Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Dr Masaburi ni mkristo kisheria mke halali ni mmoja hao wengine ni hawara tuu


UMENENA....na hata asingekuwa Mkristo hata Muislam kama Mke ni yule ulofunga nae ndoa ya Kidini hao wengine kama hujafunga nao ndoa ni hawara tuu...hawakubaliki
 
Angewaita wana familia ilikua haituhusu usisahau ukamkaribisha kwenye harusi yako
 
Wala hakutek


Wala hakuteleza ila ameisaidia familia. Kama hao wake wapo na walihudhuria hafla hiyo, na watoto pia walikuwepo kwenye tukio hilo, mtu wa baki anawezaje kuwakana sasa, na kwa kutumia mamlaka gani, ambayo marehemu katika uhai wake hakuyatumia?.
labda kaisaidia familia yako kucheka ule udhalilishaji.
Nani kawakana hao wamama aliozaa nao? ukizaa tu na mtu anakua mke wako??
masaburi ni mkristo na kazikwa kikristo, je wakristo wanaruhusiwa kuwa na wake wa 5?
Mkuu wa nchi kwanini ana muhukumu marehemu kwa kuitangaza hii dhambi hadharani?
 
katika hali ya kawaida ni kuwa kwenye misiba mingi madhambi au madhaifu ya marehemu huwa hayawekwi hadharani. hutokea pia hata maradhi yaliyosababisha kifo cha marehemu hayatangazwi.
fikiria kama familia ya marehemu wametangaza kuwa amefariki kwa shinikizo la damu,halafu ajitokeze mtu mwingine na aseme kuwa yeye ni rafiki wa marehemu na anajua kuwa amefariki kwa ukimwi!
hata kama ni ukweli lakini je,huo si udhalilishaji?
Magu ameidhalilisha familia na amemuhukumu marehemu.
 
Padri aliyekuwepo hapo angechukua jukumu la kutozika kidini mara baada ya maneno ya JPM sijui ingetafsiriwaje,nadhani padri aliyekuwepo alikua no mwenye hekima zaidi ndomana akaendelea na zoezi.Muda mwingine watu wajaribu kutofautisha kati ya hekima na ukweli.Ukisoma katika biblia njaa ilipoanguka kwenye nchi aliyokua akiishi Ibrahim na mkewe Sarah,Ibrahim aliondoka na mkewe kwenda mahali pengine yeye na mkewe ili wakajipatie chakula,walipofika mfalme wa eneo like akamtamani make wa Ibrahim na kumwuliza Ibrahim kama Sarah ni mkewe au,alichojibu Ibrahim ni HAPANA.Alivyojibu Ibrahim haukua uongo bali alitumia hekma.Magufuli angekaa kimya angekua ametumia hekima sio kwamba angekua ameshiriki kudanganya,halafu baada ya hapo angetafuta muda akae faragha na ndugu wa marehemu afanye upatanisho.Ibrahim alifanya vile kwaajili ya kuepuka kuuawa na sivinginevyo.Yohana Fungi Mapadlock atakua anaogopeka sasa kwasababu kila akisimama anazua jambo,hii si sawa.
 
Raisi Magufuli anapaswa kuambiwa kwamba watanzania huwa hawaumbui maiti anajuwa nin wanafamilia waliamuwa wasifu usomwe hivyo kwani yeye alialikwa kwamba kutakuwa na ugomvi wao walimsteri yeye kaenda kuingilia maamuzi ya familia ni kosa kubwa kafanye yeye achezee anaga zake za kimadaraka serikali huko atapambana na wananchi mabosi wake kwenye familia aachie mambo ya familia aibu kafanya
 
Ilikuwa sio mahala pake kuzungumza mambo kama yale, mambo yale yamekaa kifamilia zaidi, angetafuta muda muafaka wa kuwakutanisha pande zote then angezungumza yale ambayo alikuwa anataka kuwaambia. Sasa ilibakia watu wanashangilia na kusahau kama wapo msibani!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! si sawa....
 
Dr Masaburi ni mkristo kisheria mke halali ni mmoja hao wengine ni hawara tuu

Na Rais naye ni Mkristu, tena Mkatoliki. Anapoonekana kuunga mkono ndoa ya wake wengi lazima mtu ushangae.

Kwenye masuala kama hayo afadhali asinge comment cho chote.
 
wacha unafiki wewe,
uko tayari kwenye kifo cha baba yako au mama yake mtu aje ashike mic nakutangaza madhambi ya marehemu??

Mkitaka haya yasiwapate muache kuchepuka na muheshimu ndoa zenu, otherwise Magufuli kafungua njia na utakuwa mwendelezo. No more unafiki, kila mtoto ana haki kwa mzazi wake haijalishi alipatikana ndani ya ndoa or not. Hutaki haya yaikuye familia yako, heshimu ndoa yako.
 
wacha unafiki wewe,
uko tayari kwenye kifo cha baba yako au mama yake mtu aje ashike mic nakutangaza madhambi ya marehemu??
Sikuungi mkono, kwenye msiba wa masaburi(RIP) ilionekana wazi kabisa kuwa kuna Makundi tofauti yalivaa sare tofauti, alichofanya jpm ni kuondoa umimi na ubinafsi wa baadhi ya wahusika na si kutaja dhambi za marehemu
 
Naunga mkono
Mkitaka haya yasiwapate muache kuchepuka na muheshimu ndoa zenu, otherwise Magufuli kafungua njia na utakuwa mwendelezo. No more unafiki, kila mtoto ana haki kwa mzazi wake haijalishi alipatikana ndani ya ndoa or not. Hutaki haya yaikuye familia yako, heshimu ndoa yako.
mkono
 
Huyo marehemu alikua bize kuuza uda akasahau kuiweka sawa familia? Magu hajakosea kusema ukweli. Aliekosea ni huyo alieshindwa kuuishi ukristo wake vyema na hadi mwisho inaonyesha hakuyatengeneza.
 
