Rais Dkt. Magufuli kwa Kauli hii sikubaliani nayo na sikuungi mkono pia kwani ina Viashiria vyote vya Dharau na Jeuri pia

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
" Marehemu alipofikia muda wake wa Kustaafu nilimuomba aendelee kwani sikuona wa Kumrithi. Na mpaka hivi leo ametutoka duniani ama hakika atanipa Kazi ya ziada kumpata Mbadala wake ", alisema Rais Dkt. Magufuli.

Tusidanganyane hapa duniani hakuna Mtu ambaye hawezi kuwa bora kwa Mwenzie hata kama ikitokea amefariki au amestaafu au amefukuzwa Kazi.

Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli sasa kwa Kauli yako kama hii ikitokea utakayemteua akiwa bora kuliko Marehemu utatuambia nini tena? Je, utaenda Kufukua Kaburi la Marehemu na kumchapa Vibao kwa kumwambia kuwa kumbe alikuwa hana lolote na alikuwa anakuchelewesha tu?

Mbona hata Wewe ( Mheshimiwa Rais. Dkt. Magufuli ) muda wako wa Kustaafu ukifika au ukiwahi Kuungana na Israeli kwenda Mbinguni ( namaanisha Kufa ) bado nina uhakika Tanzania tutapata Rais mzuri tu kuliko Wewe na huenda pia akatufanya hata tukusahau tu upesi?

Umeshauriwa sana uwe unazipima Kauli zako uwapo katika Hadhira lakini kwa bahati mbaya mno umekuwa Sikio la Kufa ( siyo Msikivu ) na hushahuriki pia Kiasi kwamba unatupa Maswali mengi zaidi juu yako.

Najua utaninunia ila badilika sasa JPM.
 
ila hayo mbona ni maneno ya kawaida sana mkuu tena hasa pale unapotaka kuonyesha umuhimu wa alietangulia na huenda alikua bora kweli!

Lakini kuna ukweli huu mchungu pia...

Kwamba, kuna "kawaida" zingine ni mbaya zinastahili kuachwa kabisa...

Wizi au uasherati au uzinzi wengi husema ni "mambo ya kawaida kwa binadamu"...

Swali ni hili;

Je, ni " kawaida" njema? Ni " kawaida" inayokubalika..??
 
Alikuwa anajaribu kuelezea umuhimu na mchango wa marehemu kwa taifa...Mzee Chemistry ilikuwa inaendana na kijazi,mbaya mbovu halafu Kijazi hakuwa anamuogopa Mzee alikuwa anamshauri vzr SAA zingine Mori zikiamka kwenye tumbua tumbua.....sijaona shida sema kuna watu mnamchukia Mzee hata afanye Zuri gani hamtaongea.
 
Kwani we nani...ukubaliane au usikubaliane na kauli,hii haimpi shida....mbona nyie wengine mnajipa hadhi kubwa wakati hata jina lako halisi umeshindwa kuliweka....umeweka A.K.A hapo All rounder kujificha.
Kama ID yangu hii ya All - Rounder unaipenda basi ichukuwe Wewe Ndugu na Mimi nitaanzisha nyingine ambayo itabamba ( itakubalika ) vile vile hapa JF.
 
Mbona hata Wewe ( Mheshimiwa Rais. Dkt. Magufuli ) muda wako wa Kustaafu ukifika au ukiwahi Kuungana na Israeli kwenda Mbinguni ( namaanisha Kufa ) bado nina uhakika Tanzania tutapata Rais mzuri tu kuliko Wewe na huenda pia akatufanya hata tukusahau tu upesi?
hapa umemaliza kazi, hata akifa leo, watakuja superb 1,000,000,000,000,000,000 times kuliko yeye
 
Alikuwa anajaribu kuelezea umuhimu na mchango wa marehemu kwa taifa...Mzee Chemistry ilikuwa inaendana na kijazi,mbaya mbovu halafu Kijazi hakuwa anamuogopa Mzee alikuwa anamshauri vzr SAA zingine Mori zikiamka kwenye tumbua tumbua.....sijaona shida sema kuna watu mnamchukia Mzee hata afanye Zuri gani hamtaongea.
Absolutely Rubbish....!!!
 
Back
Top Bottom