Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Nicodemas Tambo Mwikozi

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2016
Posts
663
Reaction score
1,047
UKIJIONDOA KTK MSAFARA UTAWEZA KUIELEWA DHAMIRA YA MANENO YA MH MAGUFULI KTK MSIBA WA MASABURI

Magoiga SN-Mwanza

Yeyote aliyezaliwa katika ndoa za mitaala atakuwa amemuelewa sana mh Rais na hususani ushauri wake kwa familia ya marehemu masaburi.

Watu wengi wamenifuata Inbox kutaka kujua ni nini mtazamo wangu kuhusu hili suala. Wengi wameonyesha kulalamika na kumlaumu Mh Rais kwa maneno yake aliyoyasema msibani. Kwa kuwa ni vigumu kumjibu kila mtu inbox kuhusu mtazamo wangu ktk hili, naomba nitumie fursa hii kukushirikisha ili tuweze kutafakari pamoja.

i) Kwanza kabla ya mazishi, ulizuka mvutano mkubwa sana kuhusiana na wapi mwili wa marehemu uhifadhiwe. Kila familia ilitaka mwili ufikie kwao. Mvutano ulikuwa mkubwa sana kila familia ikitaka japo mwili ukalale ktk familia yao mara moja mara moja kabla ya kuzikwa. Hivyo mwili wa Marehemu ulipitishwa kila familia. Je unalijua hilo??

ii) Kwanza Mh Rais aliongea yale maneno kama rafiki wa familia, aliyeijua vyema familia ya marehemu na kama mtu ambaye asingependa siku za usoni familia ile ikaingia ktk mgogoro mkubwa.

iii) Kuna mahala aliwaasa vijana/watoto wa marehemu kuwa, wakishikamana wataweza kuwaunganisha mama zao. Alisisitiza mshikamano maana alijua kuna shida mahala na inaweza kuleta shida siku za usoni.

iv) Ushauri unaotolewa mbele ya marehemu unaweza kuwasaidia sana watoto na familia inayobaki ktk kujitafakari pale panapohitaji kufanya hivyo.

V) Sote tunajua, mzee wa familia anapofariki mambo mengi huenda kombo, familia huparaganyika kutokana na kugombania mali, mgawanyo usio sawa nk. Hususani ktk hizi ndoa za kimila

vi) Katika ndoa za mitaala Afrika, familia yenye financial power ndiyo inayohodhi kila kitu ikiwemo haki ya mazishi, usimamizi wa mirathi nk

MR RAIS ALIKOSEA AU ALIKUWA SAWA??

Hilo swali sina jibu lake maana kusema alikosea au alikuwa sawa inategemea sana uwezo binafsi wa mtu mmoja mmoja ktk kuitumia vyema akili yake kulitafakari suala hilo. Hivyo nitakachokifanya ili kulijibubswalinhilo, nitkuuliza mswali yenye mwongozo ili utumie muda wako kuyatafakari na kulijibu swali hilo kadiri ya uelewa wako

Akili ndogo hulalama badala ya kujihoji. Hivyo badala ya kubaki ukilalama ni vyema ujaribu kuyatafakari maswali haya ili uoate jibu iwapo Mh Rais alikuwa sawa au hakuwa sawa

i) Je ni kweli masaburi alikuwa na mke mmoja pekee?? Nini tafsiri ya Mke, na ndoa.

iii) Je ni kweli alikuwa na watoto 5 pekee?? Nini tafsiri ya watoto??

iv) Je ktk familia zetu za Kiafrika kuna wakati baadhi ya watoto hukosa stahiki zao pindi mzazi anapofariki?? Taja mazingira ambayo yamekuwa yalisababisha watoto na wajane kukosa stahiki zao

v) Kama alikuwa na watoto zaidi ya 20, na wake zaidi ya 4. Ila wanaotajwa ni mke mmoja na watoto 5. Unategemea kutakuwepo na amani ktk familia hiyo baada ya marehemu kuondoka?? Au tutegemee magazeti kuanza kuripotinkuhusu mgogoro wa kugombania mali za urithi nk?

#My_Take Kuna wakati mtu unahitaji kuondoka ktk msafara wa Nyumbu ukae pembeni ndipo unapoweza Kuyaona mambo ktk mtazamo tofauti 'in a different perspective'. Bika hivyo, utakiwa unawaza kinyumbu nyumbu kwa kutegemea akili ya anayeongiza msafara wenu
 
Mkuu ameteleza, ameisononesha familia ya marehemu, amewasononesha wastaarabu wote.


