, ndiye mwenye kufanya shuguli nyingi... sio CEO...
6. Nachelea kuamini kwamba Rais wetu angekuwa anaenda kupiga bla bla bla... isingekuwa rahisi kwake kupewa mialiko na mataifa hayo makubwa... unless tuseme anajialika mwenyewe....