Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Ni kuongeza gharama za kuhamia. kujenga. Tanzania hatuna tatizo na Dodoma tuna matatizo yetu mengi tu
 
Hii ni tetesi, dodoma kamji kamebana sana, vituko vyao vitakua hadharani, sidhani kama watakwenda kweli
 
Kama ni kweli, huo nao utakuwa ni ukurupukaji na sioni akifanikiwa katika hilo.

Dodoma haiko tayari kuwa mji mkuu wa nchi.
 
Ataishije dar wakati dsm wamekataa unyumbu.Jiji karibu lote wana limiliki Ukawa?Mwana chato ameona hawezi kuwa chini ya Halmashauri za ukawa.

Akili hizi jamani! Ukute na huyu ni baba watoto wa mtu! Pathetic!
 
Nimepewa tetesi kuwa Rais Magufuli kakataa kuishi Dar na ameagiza kuhamishiwa Dodoma yalipo makao makuu ya nchi.

Mlio jikoni tupeni uhalisia wa hili.
Itakuwa ni jambo zuri sana mtu anaweza asinielewe lakini ikiwa serikali kwa maana ya rais wizara, itakuwa ni njia mojawapo ya kupunguza tatizo la msongamano wa magari hapa jijini.
 
Na makamu wake ahamie huko pia ili iwe rahisi kuendeleza kilimo cha ubuyu...
 
Ongera Sana Rais, Utakuwa Umevunja Mfupa Uliowashinda Wengi. Utakumbukwa Sana Na Watanzania
 
Ujanja ujanja tuu wa CCM watu tunasuburi kazi sipo porojo tuu mara atembelea muhimbili,mara sijui ashtukiza bank kuu.come on ..tunataka mambo ya misingi..Ahamie Dodoma ???? Ni ngumu kuliko alivyobebwa na kuingia Ikulu...

Chochote huanzia mwanzo! Tumuombee Mungu ili hayo unayo yaomba na tunayo yaomba sote ayatekeleze kwa vitendo! Kote huko alipopita kumeonyesha mabadiliko, tayari vifaa tiba vimeshaanza kurudi na wagonjwa wanatibiwa....asingenda je?

Hivi inawezekena utembee na mtu leo leo na apate mimba leo leo na kisha ajifungue leo leo? Tumwachie nafasi kidgo
 
jizi ni jizi tu hata likijichoma moto mwenyewe..
 
Kama ni kweli, huo nao utakuwa ni ukurupukaji na sioni akifanikiwa katika hilo.

Dodoma haiko tayari kuwa mji mkuu wa nchi.

Mkuu nasikia Trumpu akipata ujiko atawafukuza wahamiaji .... .. vipi utapona kweli? Au mwenzetu na uraia ulisha uza?

Huwezi kukurupuka na maamuzi, JPM alipima nini anataka kuwafanyia Watanzania hata kabla Jambo Forums haijaanza, tayari ana malengo yake sisi tuendelee tu hapa kupiga soga lakini JPM anafanya kazi. Hilo ndio la muhimu na matunda yake hata watoto wako watayafaidi. Ni uamuzi kumsaidia au kupiga tarumbeta ambazo ziliongozwa na JS lakini yeye sio chaguo na hakujipanga katika maamuzi yake. Aliyejipanga ndio rais wa 5 wa JYMWT.
 
Mkuu nasikia Trumpu akipata ujiko atawafukuza wahamiaji .... .. vipi utapona kweli? Au mwenzetu na uraia ulisha uza?

Kwanza, haitwi "Trumpu". Ni [Donald] Trump.

Pili, ni ama umesikia vibaya au una matatizo ya kusikia kwa sababu Trump hajasema kwamba atawafukuza wahamiaji.

Yeye alichosema ni kwamba atakula sahani moja na wahamiaji haramu.

Sasa, kama mtu si mhamiaji haramu una nini cha kuhofia.

Kwa taarifa yako, hata Tanzania huwa inawafukuza/ ondoa wahamiaji haramu. Kwa hiyo, hilo si jambo geni kabisa hapa duniani.

Jaribu tu hata kwenda Kenya kiharamu halafu ukamatwe uone watakufanya nini.
 
Back
Top Bottom