Mkuu kwa heshima zote! Hicho unachosema siyo kweli isipokuwa amewatendea haki stahiki mbele ya Muumba.
Je ni uongo kuwa Marehemu alikuwa na Mke zaidi ya Mmoja?
Acheni maisha ya kinafiki. Ustaarabu gani ? Familia ipi imesononeka ile iyojichukulia hadhi ya kuwa watoto halali wa marehemu na wengine kuonekana vijakazi?
 
Mkuu kwa heshima zote! Hicho unachosema siyo kweli isipokuwa amewatendea haki stahiki mbele ya Muumba.
Je ni uongo kuwa Marehemu alikuwa na Mke zaidi ya Mmoja?
Acheni maisha ya kinafiki. Ustaarabu gani ? Familia ipi imesononeka ile iyojichukulia hadhi ya kuwa watoto halali wa marehemu na wengine kuonekana vijakazi?
wacha unafiki wewe,
uko tayari kwenye kifo cha baba yako au mama yake mtu aje ashike mic nakutangaza madhambi ya marehemu??
 
Rais ametumia hekima sana.
Kuliweka wazi mbele ya jamii suala lile kutaibana familia kutenda haki.
Yeye kama rafiki wa marehemu,yeye kama kiongozi mwenzake marehemu,alikuwa na kila sababu ya kuingilia mgogoro na kushauri.
Wanasema ukishakuwa public figure ukubali tu kuwa privacy yako na familia yako haiwezi kuwa asilimia mia tena.
Hata Magu angekaa kimya,huenda siku za usoni tungeshuhudia magazeti yakiandika mgogoro ndani ya familia hii.
 
UKIJIONDOA KTK MSAFARA UTAWEZA KUIELEWA DHAMIRA YA MANENO YA MH MAGUFULI KTK MSIBA WA MASABURI

Magoiga SN-Mwanza

Yeyote aliyezaliwa katika ndoa za mitaala atakuwa amemuelewa sana mh Rais na hususani ushauri wake kwa familia ya marehemu masaburi.

Watu wengi wamenifuata Inbox kutaka kujua ni nini mtazamo wangu kuhusu hili suala. Wengi wameonyesha kulalamika na kumlaumu Mh Rais kwa maneno yake aliyoyasema msibani. Kwa kuwa ni vigumu kumjibu kila mtu inbox kuhusu mtazamo wangu ktk hili, naomba nitumie fursa hii kukushirikisha ili tuweze kutafakari pamoja.

i) Kwanza kabla ya mazishi, ulizuka mvutano mkubwa sana kuhusiana na wapi mwili wa marehemu uhifadhiwe. Kila familia ilitaka mwili ufikie kwao. Mvutano ulikuwa mkubwa sana kila familia ikitaka japo mwili ukalale ktk familia yao mara moja mara moja kabla ya kuzikwa. Hivyo mwili wa Marehemu ulipitishwa kila familia. Je unalijua hilo??

ii) Kwanza Mh Rais aliongea yale maneno kama rafiki wa familia, aliyeijua vyema familia ya marehemu na kama mtu ambaye asingependa siku za usoni familia ile ikaingia ktk mgogoro mkubwa.

iii) Kuna mahala aliwaasa vijana/watoto wa marehemu kuwa, wakishikamana wataweza kuwaunganisha mama zao. Alisisitiza mshikamano maana alijua kuna shida mahala na inaweza kuleta shida siku za usoni.

iv) Ushauri unaotolewa mbele ya marehemu unaweza kuwasaidia sana watoto na familia inayobaki ktk kujitafakari pale panapohitaji kufanya hivyo.

V) Sote tunajua, mzee wa familia anapofariki mambo mengi huenda kombo, familia huparaganyika kutokana na kugombania mali, mgawanyo usio sawa nk. Hususani ktk hizi ndoa za kimila

vi) Katika ndoa za mitaala Afrika, familia yenye financial power ndiyo inayohodhi kila kitu ikiwemo haki ya mazishi, usimamizi wa mirathi nk

MR RAIS ALIKOSEA AU ALIKUWA SAWA??

Hilo swali sina jibu lake maana kusema alikosea au alikuwa sawa inategemea sana uwezo binafsi wa mtu mmoja mmoja ktk kuitumia vyema akili yake kulitafakari suala hilo. Hivyo nitakachokifanya ili kulijibubswalinhilo, nitkuuliza mswali yenye mwongozo ili utumie muda wako kuyatafakari na kulijibu swali hilo kadiri ya uelewa wako

Akili ndogo hulalama badala ya kujihoji. Hivyo badala ya kubaki ukilalama ni vyema ujaribu kuyatafakari maswali haya ili uoate jibu iwapo Mh Rais alikuwa sawa au hakuwa sawa

i) Je ni kweli masaburi alikuwa na mke mmoja pekee?? Nini tafsiri ya Mke, na ndoa.

iii) Je ni kweli alikuwa na watoto 5 pekee?? Nini tafsiri ya watoto??

iv) Je ktk familia zetu za Kiafrika kuna wakati baadhi ya watoto hukosa stahiki zao pindi mzazi anapofariki?? Taja mazingira ambayo yamekuwa yalisababisha watoto na wajane kukosa stahiki zao

v) Kama alikuwa na watoto zaidi ya 20, na wake zaidi ya 4. Ila wanaotajwa ni mke mmoja na watoto 5. Unategemea kutakuwepo na amani ktk familia hiyo baada ya marehemu kuondoka?? Au tutegemee magazeti kuanza kuripotinkuhusu mgogoro wa kugombania mali za urithi nk?

