usiwe mtumwa wa buku 7 shirikisha ubongo wako hapo mara chacheHizi ni ngonjera za kipuuzi sana. Kwa nini mnahangaika na mariwaya wakati mwenyekiti wenu anasema kuwa anayo CD inayoonesha waripuaji wa bomu pale Soweto?
..
....Ninaweza kunusa kitu hapa!!!
stay tuned hapa hapa!!!
Huyu hana lolote, ni mpuuzi tu amekuja kusikilizia moto wa bomu la Soweto ukoje. Mkuuyakaya Kamwambie Mwigulu time'll tell.
Tutamkamata akiwa hai na ataonja kila harufu ya maumivu hapahapa Ar kama mlivyokuja kuuwa watu hapa.
Na LAZIMA AUWAWE KAMA ALIVYOUWA.
Ook, sasa labda nikuulize swali.
Wewe umeamua kuingia kwenye battle ground kwa sababu mtoto WAKO TU( nielewe vizuri) alikufa??
mkuu unamuomba rais aunde tume wakati yeye ndiye aliyewatuma kufanya kampeni chafu dhidi ya CHADEMA,
ila pia mwenyekiti wa CHADEMA lazima afanye kitu kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, hili suala ni nyeti na halivumiliki hata kidogo
Mkuuyakaya, ni kwanini wewe ulivyoona haya mambo sii sahihi hukuripoti hili suala polisi au kutoa alert even hata JF kama @mwigulunchemba alivyokuwa anawaagiza kwamba msifike kwenye huo mkutano wa CDM wa kufunga kampeni??
Huyu ni mtuhumiwa na 1 kwakua ameamua kusema mwenyewe, kamwe tusidhani ni mtu mzuri tangu tukio kutokea mpaka hivi sasa muda gani umepita? Huyu alikuwa na uwezo kurahisisha kukamatwa kwa waarifu na kama si kuzuia kabisa, maana alikua na taarifa ya jambo baya kutokea, kwanini hakulipoti polisi au kama hakua na imani nao angelipoti hata kwa viongozi wa chadema. Angekua mzalendo wa kweli kwavile alishindwa kuripoti kabla ya tukio, angefanya hivo mara baada ya tukio kutokea. kama kweli na watanzania wenzake waliopoteza maisha, na wengine kupata vilema vya maisha alikua wapi muda wote wa miezi 6. Je asingahama CCM, na Mwigulu kuandika mada ya kujitetea tungeajuje haya, mimi kwangu mtoa mada hii nae anahusika moja kwa moja na mauji haya, na anaswa kumatwa kama mtuhumiwa maana nae alishiriki kupanga mauji hayo.
Mkuu maji yaliyotulia ni ngumu kujua kina chake. Timbwili nililolianzisha Elerai ccm wote wanalijua, na kunidhuru wanaogopa maana Mbunge wangu nilishampa hii taarifa na polisi nilisharipoti. Sasa kwakuwa Nchimbi kapigwa chini hakuna aja tena ya mimi kuremba na ndio maana head title nimeandika "RAISI ANISUKUMA NIPIGANE VITA"
Sipigi tena vita baridi sasa nimeamua kujitupa on Batle ground.
Mhe. Lema mbunge wa waathirika tikio hili, nakumba ukafungue kesi shahidi na 1 ni huyu anaejiita mkuu kaya hapa, pamoja bandiko lake hapa jukwaani. Nae mwenyewe akiwa mmoja wa walioshiriki mauaji hayo, alishiriki kikao cha kupanga mauji na akaamua kukaa kimya, na hata baada ya mwanae mwenyewe kuuwawa kwanye tukio lile. Leo damu imemrudia amekuta anaeleza kujua anachokifanya, alishondwa kuripoti polisi labda hakua na imani nao lakini hata kwa kiongozi yeyote wa CDM. huyu tusimuone kama mtu mwema kamwe, anatafuta pa kujificha na uzuri amekohoa peleka mahakani ataje wenzie wote waliohusika na mauaji. Huyu hafai mwanachama/kiongozi wa CDM, maana jambo hatakama ni baya ilimradi anasilahi nalo analinyamazia bilakujali litawaumiza wengine Mhe. Lema.
Kafungue kesi mahakamani mnataka tume ya nini tena mtumie fedha za walipa kodi. Mashahidi si wapo mbona watanzania tukuwa kama vile akili zetu ni za kuazima na hatujui haki zetu?Natumai Sikuku ya X-mas ilienda vizuri na leo hii tupo pamoja katika kusukuma gurudumu hilii zito la maendeleo ya Taifa letu wakati tunahesabu siku chache zipite tuuzike mwaka 2013 na Mungu akipenda tuuanze mwaka 2014.