Yule wa zanzibar aliona mbali kutaka akifa kusiwe na mazishi ya kiserikali! Naona sasa viongozi wa serikali wataandika kabisa waraka wakifa wasizikwe kwa utaratibu wa kiserikali!
 
Dr Masaburi ni mkristo kisheria mke halali ni mmoja hao wengine ni hawara tuu
Wananchi hivi kuficha ukweli ni hulka ama mila za sisi waafrika? Niseme tuu marehemu aliishi na wake hao aliowasema Raisi bila kificho na hata kanisa alilokuwa akipata huduma za kiimani lilijua. Kama alikuwa ni Mromani Katoliki...Basi kumbuka sakrementi ya kitubio ya kukili imani yake (mojawapo ni kukili amefanya kosa la kuoa mitala na kamba yeye katika sakramenti ya ndoa ameoa mke mmoja) na kama alifanya hivyo akiwa hospitali basi kulingana na misingi ya kanisa hilo huyo alistahili huduma zote za kiroho katika safari yake ya mwisho hapa duniani. Pili Raisi kama binadamu alizungumza kile ambacho marehemu alikiishi, sasa kama kati yetu tunataarifa kinzani kwamba marehemu hauishi maisha hayo basi na aseme kile kilicho sahihi (hapo utasema Raisi alikosea). Tatu, inawezekana islete mantiki sasa kwa mtazamo wa jumla kwa jamii juu ya alichokisema lakini kwa ustawi wa familia ni muhimu sana kusema kitu ambacho hata jamii nje ya familia wanakijua kuhusu maisha ya familia na wigo wake kwani itawasaidia wana familia kuzingatia ukweli kwamba wao si adui bali ni ndugu wa damu. Nne Raisi wetu Magufuli sio kiongozi wa kwanza kusema kiongozi fulani ana mitala (ameishi na wake zaidi ya mmoja kulingana na dini yake ya kikristo) Kumbukeni kwenye mkutano na waandishi wa habari mwaka 1995 Baba wa taifa hayati Mwl. J.K. Nyerere alisema nanukuu (" Kipindi hicho mwenzangu George Kahama alikuwa ameendelea ana wake wawili") na kiongozi huyu aliweza kusema vile kwasababu sio kwamba alikuwa kiongozi bali alikuwa Rafiki wa mlengwa na hivyo alikuwa na Moral authority ya kuzungumzia kiasi fulani maisha ya jamaa yake kwani yeye amekuwa sehemu ya maisha hayo kwani wameishi kama ndugu, rafiki na jamaa wa karibu. Kwa alilolifanya mheshimiwa Raisi kwa mtazamo wangu kama mwili wa marehemu ulipelekwa kila nyumba ya wake aliokuwa naishi nao na kwenye risala akatajwa mke na watoto wa nyumba moja hapo panatatizo ni bora kulisema ili jamii ikajua ukweli wa maisha ya marehemu.
 
Rais amegonga pale ambapo ni shida sana wengi kutamka. Tatizo ni kubwa, wanaume wanaficha wenzi waliozaa nao, wanawake wa ndoa wanadai wao ndio wana haki, sheria zinanyima haki watoto ambao hawajulikani hata wakijitokeza (labda mtoto huyo awe na tajiri), makanisa hayawataki watoto wa nje, waislamu wanawaita wanaharamu, lakini kwa mila zetu mwanaume akizaa mtoto huyo ni wake, halali.
Kwa hiyo Magufuli alikuwa halali kwa mila zetu za Kiafrika. Ametufungulia njia ya kutambua watoto wetu mapema.
Halafu inakuwaje mtu ambaye hakuwepo wakati mtu anazaa na huyo mpenzi au mke wake lakini anakuwa kimbelembele kumkana mtoto anayejitokeza kuwa ni mtoto wa marehemu.
Iweje ambae hakuwepo awe na kimbelembele kumthibitisha?
 
suala hapa ni kuwa kama familia yenyewe wameamua kuficha aibu ya marehemu ya kuwa na wake wengi ilhali yeye ni mkristo,je ilikuwa ni sahihi kwa mtu mwingine kukanusha na kuweka wazi mbele ya halaiki? kama ilikuwa ni kutaka kutoa ushauri kwa watoto si JPM angewaita faragha azunguze nao?

Sidhani kama ni watoto/wake wote wa marehemu walihusishwa katika kuiandika ile taarifa, kama wangehusishwa si rahisi Kwa mkuu wa nchi kuingilia kati na kusema aliyoyasema. Nikionacho ni kwamba ile familia moja tu yenye cheti cha kanisani ndo iliamua nini kisemwe kuhusu marehemu na kuwaacha wengine wakinung'unika kutofanyiwa haki! Acheni uzinzi, heshimuni ndoa zenu, otherwise thanks Magu kujitenga na unafiki na kusema ukweli. Kweli wewe ni raisi wa wanyonge!
 
Waandika risala wangesema ameacha mke mmoja na watoto 22. Watoto hawakanwi.

Mke halali kikristo ni mmoja tu yule mwenye ndoa. Na maadam hao wengine hawakuolewa nae basi sio wajane wake.
 
Rais kakosea sana, hakupaswa kuingilia swala hilo, hata kama aliona kunasitofahamu kwenye taarifa ya familia hakupaswa kuongelea,angeongelea masuala ya kitaifa tu kuhusiana na Marehemu tu.
 
Back
Top Bottom