Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Rais ametumia Moral authority sio legal authority

Hata kama alichokisema raisi ni ukweli, lakini mahali alipoongelea huo ukweli si mahali sahihi, kwani hio familia haina watu wenye busara ambao mh. Rais kama mwanafamilia angeweza kukaa na kuongelea mambo hayo faragha! Alichokifanya raisi kwenye familia ya watu sio uungwana"
 
Kwa mtazamo wangu sidhani kama issue ni kweli au siyo kweli!!?

Issue hapa inayojadiliwa yeye alisema kama nani wakati familia iliamua kusema tofauti??

Kama rafiki,Mwenyekiti wa CCM,Mkuu wa Nchi,Baba mwenye Familia na raia halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Muumini wa Ahadi ya MwanaCCM ufiti na unafiki kwangu mwiko,Binadamu wote wakp sawa!
 
Amewatia sana faraja wake na watoto ambao hawakutambuliwa awali. Kuna maswala ambayo hayahitaji tafsida kuyaelezea.

Wanao beza ni haki yao kikatiba ila Rais ameweza kuwasemea waliofungwa mdomo kwa kisingizio cha ustaarabu!
 
Yes sasa anazaidi ya wawili je wapigwe mawe mpaka wafe au Imani ya Kristu inatuelekeza tusamehe 7X70?

Niwangapi miongoni mwenu kuwa wa kwanza kurusha jiwe?
hatuwez kumsamehe au kumuhukumu kwakuwa hajatukosea
 
Sikuungi mkono, kwenye msiba wa masaburi(RIP) ilionekana wazi kabisa kuwa kuna Makundi tofauti yalivaa sare tofauti, alichofanya jpm ni kuondoa umimi na ubinafsi wa baadhi ya wahusika na si kutaja dhambi za marehemu
acheni kiherehere kwenye misiba ya watu,
yani watu wakivaa rangi tofauti ndiyo mumzalilishe marehemu??
 
Alikosea sana, ili ni internal affair ya familia,kulikua hakuna 7bu ya kupublish kweny public,kama ni family friend angekutana nayo faragha,
 
Baada ya mazishi ndugu jamaa na marafiki wataitwa kwa ajili ya kikao cha ndani ya familia au koo huku M/Kiti wa mtaa akishirikishwa japo siyo lazima sana ila muhimu.

Muhtasari wa kikao utafafanua kinaga ubaga kuhusu Mali,Mke na Watoto wa marehemu, pamoja na kumchagua msimamizi wa Mirathi wataenda Mahakamani kufungua shauri la Mirathi. Mahakama kwa kushikirikiana na baraza la wazee litajiridhisha kuhusiana na mali, Mke/Wake/,Mtoto/Watoto wa marehemu na kuondoa sintofahamu yoyote iliyopo kwenye familia na kumtambua rasmi msimamizi wa mirathi.

Lakini haya yote yanakamilika baada ya mahakama kutoa muda(notice) ya siku 90 kwenye magazeti na ubao wa matangazo wa ofisi za Serikali ili kuwapa fursa wale wote wenye kila aina ya malalamiko dhidi ya shauri husika ili yashughulikiwe. Haya yote tumejiwekea sisi wenyewe Sheria, Taratibu na Kanuni. Mengine yataongezewa au kusahihishwa na wajuvi zaidi pale wanapoona panafaa kufanywa hivyo.

Hivyo basi, Ndg YULE hakuwa na sababu yoyote ile ya kuongea maneno yale yenye ukakasi na kumpunguzia credibility/PR yake? , Ndg YULE hakutumia busara na hekima kutatua kile anachofikiri ni tatizo!!, Ndg YULE anatakiwa ajitambue kuwa yeye ni Kiranja Mkuu hivyo si kiingiacho bali kimtokacho ndiyo Najisi, Ndg YULE afahamu kuwa "Utapimiwa kipimo kilekile unachowapimia wenzako".

Alamsiki!!
 
Yani watu wataongea mengi sana kumtetea mshkaji...But deep down wote tunajua kuwa IT WAS NOT HIS PLACE TO SAY WHAT HE SAID......Kakosa busara na kutaka sifa za kijinga hata kwenye misiba...Kwani angekaa kimya akaja kuwaita pembeni kuwasuluhisha nini kingeharibika!!?...Oooh yeah, tusingekuwa tunamuongelea hapa ryt?....
 
Rais yuko sahihi kabisa,alichofanya ni kuionyesha familia ya marehemu wajitambue kwamba wako wengi.
Kama inaifahamu sana familia alitakiwa aalikwe kwenye kamati ya mirathi huko ndo aseme ho anaouita ukweli; siyo pale hadharani. Mkuu anatakiwa awe makini na kauli zake.
 
Amefanya jambo la hekima na busara machoni pa watu. Waafrika tumezoea kupeana sifa za uongo pindi mtu anapofarik, laiti tungekuwa tunaambizana ukweli unafiki ucngalikuwepo
 
Kama anaifahamu sana familia alitakiwa aalikwe kwenye kamati ya mirathi huko ndo aseme ho anaouita ukweli; siyo pale hadharani. Mkuu anatakiwa awe makini na kauli zake.
Ndio maana king Solomon asked God for wisdom and not wealth.
 
Yani watu wataongea mengi sana kumtetea mshkaji...But deep down wote tunajua kuwa IT WAS NOT HIS PLACE TO SAY WHAT HE SAID......Kakosa busara na kutaka sifa za kijinga hata kwenye misiba...Kwani angekaa kimya akaja kuwaita pembeni kuwasuluhisha nini kingeharibika!!?...Oooh yeah, tusingekuwa tunamuongelea hapa ryt?....
Aje awapatanishe?
 
Sijaona bays lolote alilozungumza Mh,zaidi kaona mbali kwani kuna uwezekano hao watu wangekuwa na mgogoro mzito kwenye mirathi na huenda wangezuia hata mirathi mahakamani. Tumezidi kuficha mambo na ndio maana hatukubali. Mh kaepusha hata mauaji hapo.
 
hata polisi hukamata mtuhumiwa bali ni mahakama pekee yenye uwezo wa kumtia mtu hatiani,


Kwa maana hiyo bado siyo dhambi bali dhana tu kuwa wake wawili kama vile siyo utamaduni ! Acheni kuwa tenga watoto wa Marehemu na kuugeuzwa kuwa familia isiyo na mzazi(watoto wasiokuwa na Baba). Kunyamaza kwao Muda huu wa Majonzi msiuchukulie kama haki. Big Up Mheshimwa kwa kusema ukweli daima. Haipendezi kushiriki kumsindikiza mpendwa na muda huo uongo kusemwa mbele yako na upatapo muda wa kusema neno usiseme.
 
Back
Top Bottom