hivi ccm unawajua kweli wewe ?
Na wewe CDM unawajua?
Two wrongs dont make a right, CDM wapeleke mkanda wa ushahidi polisi, wanaweza kutoa copy na wao wakabaki na yao kama woga ni wahusika ku-edit original copy kufuta ushahidi.
Watu ambao walikuwa wakwanza ku-publish Mwangosi alipopigwa bomu leo hawataki kutuonyesha ushahidi kamili wahusika waonekane zimebaki hadithi. Hivi CDM na siasa zao za kutafuta sympathy wangeacha kweli kuweka ushahidi wote kama wanao maana wao kwa kupenda kuonewa huruma si ndio design yao.
Jamaa anadai yeye alikuwa ni mwana-ccm damu mpaka hapo, bomu limerushwa mbele, katika umati ina maana watu waliokuwa mbele ndio waliofika mapema kwenye mkutano ule. Sasa tena kada wa CCM ana amka asubuhi na mapema yeye mwanawe kwenda kusikiliza chama cha upinzani, wewe ni CCM unamfundisha mwanao kuipenda CDM umeona wapi?
Halafu acheni hadithi amna mtu anaeweza kuhujumu CDM kwa sasa, kama kuna watu wanania hizo ni kwa sababu viongozi tu hawako stable au kuna baadhi ya viongozi wenye njaa zinawasumbua na kupokea rushwa. Hila chama chenye mikakati yake ambayo wanaifanya kama kawaida kinahujumiwa vipi umewahi kujiuliza hilo.
Kuhujuumiwa ina maana viongozi wako hawawezi fanya kampeni zao, wanafungwa, media zenye kutoa habari zenye sifa za chama zinafungiwa (tofautisha sio zinazo andika habari za udaku na kushindwa kupeleka ushahidi unapo ombwa), serikali ina freeze asset za chama, yeyote anaetoa support ya fedha kwenye chama lupango, viongozi wao hawaruhusiwi kutoka nje ya nchi kuongea na wafadhili wao kisiasa etc to do with hindering the party plans. CDM wanahujumiwa vipi hapo?
Ndio kuna watu hawana nia njema na CDM sikatai pengine kwa maslahi ya wachache, lakini kwa uhuru walionao CDM ukizingatia na vyama vya siasa nchi nyingine they are pretty much running their own show, tunayoyasoma largely ni uongozi mmbovu au watu wachache wenye maslahi binafsi, lakini CDM amna anaeweza kukihujumu kutokana na uhuru waliokuwa nao ndani ya nchi ni uongozi wa ovyo tu.