Wana Jf siku mbili zilizopita Mh. Mwigulu Nchemba alileta post yake ya utetezi humu ndani na mimi niliichachinga kwa kueleza maumivu yaliyo ndani ya moyo wangu. Na baadhi ya wana Jf walinishauri nianzishe Thread japo halikuwa wazo langu mwanzo.
Mnamo mwezi wa sita mwaka 2013 kulikuwa na uchaguzi mdogo wa madiwani katika baadhi ya mikoa ya Tanzania, Arusha ilikuwa mojawapo ya mikoa hiyo huku ikiwa na kata zipatazo 4 zikirudiwa uchaguzi. Nakumbuka vyama vinne vilijitokeza katika kusimamisha wagombea ila chama cha CCM na CHADEMA ndivyo vilikuwa vikishindana. Kipindi hicho nilikuwa mwanachama wa Cmm na nikimfanyia kampeni kwa karibu mgombea udiwani kwa tiketi ya ccm wa Kata ya Elerai Ndg. Emanuel Laizer.
Wakati kampeni zinaendelea na tunakaribia kufikia mwisho tulipata ujumbe kuwa kuna Mjumbe toka makao makuu ya chama atakuja akiambatana na mawaziri ili kuongeza nguvu na atakapofika tutatakiwa tufanye kikao cha siri ambapo katika kikao hicho tutapewa mbinu na mipango mbalimbali ya kukabiliana na Chadema. Na wajumbe watakao ruhusiwa kuuudhuria kikao hicho ni wale viongozi wa mitaa na watu wanao aminika na chama tu.
Tarehe13/06/2013 siku ya alhamisi saa moja jioni tulikutana katika eneo la chuo kimoja cha ufundi (Help to Selph Help Project )kilichopo Sakina kuelekea Olmatejo, kulikuwa na ulinzi mkali ndani na nje ya chuo hicho na magari yapatao sita hivi aina ya Toyota vx na V8 yakiwa yamepaki chuoni hapo, huku taa za chuo hicho zikiwa zimezimwa zoto isipokuwa taa za chumba cha mikutano tu. Tulipewa tangazo kuwa tunatakiwa tuzime simu zetu na tuzikabizi kwa bwana mmoja ambae alikuwa mlangoni (nafikiri waliogopa kurekodiwa au kupigwa picha) kabla ya kuingia ukumbini.
Tulipo kuwa ukumbini aliingia Mwigulu Nchemba na kuanza kutupa moyo na maelekezo ya mbinu mbalimbali za kikampeni, na muda uliposogea majira ya saa 10:00 usiku ndio akaanza kutoa kauli zilizotuacha na maswali mengi kichwani., namnukuu "Kesho tarehe 14 tutafunga kampeni zetu zote na tuna sababu ya kufanya hivyo, kwa sababu tunazo taarifa kuwa Chadema watafunga kampeni zao tarehe 15 siku moja kabla ya uchaguzi ndio maana tumeamua kufanya hivyo. Pili kila mmoja anatakiwa aimize jamiii yake na rafiki zake kwamba siku ya tarehe 15 wasisubutu kwenda kwenye mkutano wa Chadema na yeyote aliopo hapa asisubutu kwenda na atakae enda kitakacho mkuta tusilaumiane" mwisho wa kunukuu.
Kiukweli sina ushaidi wa picha wala rekodi yoyote inayoonyesha mwigulu akiyasema hayo ila nina wajumbe wanne waliokubali kutoa ushaidi pindi kesi itakapoenda mahakamani.
Kwa kuwa Raisi amemfuta kazi aliyekuwa Waziri wa mambo ya Ndani Mh. Nchimbi, ambae alikuwa mtu wa kaaribu sana na Mwigulu Nchemba ndio sababu hasa iliyonifanya kupigana vita hii na wale waliosababisha na namna yoyote kifo cha mwanangu.
NB:
Mh. Raisi nakuomba uunde tume huru ya kijaji ili mimi muhathirika mkuu na wajumbe waliokuwa katika kikao hicho cha Mwigulu Nchemba tuweze kutoa ushaidi utakaoweza kuisaidia tume hiyo kufanya kazi yake kwa uraisi. Nakuomba sasa Mh. Raisi usikie kilio chetu.
Mkuu Kenwood, kifo cha mwanangu ni sababu hasa iliyonifanya nipigane hii vita, na kiukweli kama mwanangu kifo kisingemfika nisingekuwa na sababu yoyote ya kupambana na Mwigulu kwakuwa angeendelea kuwa kiongozi wangu ndani ya chama.
Ila napenda uelewe wajumbe wote tuliokuwa katika ukumbi wa Chuo tulikuwa tumeenda kusikiliza na sio kupanga jambo lolote maana taarifa za awali tuliambiwa kuna mbinu tunakuja kupewa na sio kupanga.