Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Hizo ni mbinu za kumfanya Rais ashindwe kutekeleza kauli mbiu yake ya hapa kazi tu.atawajibishaje wazembe akiwa mbali na ofisi za serikali na hata kubali. Ikulu kusafishwa ni kawaida na mara nyingi Waziri mkuu huapishwa Dodoma!
 
Dodoma haikuichaguliwa kwa sababu ya cold war. Dodoma ni katikati ya Tanzania. Ni rahisi kwa mtu kusafiri kutoka Kigoma, Iringa, Mwanza kwenda Dodoma kuliko Dar-es-Salaam. Wanigeria walipoamua kujenga Abuja walikuja kuangalia plan za Dodoma na wenzetu kwa sababu ni serious wakajenga na wakahamia. Sijui ni kitu gani kilichochelewesha kuhamishia serikali Dodoma hasa baada ya Mwalimu Nyerere kustaafu. Serikali ikihamishia shughulli zake Dodoma na kuacha Dar-es- Salaam kuwa mji wa biashara itasaidia sana msongamano wa magari saa za kwenda kazini. Haihusiani hata kidogo na cold war.
mkuu umesema vizuri hasa hili la kupunguza msongamano
 
Wazo zuri lakini nahisi utekelezaji wake kwa sasa ni mgumu mno.

Akihama yeye lazima wizara zote zihamie Dodoma. Maana yake kutahitajika pesa nyingi sana. Anahitaji pesa hizo kwenye elimu, afya na miundombinu.

Umesomeka Mkuu.Hakuna jambo la ajabu kuhamia Dodoma Mzee Kawawa alihamia Dodoma alipokuwa Makamu wa Raisi na Waziri mkuu miaka ya 70.Nakumbuka wakati ule nia haikuwekwa wazi, wabunge walipinga sana japo mwisho walisalimu amri. Lakini Mwalimu Nyerere akiwa Raisi hakuhamia ingawa yeye ndio aliyekuwa mstari wa mbele kuhamasisha serikali ihamie Dodoma.Kwa kipindi hiki sio Kipaumbele.Majukumu ni mengi ni kuongeza mizigo isiokuwa ya Lazima na hakuna utashi.
 
Hahahaaa, sawa Bana. Labda kwa kuwa ulikuta Wanyamwezi wenzio kibao huko Mami. Kama DC inafaa, Dom pia inafaa.

Bachonga Magembe benekele kabisa kabisa, Kabadi....



Hii dansi ingefaa itumike mashuleni kama P.E.
 
Last edited by a moderator:
Sio kweli watanzania kwanini mnapenda sasa tetesi? Msiwe Na haraka ila atahamia chato kwanza
 
Wanaukawa mtampenda na kumfagilia kwa lipi?
1.kwa kuleta nidhamu ya matumizi ya pesa za umma
2.kusimamia fikra ya uzalishaji mali
3.kukekemea ufisadi kwa vitendo
4.haja ya kuwa na taifa lenye Afya,Elimu na miundo mbinu kama mtaji wa maendeleo
 
Kama gazeti linavyosema hapo chini kwamba Wizara tano kuhamishiwa Dodoma Mji Mkuu hivyo ni dhahiri kabisa kwamba Magufuli wetu amedhamiria kwenda hatua KUBWA zaidi mbele kwenye hili swala la kuhamia Dodoma!

Safi sana Magufuli wetu, haya ndiyo maamuzi magumu!

DSC02968.jpg
 
Safi sana. Kati ya hizo tano, TAMISEMI lazima iwepo. Nyingine ni Elimu, Hizo tatu zingine changieni ninyi
 
Ili kuleta maendeleo ya haraka Mikoani, wizara hizi zingetawanya nchini kote mfano:
1. Nishati na Madini ingepelekwa kanda ya ziwa huku kitengo kikuu cha nishati kikiwa kusini i.e Mtwara au Lindi
2. Kilimo na ushirika ipelekwe Nyanda za juu Kusini
3. Utalii iende Kaskazini i.e Kilimanjaro au Arusha
4. Wanawake jinsia na watoto ipelekwe Singida au Dodoma
5. Waziri mkuu yote iende Dodoma
6. Afrika Mashariki haina umuhimu iwe chini ya wizara ya mambo ya nje
7. Mambo ya Nje Dar
8. Fedha na Uchumi Dar


Nitaendelea
 
Ili kuleta maendeleo ya haraka Mikoani, wizara hizi zingetawanya nchini kote mfano:
1. Nishati na Madini ingepelekwa kanda ya ziwa huku kitengo kikuu cha nishati kikiwa kusini i.e Mtwara au Lindi
2. Kilimo na ushirika ipelekwe Nyanda za juu Kusini
3. Utalii iende Kaskazini i.e Kilimanjaro au Arusha
4. Wanawake jinsia na watoto ipelekwe Singida au Dodoma
5. Waziri mkuu yote iende Dodoma
6. Afrika Mashariki haina umuhimu iwe chini ya wizara ya mambo ya nje
7. Mambo ya Nje Dar
8. Fedha na Uchumi Dar


Nitaendelea

Hizi ni ndoto zako ama ndio mipango ya Magufuli?
 
Nchi ishafunguka vya kutosha, wizara zote zinatakiwa zihamie Dodoma even raisi mwenyewe ahamie Dodoma kasoro wizara ya fedha!
Ila kabla ya yote uwanja wa ndege wa Dodoma ule mpya ujengwe then ndo wahamie Dodoma
 
Kutawanya wizara si busara na juzi nilimsikia prof mmoja akisema hivyo, kuna baadhi ya wazara mambo yanaingiliana mfano mambo ya ndani inaingiliana na wizara nyingi sasa kama zitakuwa zimetawanywa hamuoini itakuwa gharama kwa mtu kwenda hizo ofisi. Mfano mwalimu anashughulikia anataka Passport(Uhamiaji) na anataka ruhusa(Elimu/Tamisemi).

Mimi ningedhani kuwe na Governemnt Village ambapo wizara zote zinakuwa jirani jirani kama ilivyo UDOM na colleges
 
Back
Top Bottom