#My_Take Kuna wakati mtu unahitaji kuondoka ktk msafara wa Nyumbu ukae pembeni ndipo unapoweza Kuyaona mambo ktk mtazamo tofauti 'in a different perspective'. Bika hivyo, utakiwa unawaza kinyumbu nyumbu kwa kutegemea akili ya anayeongiza msafara wenu
Kwanza wewe mtoa mada unapaswa utujibu kama Magufuli alisena haya kama nani...je, alisema kama msemaji wa familia au msemaji wa hiyo michepuko ya Masaburi?
 
Rais ametumia hekima sana.
Kuliweka wazi mbele ya jamii suala lile kutaibana familia kutenda haki.
Yeye kama rafiki wa marehemu,yeye kama kiongozi mwenzake marehemu,alikuwa na kila sababu ya kuingilia mgogoro na kushauri.
Wanasema ukishakuwa public figure ukubali tu kuwa privacy yako na familia yako haiwezi kuwa asilimia mia tena.
Hata Magu angekaa kimya,huenda siku za usoni tungeshuhudia magazeti yakiandika mgogoro ndani ya familia hii.

Mkuu ameitia aibu hii familia na amemtanazia marehemu madhambi yake.
 
Mkuu ameteleza, ameisononesha familia ya marehemu, amewasononesha wastaarabu wote.
Mkuu, hii ni 'paradox of virtue' nadhani.
Sasa aliyesononesha familia ni aliyesema ukweli au aliyefanya uongo kwa kuoa wake na kuzaa watoto nje na kushindwa kuwapatanisha wakati akiwa hai!? Mkuu jaribu kujiweka katika nafasi ambayo unamuita mtu kaka au dada na yeye anasema 'wewe sio ndugu yetu' na huwezi kutafuta baba mwingine zaidi ya uliyeambiwa na mama!
 
sijui kama ilikuwa sehemu sahihi japo naamini ndoa za namna ile huwa zinamikwaruzano sana hasa baba kama hajaweka mambo sawa
 
wacha unafiki wewe,
uko tayari kwenye kifo cha baba yako au mama yake mtu aje ashike mic nakutangaza madhambi ya marehemu??
Kipi kibaya, kuyasema yale aliyoyasema rais ili hao watoto wakae vizuri (bila kujali wamezaliwa na mama anae tambulika au la) au kuumfichia siri marehemu na watoto waachane vibaya isipokua wale 5 tu. MAsaburi awe alitubu kwa muumba wake au hakutubu, maneno mazuri baada ya kifo chake hayawezi badirisha chochote kwa Mungu. Nampongeza mhe Magufuli kwa kusema ukweli. Watanzania tujifunze kuusema ukweli hata kama unaumiza, haya mambo ya kua tunasema Fulani alikua mzuri sijui nini, hayatusaidii hata kidogo.
 
Mambo ya familia ni ya familia, Haipaswi kuyaingilia, yanamalizwa katika vikao vya familia au mahakamani na siyo kwa presidential decree!

Wanaosema eti kwa kusema vile kaisaidia familia, kaisaidiaje familia?, kwamba kwa kuwa yeye kasema na kwa kuwa yeye ni mkuu basi familia itatii?

Siyo rahisi kihivyo!

Familia zina siri zake, kuna kubambikiziwa watoto, kuna kuchepukiwa, kuna kupiga talaka kimyakimya

Sasa from no where mathalani mtu aje aseme namjua fulani na fulani nae ni mtoto wa marehemu, wakati labda mtoto yule si wako na ndiyo chanzo cha ugomvi wako katika mahusiano lakini hata hivyo umelifanya siri, hii inakuwa very insensitive kwa msemaji kuyasema hayo!
 
sijui kama ilikuwa sehemu sahihi japo naamini ndoa za namna ile huwa zinamikwaruzano sana hasa baba kama hajaweka mambo sawa
Mkuu hapa NDOA ni moja tu...hao wengine ambao makufuri anaowapigia debe ni VIMADA tu.
 
Back
Top Bottom